Media, Tumedhalilishwa!, Tumejidhalilisha!. Ni Matokeo ya Sheria Mbovu, Umasikini, Dawa ni Kuunganisha Habari na UtangazajI, Tulipwe Fungu Nene!.


Umeongea vyema sana.

Kada ya watu wanaogombania buku siyo ya kumshauri mtoto akaisome.
 

They don't value their profession. So no one will value it. And that's why wanaitwa na watu wa bongo movie na kuwarushia elfu moja, elfu mbili etc.

Ukitaka profession yako iheshimike tupilia/ondoa mbali njaa za hapa na pale. Be expensive one hata kama una njaa utaonaunavyoheshimika.
 
 
Maeneo meeeeengi hamna kitu hapo

Bongo taifa la zero
 
Kwa umri wako kumbbe weee ni baba yangu. Waandishi Kanjanja wNadhalilishwa na Uwoya?? duu hii njaakweli, Uwoya mwenyewe ana njaa mpaka kichwani nae kapata vibonde wake. hahahaa
 
Almost 30 years of experience in a single industry an authority and a legend indeed.

But this Uwoya saga is just ‘a fuss about nothing’.
Uwoya alikuwa hana kitu cha kuwapa waandishi wa habari, kuwapa kwa bahasha hata elfu 50 kila mmoja uwezo huo hana, ilibidi afanya mchezo wa kurusha hizo miambili.miambili atakaepata apate atakayekosa akose.
 
Mkuu, imekuwa ni busara kwako angalau kuliangazia hili. Mfano mdogo, nimejikuta nafuta baadhi watu na vyombo vya habari huko Istagram haswa wa kitanzania, tatizo kubwa hukuti habari ya maana ni Diamond, sijui Kiba sijui nani kamtukana nani na ujinga ujinga mwingine wa picha za uchi-uchi wanajiita video vixens/models.

Ni wakati muafaka, Serikali ijaribu kudhibiti waandishi na vyombo vya habari haswa kwenye suala la habari za mtandaoni ipi ipewe kipaumbele. Naamini kuna jinsi ya kuzuia hizi content online zisiweze kupatikana kirahisi. Hapa hatuna sababu ya kusema eti kila mtu ana starehe yake, ili tuendelee kama Taifa vitu vya kipuuzi visipewe nafasi na hata kama unavihitaji lazima usote sana kuvipata.

Hapo bado hujasikiliza mahojiano wanayofanya hawa waandishi wetu wa kileo na the so called 'celebrities'...duh!

Wacha niishie hapa.
 
Poleni sana. Hilo jambo linaonyesha kuna ombwe kubwa, na huyo Uwoya ameamua kuweka mambo hadharani. Amemwaga mboga. Tusimlaumu.
Ila wakati mwingine bloggers na vijana wachanga katika Tasnia ya habari wanaona jinsi mnavyobadilisha magia, mara leo uko upande ule kesho uko kwa Musiba. Kwa ujumla nyinyi wakongwe mnashindwa kusimamia kile mnachokiamini, na pengine kigegeu kinawafanya wahisi kuna vitu vinafanyika nyuma ya pazia vinavyoviviza na kubadilisha mawazo yenu.
Hizo ni rasharasha tusubiri wakati wa masika (wakati wa uchaguzi mkuu?) tutaona maajabu yatayostaajabisha vyumba vya habari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…