Waandishi mmefikia hatua ya kudhalilishwa kiasi hiki?

Leo nimesikitishwa sana kwa na kitendo cha aibu cha msanii Irene Uwoya kugawa rushwa ya fedha kwa wanabahari mbele ya kamera.

Uwoya amefanya hivyo mbele ya camera kitendo kinachodhalilisha sana taaluma ya habari.

Lakini pia, sijathibitisha, naambiwa aibu nyingine ya mwaka ni kuwa wapo wanahabari waliopigana vikumbo kugombania fedha hizo alizokuwa akizigawa kwa mtindo wa pedeshee wa kike.

Kama hili la pili ni kweli basi, historia leo imeandikwa, hatuna waandishi nchi hii bali tuna wasanii katika tasnia ya habari.

Hapa ndio unajiuliza watetea taaluma ya habari kama hata ile Idara ya MAELEZO, Jukwaa na wahariri na MCT wako wapi?

Hawa waandishi wakemewe na au hatua zichukuliwe dhidi yao.

Mwalimu wangu Dr Kibatala (sio huyu wakili) aliwahi kutoa neno likanukuliwa visivyo. Alipowaambia waandishi wa habari ukweli huo wakamtolea clip kuthibitisha kuwa ni kweli kasema yaliyoandikwa. Dr Kibatala akawaambia hivi: nilichokisema nyie hamna uwezo wa kukitafsiri inavyotakiwa maana wengi wenu mmekimbilia uandishi wa habari baada ya kushindwa mitihani ya sekondari. Anaebisha naomba aniruhusu nitoe matokeo yake hadharani.
Challenge hiyo aliwapa waandishi miaka ya mwanzo ya 90, hadi leo hii hakuna mwandishi aliempa hicho kibali.
 
vijana makanjanja wanaofanya kazi kwenye hizi online media kama wanahabari rasmi ni janga katika sector ya habari.

naishauri serikali adhibiti online media.
nalisema hili kwasababu ukichunguza zile microphone zilizokuwepo kweye lile tukio ni za online media.
 
KABISA KABISA !!!!
LAKINI PALE NAONA KUNA MA BLOGER TU, TUSI WA JUDGE SANA WAANDISHI WA HABARI WENYEWE!!!
Hata wangekuwa wa_boo_nge wangegombania hivyo hivyo,hakuna asiyetaka hela aysee
 
Leo nimesikitishwa sana kwa na kitendo cha aibu cha msanii Irene Uwoya kugawa rushwa ya fedha kwa wanabahari mbele ya kamera.

Uwoya amefanya hivyo mbele ya camera kitendo kinachodhalilisha sana taaluma ya habari.

Lakini pia, sijathibitisha, naambiwa aibu nyingine ya mwaka ni kuwa wapo wanahabari waliopigana vikumbo kugombania fedha hizo alizokuwa akizigawa kwa mtindo wa pedeshee wa kike.

Kama hili la pili ni kweli basi, historia leo imeandikwa, hatuna waandishi nchi hii bali tuna wasanii katika tasnia ya habari.

Hapa ndio unajiuliza watetea taaluma ya habari kama hata ile Idara ya MAELEZO, Jukwaa na wahariri na MCT wako wapi?

Hawa waandishi wakemewe na au hatua zichukuliwe dhidi yao.
Wanaojiita waandishi wote form four waliangukia pua, ni division four
 
Kumbe ndio maana tasnia hii inadharaulika kila mahali, sio hapa DSM, Arusha au Mwanza.

Mnafikia mahali mnatupiwa noti kama mbwa anavyotupiwa makombo na mnagombania kiasi cha kuvunjiana kamera zenu na tape recorders?

Yaani hawa wasanii uchwara ndio wa kuvunja heshima zenu kiwango hicho?

Ndio maana mnaweza kununulika kiasi cha kuandika au kutoandika atakacho mtoa pesa.

