Meena Ally anaharibu kipindi cha Amplifier

Meena Ally anaharibu kipindi cha Amplifier

cheetah255

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2017
Posts
1,382
Reaction score
2,416
Nasikiliza kipindi cha Amplifier top10 countdown kinachorushwa hewani na redio ya watu Clouds FM na nimegundua kimepoteza kabisa taste yake, mvuto na burudani iliyokuwa inatolewa kipindi cha nyuma alipokua anatangaza Millard Ato peke yake.

Hapo nyuma nilijikuta nikifungulia hiki kipindi baada ya mihangaiko kila jioni na kupata burudani murua na kutoa stress pamoja na uchovu lakini baada tu ya huyu bidada Meena Ally kujiunga kipindi kimepoteza mvuto kabisa, amekuwa akimvuruga tu Millard na kumtoa kwenye concentration ya utangazaji.

Yaani anazidisha utani mwingi hadi anajisahau kama yupo kwenye kipindi mara kumkashifu Millard akikosea baadhi ya maneno yakiingereza kwa kejeli, yaani ni vurugu vurugu tu hadi nahisi Millard anachoka.

Huyu dada ni mtangazaji mzuri kwenye vipindi vingine ila kwenye hiki kipindi cha countdown hakuna chemistry kabisa kati yake na Millard.

Meena ana sauti nzuri apewe vipindi vingine hapo mawingu, amplifier anaharibu!
 
Halafu utani wenyewe umekosa ubunifu, kila siku utani wa kuwa anamdai pesa milard hataki kumlipa, each and everyday utani uleule miezi kadhaa sasa utani huohuo. Ikifika wakati anaanza tu utani you can easily predict atasema nini.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hayuko creative kabisa.Millard alikimudu sana kipindi akitangaza peke yake.
 
Kile kidada utoto mwingi sana. Sijui nani alikileta Amplifier? Wakipeleke huko leo tena au kwa kina B12.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Katika vipindi vilivyotulia pale ni hicho cha amplifaya ila ingependeza aendeshe millard ayo pekeyake...maana PB makelele.....LEO TENA makelele....XXL ndio bangi tupu....JAHAZI nao makelele ya kileviii sijui wanakujaga wamelewa pale?,,,ila jahazi ya zamani wakati wa caputaini mwenyewe ilikua poa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom