Young Tanzanian
JF-Expert Member
- Mar 10, 2012
- 1,736
- 293
Joka la mdmu membe atakua anataka aztumie kuhonga apate urais ata za ghadafi naskia kazfcha
Alipaswa kusema 'wizara ya mambo ya nje' sio MEMBE.hili suala limefanywa na wizara,sio Membe binafsi.
Hivi huu Muungano una faida gani?
una faida nyingi,lakini moja tu ndo muhimu tena kwa ZNZ.muungano ukivunjika wataanza kupinduana kama comoro,Tanganyika haitaki kuona hilo kwenye koloni lake.
Leo watu wetu wamefukuzwa zantel wangapi? Rushwa imeifanya kampuni ya zantel kufilisika na itakufa kama inavyokufa nchi ya znz, wallah nakupeni kwa ufupi, kampuni ya zantel ilikuwa na ubia wa WARABU, WAHINDI NA SERIKALI YA ZNZ, WAHINDI WAKATAKA KUIPELEKA ZANTEL TANGANYIKA, WAARABU NA SERIKALI YA ZNZ WAKAKATAA, WAHINDI WAKASEMA TUPIGENI KURA YA MAONI ATAKAESHINDA NDIO ATAFUATWA, WAHINDI WAKAJUWA TUTASHINDWA, BASI WALILOLIFANYA WAHINDI WAKAWAFATA WALE BODI MEMBERS WA SERIKALI YA ZNZ WAKAWAPA RUSHWA KUBWA TU ILI WAUNGE MKONO ZANTEL KUHAMIA DAR, MWISHO WA SIKU KUPIGWA KURA MWARABU ANASEMA NO, WAHINDI NA SERIKALI YA ZNZ WAKASEMA YES, HATIMA YAKE ZANTEL HIYO DAR, NA DAR WANAOIMALIZA ZANZTEL NI TIGO, AIRTEL, VODACOM, WANAWAHONGA WAFANYAKAZI WA KIBONGO KUIYUWA MITAMBO KWA MAKUSUDI ILI KAMPUNI IFE NA ITAKUFA KWA TAARIFA YENU, TUMELALAAAAAA, WATU WANAKWENDA MBELE, UKISEMA UNAITWA CUF, MUWAMSHO, AKILI HATUNA, WALA MIPANGO, SISI TUPO KWENYE SIASA TU, WATU WANAJENGA NCHI ZAO SISI TUPO NA FITNA, HASADA, WAJINGWA WAKUBWA.
Hoja kama hizi mimi huwa nashindwa kujua undani wake make hazina upande wa pili uanweza kumhukumu mtu ukamuonea bure.
Mkuu Nguruvi3 umeandika vyema kabisa kuhusu masuala yaliyoibuliwa. Kuhusu kukalia fedha, Mimi napata taabu kuelewa huyu aliyeandika huko mzalendo. net anakusudia nini hasa. Nijuavyo masuala ya mikopo au misaada ya aina hii yanashughulikiwa na wizara ya fedha/ hazina (masuala ya muungano) na yale ya zanzibar kuna ya uchumi na fedha. Sijaelewa vizuri Membe ameingiaje hapa labda afafanue. Hata kama Membe kama waziri wa mambo ya nje angekasimiwa mamlaka ya kusaini kwa niaba ya hazina sioni sababu na mantiki ya kuzikalia kwani pesa hizo hazitolewi mkononi. Nina wasiwasi, huenda huyu mtu ana chuki binafsi na hawa viongozi wa wizara ya mambo ya nje kwani mbali ya Membe amemvaa naibu waziri Mahadhi kwa mambo ya uzinzi. Leo nimeamini, ni kweli busara ya baadhi ya watu huonekana wanapokuwa kimya. Basi maadam mwenzetu huyu hakukaa kimya ndo hivyo tena.
Kwanza habari za mzalendo ni majungu.
Pili, elimu ya mzalendo.net ni majunguTatu, elimu ya wznz kusoma na kutafuta ukweli ni ndogo.
Naonyesha uongo wa huyu bwana.
1.Membe amewanyima wazanzibar Visa kuhuduhuria vikao vya kimataifa kwa kuwanyima VISA
Wazanzibar visa ya nchi nyingine haitolewi na wizara ya mambo ya nje ya Tanzania.
Kama unakwenda US visa inatolewa na ubalozi wa US kama itakavyokuwa kwa visa ya UK, China n.k.
Kauli hii ni ya uongo na ni wajinga tu, narudi wajinga tu watakaokubali.Ni kauli ya kupuuza sana.
Membe hawezi kutoa visa ya Marekani. Wznz wanaafiki, uwezo wa kupambanua pumba na mchele mhh
2. Wanasema mambo ya nje yaondolewe katika muungano.
Hapa ni kuwa wanataka muungano lakini hawataki mambo ya nje yawe ya muungano.
Halafu anasema znz imeonyonywa na Tanganyika kwa miaka 48 wakati huo huo anataka muungano isipokuwa mambo ya nje.
Wazanzibar kataeni mambo ya nje yasiwe ya muungano, na msiishie hapo kataeni ulinzi na mambo ya ndani pia yasiwe ya muungao. Mkikubali kupewa ulinzi basi mjue na mambo ya nje yatakuwa ya muungano.
Hakuna nusu glasi.
Ulinzi na usalama hamzungumzii kwasababu mnajua ni suala la gharama, ndio utamaduni wa wenzetu, kubebwa rahaaaa mustarehe!
3. Hizi habari za Membe kukalia bilioni 200 zimekuja mwezi mmoja tu na ndio maana BLW wamejawa na ghadhabu na jazba
Huu ni uongo, hawana jazba wala ghadhabu wanafoka tu kwasababu wapo znz wakipanda meli kimyaa!