Ukienda kama kule Mwanza unakuta waandishi wamebakia kupigana majungu kiasi hata wenyewe hawaelewani kisa kugombea mshiko.

Jibadilisheni muheshimiwe!

View attachment 1154274
Mkuu Mkongwe Mzoefu, kwanza asante kutuletea clip hii, hivyo mimi kama mwandishi wa habari, mkwongwe na mzoefu nina haya ya kusema.
  1. Kwanza ni kweli na kiukweli kabisa, waandishi hao habari, wamedhalilishwa kutupiwa fedha kama mbwa, Irene Uwoya amewadhailisha waandishi kuwatunza kwa kuwatupia fedha kama mbwa wanavyotupiwa nyama. Japo Irene Uwoya alifanya kitendo kile cha tunza kwa nia njema, tunza za waandishi zinafanywa kwa heshima maalum ikiwemo kuwawekea hizo tunza kwenye bahasha za khaki na waandishi kukabidhiwa kwa majina na waandishi kusaini. Irene Uwoya ni kiazi, she is imbecile, huwezi kuwatunza kuwatunza watu mtindo wa kuwatunza wasanii on the stage au zile tunza za kitchen party, alifanya vile kutafuta kiki. NB. Nasisitiza Bahasha za waandishi sio rushwa.https://www.jamiiforums.com/threads/waandishi-wa-habari-na-bahasha-sio-kila-bahasha-ni-rushwa-pasco-wa-jf.215720/#js-post-3196765
  2. Waandishi waiokuwepo kwenye tukio hilo pia wamejidhalilisha na kutudhalilisha sisi waandishi wengine wote kuonekana waandishi ndio tuko hivyo kitu ambacho sii kweli. Waandishi wa ukweli tuliopitia mafunzo hatuko hivyo. Kwenye kundi lile naamini kulikuwa na waandishi wa ukweli ambao wao hawakugombea lakini kwa vile lilikuwa zogo, wote wakaonekana waligombea, kwa mtindo wa samaki mmoja akioza, samaki wote wameoza. Haiwezekani mpiga picha mwenye camera ya million 20, agombee elfu 10,000 na kurisk kuharibu kifaa chake cha million 20!.
  3. Kwa jicho la haraka, wengi wa waandishi waiokuwepo pale ni waandishi wa michezo na burudani wakiwemo wale wa online media na ma bloggers. Hawa ni waandishi in a sense ya kuhabarisha jamii kupitia online platforms mbalimbali kama online TVs, blogs, forums, fb, insta, twitter etc. Hawa wanakuwa licenced na TCRA.
  4. Tukio hili ni blessing in disguise kuonyesha jinsi sheria mpya ya habari inavyotuetea majanga. Kwa mujibu wa sheria, waandishi wa habari wanasajiliwa na Idara ya Habari Maelezo na kupewa Press Cards baada ya kukidhi sifa na vigezo ikiwemo kuwasilisha vyeti vya kitaaluma. Idara hii ya Habari Maelezo iko chini ya Wizara ya Habari, hivyo wanaopata Press Cards za Idara ya Habari Maelezo ni waandishi kweli wenye sifa vigezo na weledi, hawawezi kugombea pesa kama mbwa.
  5. Wakati Maelezo chini ya Wizara ya Habari wanasajili waandishi wa habari wa ukweli wenye taaluma sifa na vigezo, Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA, chini ya Wizara ya mawasliano, wao wanasajili ma bloggers na online TV, sifa ya kusajiliwa ni kulipia ada ya usajili ya TZS 1,000,000. Baada ya kulipia ada hiyo, majina yao yanapelekwa Maelezo kuwa issued na Press Cards za Maelezo, hivyo tukikutana kwenye news events wote tunaonekana sawa ni waandishi wa habari wenye Press Cards, mmoja kasomea uandishi kama taaluma, mwengine katokea mtaani hana a wala b kuhusu fani ya habari, matokeo ndio haya sasa ya waandishi kutupiwa fedha kama mbwa na wao kugombea kisha wote kuonekana the same!.
  6. A way Forward. 1. Idara ya Habari isikubali kuletewa makorokocho ya TCRA na kuwapa Press Cards kama za waandishi. Maelezo watenganishe Press Cards kati ya waandishi wa habari wa ukweli waliosomea na hawa ma bloggers na online media ili ikitokea tukio la udhalilishaji wa mwandishi tujue ni mwandishi mweledi wa newsroom au wale wa mitaani wa TCRA. Kinachofanywa na Maelezo kwa sasa ni sawa na madakitari medical doctors kupewa same licenses sawa na waganga wa kienyeji, maana wote wanatibu, mmoja kasomea, mwengine anatumia maruhani and they are the same.
  7. Way Forward 2: Baraza la Idhibati kwa Waandishi wa Habari lianzishwe ili kutuondolea aibu hii na udhalilishwaji huu. Waandishi wajulikane ni waandishi kweli kama ilivyo kwa wanasheria, madakitari na ma engineer, kuwa wakili mtu lazima ahitimu LL.B, chini ya hapo ni paralegal, ili uwe daktari, lazima uhitimu MD, etc, sasa tufike mahali ili kuwa a licensed na accredited journalist lazima uwe na kiwango fulani cha elimu. Wale wasio kidhi vigezo nao watakuwa na utambulisho wao kama ni technical people ma cameraman, ma bloggers, waandishi wa mtaani wa online TV etc.
  8. A Way Forward 3: Turekebishe sheria kuunganisha habari na mawasiloano ambapo mambo yote media yawe chini ya sheria moja. Kwa sasa vyombo vya habari vya print media vinaratibiwa na kudhibitiwa na sheria ya habari chini Wizara ya Habari, na vyombo vyote vya utangazaji vinaratibiwa na sheria ya Utangazaji iko chini ya TCRA, iliyoko chini ya Wizara ya Mawasiliano
Paskali
 
