Katika hali ambayo inaonyesha dhahiri shahiri suala la mbio za urais ndani ya CCM linampa wakati mgumu Waziri wa mambo ya nchi za nje, Mhe. Bernad Membe amezidi kutoa kauli zenye maswali mengi.
Hiyo imetokea wakati akichukua fomu ya kugombea urais kupitia CCM mjini Dodoma Membe amesema akifanikiwa kuwa Rais atapambana na rushwa kwa kuhakikisha anawaajibisha wapokea rushwa na kuwasamehe watoa rushwa wote ambao watakiri kutoa rushwa.
Kauli ya Membe anaitoa kinyume kabisa na sheria za nchi zinavyosema, kinyume kabisa na sheria ya rushwa nchini ilivyoainishwa kisheria.
Kwa mujibu wa sheria ya PCCA sheria No. 11/2007 section 15 inaeleza wazi kuwa "Anayetoa na kupokea rushwa wote ni wahalifu". Hivi ndivyo sheria inavyosema.
Leo hii Membe anaposema akiwa Rais atahakikisha wanaopokea rushwa ndio watakuwa wahalifu, hii sheria kaitolea wapi? Ni nani amempa madaraka Membe ya kuvunja sheria za nchi zilizotungwa na Bunge? Membe anataka kutuambia akiwa Rais hatafuata utawala wa kisheria, hapo utawala bora utatoka wapi? Bila ya kuwepo mtoaji rushwa, mpokeaji angetokea wapi?
Membe anataka kutuambia atakuwa mvunja katiba ya nchi atakayoiapa kuilinda endapo atafanikiwa kuwa Rais? Ina maana hata zile ahadi zake anaweza kuja kuzipindua na kufanya anayoyajua yeye kwani ameshaanza kutuonyesha dalili za kubadilika mbele ya safari. Hakika huku ni kuchanganyikiwa kwa wazi wazi anakoendelea kuonyesha Membe.
Membe hakuishia hapo bali ametoa kauli nyingine za kuchanganyikiwa wakati akielezea suala lake kuwa na undugu na Rais Jakaya Kikwete.
Membe amesema suala la yeye kuwa ndugu na Rais Kikwete endapo ni kweli au si kweli haliwahusu Watanzania ambao asilimia kubwa wamemjua wakati huu wa kuisaka Ikulu.
Membe ameonyesha wazi wazi kushindwa kukana undugu wake na JK na hivyo kushindilia maneno yanayozagaa mitandaoni ya JK na Membe kuwa ni ndugu wa damu.
Wapo baadhi ya watu wanaodai Baba yake halisi Membe ni Mzee Mrisho Kikwete ambaye alizaa na Cecilia John Membe ambapo kwa kabila la Wamwera uchukua jina la ukoo wa Mama na kulifanya ndio jina la ukoo wa mtoto. Ikumbukwe, Wamwera ni kabila linalofuata matrilenial system ambapo Mama ndiyo mwenye dhamana kubwa na mtoto.
Watu wamefukunyua undugu huo kufuatia kuona jitihada na nguvu za wazi wazi zinazofanywa na familia ya JK katika kuhakikisha undugunization ya kumrithisha kiti cha urais Membe kwa kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya kisultan ya kurithishana madarakani ilihali kuna mfumo wa kidemokrasia.
[/QUO
Wewe dada umeoga? pole kwa kutumika kama ile mipira! ni mtu hatari sana,unaleta mambo ya vijiweni! hayana kichwa wala miguu,hayana impact yoyote kwa taifa, halafu id yako ni fake una id nyingine imetuma uzi!
kwa maslahi ya nani unaleta huu utumbo?
Nenda face book hapa ni akili kubwa tu!