Juzi walikuwa Dodoma hakuna aliyenyanyua mdomo kusema leo ghadhabu inatoka wapi.
Ukumbi wa bunge la katiba unaandaliwa na wao wameomba idadi iongozwe, ghadhabu za muungano zitoke wapi!
4. Ushirikiano wa kimataifa umeingizwa baada ya sakata la OIC
Hapa ndipo utashangaa kuona wznz wanakubaliana na hili.
Hakuna anayekwenda maktaba kufanya hata kautafiti kasikohitaji fedha
Sakata la OIC limetokea miaka ya 1990 Mwinyi akiwa rais wa JMT.
Katika historia ya nchi hii kwa miaka 48 znz haijawahi kuwa na waziri wa mambo ya nje pekee.
Narudia pekee kwa maana kuwa hatujawahi kuwa na mawaziri wawili.
Kwahiyo suala la mambo ya nje lilikuwepo kuanzia mwaka 1964 kwasababu nilizosema.
Sijui hawa wenzetu uongo wanautoa wapi yarabi. Hata hili la miaka 20 linahitaji elimu kweli?
cc. JokaKuu Jasusi FJM Nonda Mchambuzi Mzee Mwanakijiji
Tena ningependa huo muungano uishe hata leo.Kama kawaida yako Bwa, Muabudu Nyerere....
Tafuta watoto wa chekechea uwafundishe hiyo elimu yako ya Muungano. Sisi hutupati na tunajua ni kinaendelea. Siku za Muungano zinahesabika.
Ha ha ha! FJM wao hawataki muungano, lakini pia hawataki kusimama wenyewe. Woga wakubwa sana hawa!Ushirikiano wa Kimataifa uliingizwa kwenye Muungano baada ya Zanzibar kutaka kujiunga OIC? Nani alikuwa Waziri wa mambo ya nje (Kimataifa) wa Zanzaibar wakati inajiunga na OIC, na uwaziri wake ulikoma lini? Hivi vituko vitaisha lini?
Wazanzibari wanalalamika sana kuhusu kunyonya na kutaka waachwe wapumue, lakini inashangaza hakuna mtu anayetamka wazi wazi Muungano uvunjwe, kwanini? Kwa nini hawawapigi marufuku wabunge wao wasipande boti kuja kwa 'wanyonyaji?
Kwanza habari za mzalendo ni majungu.
Pili, elimu ya mzalendo.net ni majunguTatu, elimu ya wznz kusoma na kutafuta ukweli ni ndogo.
Naonyesha uongo wa huyu bwana.
1.Membe amewanyima wazanzibar Visa kuhuduhuria vikao vya kimataifa kwa kuwanyima VISA
Wazanzibar visa ya nchi nyingine haitolewi na wizara ya mambo ya nje ya Tanzania.
Kama unakwenda US visa inatolewa na ubalozi wa US kama itakavyokuwa kwa visa ya UK, China n.k.
Kauli hii ni ya uongo na ni wajinga tu, narudi wajinga tu watakaokubali.Ni kauli ya kupuuza sana.
Membe hawezi kutoa visa ya Marekani. Wznz wanaafiki, uwezo wa kupambanua pumba na mchele mhh
2. Wanasema mambo ya nje yaondolewe katika muungano.
Hapa ni kuwa wanataka muungano lakini hawataki mambo ya nje yawe ya muungano.
Halafu anasema znz imeonyonywa na Tanganyika kwa miaka 48 wakati huo huo anataka muungano isipokuwa mambo ya nje.
Wazanzibar kataeni mambo ya nje yasiwe ya muungano, na msiishie hapo kataeni ulinzi na mambo ya ndani pia yasiwe ya muungao. Mkikubali kupewa ulinzi basi mjue na mambo ya nje yatakuwa ya muungano.
Hakuna nusu glasi.
Ulinzi na usalama hamzungumzii kwasababu mnajua ni suala la gharama, ndio utamaduni wa wenzetu, kubebwa rahaaaa mustarehe!
3. Hizi habari za Membe kukalia bilioni 200 zimekuja mwezi mmoja tu na ndio maana BLW wamejawa na ghadhabu na jazba
Huu ni uongo, hawana jazba wala ghadhabu wanafoka tu kwasababu wapo znz wakipanda meli kimyaa!
Juzi walikuwa Dodoma hakuna aliyenyanyua mdomo kusema leo ghadhabu inatoka wapi.
Ukumbi wa bunge la katiba unaandaliwa na wao wameomba idadi iongozwe, ghadhabu za muungano zitoke wapi!
4. Ushirikiano wa kimataifa umeingizwa baada ya sakata la OIC
Hapa ndipo utashangaa kuona wznz wanakubaliana na hili.
Hakuna anayekwenda maktaba kufanya hata kautafiti kasikohitaji fedha
Sakata la OIC limetokea miaka ya 1990 Mwinyi akiwa rais wa JMT.
Katika historia ya nchi hii kwa miaka 48 znz haijawahi kuwa na waziri wa mambo ya nje pekee.
Narudia pekee kwa maana kuwa hatujawahi kuwa na mawaziri wawili.
Kwahiyo suala la mambo ya nje lilikuwepo kuanzia mwaka 1964 kwasababu nilizosema.
Sijui hawa wenzetu uongo wanautoa wapi yarabi. Hata hili la miaka 20 linahitaji elimu kweli?
cc. JokaKuu Jasusi FJM Nonda Mchambuzi Mzee Mwanakijiji
Wazanzibari ndio hao wanalalamika, faida hawaioni wanachokiona ni hasara tu. Kama na sisi hatuna faida nao na una hasara tu kwanini tuung'ang'anie?
Kama inabidi uwepo, Serikali tatu. Kila mtu awe huru kufanya maamuzi yake.