Membe ananikumbusha Kolimba

Membe ananikumbusha Kolimba

Mkuu kuna sheria ya cyber crime, unaifahamu vizuri lakini au unaropoka Jamii Forum?, ukiombwa utoe ushahidi wa maneno yako utakuwa tayari kutoa ushirikiano?. Sio Kila kifo kina mkono wa mtu, usipende sana kusikiliza stori za mitaani
Peleka mikwara yako huko ulipolalia , hivi Nchi hii kuna kitu kinaitwa ushahidi? Tokea lini ushahidi ukakubalika mbele ya mwenye pesa? Kombe aliuawa kwa kufananishwa na jambazi tena aliinua mikono juu akajitambulisha lakini bado alipigwa shaba, kama unataka Ushahidi nenda nyumbani kwa Nyerere kawaulize ndugu wa Nyerere watakupa picha A-Z . Kisha kautoe unapotaka wewe.
 
Membe ana hasira katumia pesa nyingi kumwingiza Magufuli ikulu lakini mpaka sasa hajapewa Dili lenye Ulaji ili arejeshe pesa zake.
 
Kuna umuhimu wa kuweka historia ya mambo iliyo sahihi; marehemu Horace Kolimba katika uhai wake alikosoa kuwa chama yaani ccm kilikuwa kimepoteza dira na wala hakuikosoa serikali na ndio maana aliitwa kujieleza mbele ya kamati kuu ya chama!!

Membe kwa upande wake anakosoa kile anachoamini kuwa serikali ya Magufuli haijafanya sahihi; lakini hayo ni mawazo yake ambayo mimi nayaona kama ni potofu. Rais Magufuli ana dhamira ya kupunguza matumizi ya serikali na sehemu ambayo imebainika kuwa ni kubwa katika matumizi hayo ni safari za nje za watumishi wa serikali hivyo kuthibiti matumizi hayo ndiyo ameweka utaratibu wa kuwazuia watumishi bila kusafiri mpaka wameruhusiwa na mamlaka stahiki.

Membe na watu wengi wanapotosha kuwa Rais amekataza watumishi wasifanye safari za nje hilo sio kweli, Rais amekataza watu kufanya safari kwenda nchi za nje bila kuwa na umuhimu wa kufanya hivyo!! Yeye mwenyewe Rais pia atafanya safari kwenda nchi nje pale tu itakapokuwa ni lazima afanye hivyo na wala hajasema kuwa yeye hatafanya safari za nje kama watu wanvyotaka watu waamini.

Sio siri kuwa Membe na genge lake waliwekeza sana kuutaka urais pamoja na kupata msaada wa fedha nyingi toka Libya ; sasa maadam wananchi waliamua kuwa Membe hafai ingefaa akae chini na kufanya biashara ya hotel aliyojenga kutokana na hizo fedha za Gaddaffi!!

Kumlinganisha Membe na marehemu Kolimba ni kutaka kumkweza Membe afikie mahala asipo stahili; Horace alikuwa ni mtu mwenye hadhi ya juu sana!
Membe analilia Ulaji pia ana Machungu sana maana kaiteketeza pesa ya marehemu Gaddafi wa libya kwa ajili ya Magufuli alafu leo hajapewa cheo chochote kile ! Katumwa na wengine awasemee hayupo peke yake yupo na kundi lake wakiwemo akina January makamba na wenzao ambao hawana ubavu wa kuthubutu kusema yaliyopo mioyoni mwao.
 
Magufuli akiugua mafua .. membe umesababisha.. haaa
 
Kwa kadiri nilivosoma story ya Kolimba kumbukumbu zinanieleza Kolimba alikufa kwa kupigwa risasi licha ya kunyoosha mikono juu kuashiria kuwa amesalenda!!

Hiki kisa chako kumuhusu ni kipya kwangu. . hilo tu

BACK TANGANYIKA
 
Awamu hii ya tano utaandika sana!

Utajitahidi kujenga hoja zenye hoja, vihoja na viroja.

Utajaribu kutafuta viunganisho vya hoja hata visivyo na mantiki ambavyo wengine wanasema dots.

Nani amekudanganya kuwepo kwako wakati Kolimba akitamka maneno hayo ndiyo kigezo cha kufahamu zaidi ya ambao hawakuwepo?

Kuleta dots zinazodai Membe anaweza kuwa Kolimba ni absurd to say the least.

Watu wa aina yako ni wale ambao walikuwa wanashangaa kuwaona kina Mzee Warioba wakimpigia kampeni Magufuli huku wakitoa sababu wakisema anasaliti Rasimu yake ya Katiba Mpya bila kujua mantiki ya lesser evil.

Hata pumba kwa wengine wenye fikra fupi huwa ni nguvu ya hoja!
Nina wasiwasi kama umemuelewa The boss.
 
frankly speaking,mleta mada huwa anawazaga mambo ambayo hayapo,basi tu ilucinations zako na poilitics za nyumbani;nimeona sana kwenye post zako nyingi.
Niseme tu,mimi sio fan wa Membe ila nathani kama mwanachama na raia yoyote watanzania anayo haki kuhoji baathi ya mambo sababbu anao uzoefu kwa miaka mingi.
Mimi nathani sidhani kama ni chuki juu ya Magufuli na serikali yake,ndio maana wanaita siasa.Siasa sio ngumi,kuchukiana,bali kupingana kwa hoja.
Zama za kale sio sawa na zama za muda huu.Kolimba kwaa taarifa yako,hakuuwawa na mkapa bali chama.Inasemekana alikuwa mbioni kutoa siri za chama na kuanzisha chama chake na kuchukua baathi ya watu ndani ya chama.Basically,kuua chama cha mapinduzi but who knows.Haya ni ya kusikia tu.
Hivyo,sioni ajabu sana Membe kusema lolote juu ya serikali ya Magufuli.Tusitake kukuuza maneno na mambo ambayo hayamo na kuleta uchochezi kwa mambo madogo sana kwenye jamiii.
Mkuu,wewe ni mtu ambaye nakuona uko so negative sijawahi kuona uko optimistic na kitu chochote.I wish to meet you in person to prove me.Stay positive brother kaka.
 
Membe ni Nyoka wa TISS hawamuwezi.

Mkuu Nchi ina mambo mengi ,umesahau Brigedia Kombe aliyekuwa mkuu wa Kitengo wakati wa Nyerere,akaendelea wakati wa Mwinyi na kufanya na Mkapa akastaafu wakati wa mkapa. Yaliompata alishukiwa eti ameiba gari la Mhindi akamiminwa risasi na kundi la polisi huko Moshi-Arusha."usicheze na Government cheza na serikali"
 
Huy
Membe ni Nyoka wa TISS hawamuwezi.
Hiyo ni moja mkuu Savimbi. La pili hapo ni watanzania waache ujinga wa kuogopa kutoa mawazo yao eti kisa kuna aliyetoa wakamfanyizia kwa ule utaalam wao wa kuweka mambo flani kwenye mike au mambo kama haya. Mimi nakumbuka sana yaliyomkuta Jamaa yule, ila isiwekigezo cha kuwanyima watanzania wa leo kutoa maoni yao kwa kile kisa, No hata kidogo. Kama hoja ina nguvu basi na vigezo vizingatiwe na kama haina mashiko basi mhusika aeleweswhwe wapi kachemka na si KUMLINGANISHA NA MAREHEMU. Tunahisi bila kuthibitisha kuwa yule walimkolimba kiaina maana hata hakumaliza ile hoja yake ya ccm haina dira wala muelekeo, hawakumpa chance ya kuimaliza angalau watz tumuelewe alikua na maana gani. Sasa huyu wa sasa haimaanishi hajui yale mambo yao, najua anajua sana na labda anayo maana yake kusema aliyosema, so why the big boss na mlingano wako huu?? Au ndo unamfundisha uoga??? Kwani JPM ni Mungu asikosolewe??? Kwani unapokua kiongozi ndo unakua more perfect???? Oode mbe.. Kama yule walimkolimba, poa ila alisema kwa kinywa chake na wapo waliomuelewa sana tu, na huyu wakimmembe bado itakua poa tu maana kana watz weengi tu wamemuelewa na kifo chake kitakua changamoto zaidi kwa hali ya sasa.
 
Kwa kadiri nilivosoma story ya Kolimba kumbukumbu zinanieleza Kolimba alikufa kwa kupigwa risasi licha ya kunyoosha mikono juu kuashiria kuwa amesalenda!!

Hiki kisa chako kumuhusu ni kipya kwangu. . hilo tu

BACK TANGANYIKA

Hapana mkuu respect wa boda, aliyekufa hivyo ni mzee Kombe na si Kolimba. Kolimba alifia Dom na Kombe alifia karibu na nyumbani kwake kwa kupigwa risasi ili mambo flani yasitirike.
 
Kama utakataa kukosolewa katika maisha hutojifunza chochote coz no one is perfect

Huu ujumbe unatakiwa umkute JPM direct bila kupitia popote, maana kuna watu wanamwona tayari kama malaika ama Mungu wao kabisa.
 
Peleka mikwara yako huko ulipolalia , hivi Nchi hii kuna kitu kinaitwa ushahidi? Tokea lini ushahidi ukakubalika mbele ya mwenye pesa? Kombe aliuawa kwa kufananishwa na jambazi tena aliinua mikono juu akajitambulisha lakini bado alipigwa shaba, kama unataka Ushahidi nenda nyumbani kwa Nyerere kawaulize ndugu wa Nyerere watakupa picha A-Z . Kisha kautoe unapotaka wewe.
Mimi sijawahi kukuona siwezi kukupiga mikwara, nakukumbusha tu hali halisi ya sasa. Watanzania tunabakia kuamini sababu za ziada za vifo, hata siku moja mtanzania hafi kifo cha kawaida lazima kuna hadithi ndefu nyuma ya kifo chake. Huu unaitwa umasikini wa mawazo.
 
Back
Top Bottom