Wanatunzwa bwana kwani nani kasema wanadhalilishwa!!!
Wew usiye na dhambi uwe wa kwanza kutupa jiwe kwao....watu wameaga kwao wanaenda kutafuta pesaaa, sikija kirahis kwanin usichangamkie fursa.
Au inakuuma hukuepo?!
Stupid reply of the highest order
 
Ndio maana siku zote nawazarau sana hawa wanahabari pamoja na walimu, wanapenda sana kujidhalilisha.....
 
Kumbe ndio maana tasnia hii inadharaulika kila mahali, sio hapa DSM, Arusha au Mwanza.

Mnafikia mahali mnatupiwa noti kama mbwa anavyotupiwa makombo na mnagombania kiasi cha kuvunjiana kamera zenu na tape recorders?

Yaani hawa wasanii uchwara ndio wa kuvunja heshima zenu kiwango hicho?

Ndio maana mnaweza kununulika kiasi cha kuandika au kutoandika atakacho mtoa pesa.

Ukienda kama kule Mwanza unakuta waandishi wamebakia kupigana majungu kiasi hata wenyewe hawaelewani kisa kugombea mshiko.

Jibadilisheni muheshimiwe!

View attachment 1154274

Kwani Irene Uwoya ameidhalisha tasnia au ameonesha tafsiri halisi ya tasinia? Ukiangalia video utaona kuna mwanatasnia mmoja anajielewa aliokota fedha na mrejeshea apiginga zoezi zima.
 
Hahahaha akaharibu kikao hapo mwishoni...
Kumbe ndio maana tasnia hii inadharaulika kila mahali, sio hapa DSM, Arusha au Mwanza.

Mnafikia mahali mnatupiwa noti kama mbwa anavyotupiwa makombo na mnagombania kiasi cha kuvunjiana kamera zenu na tape recorders?

Yaani hawa wasanii uchwara ndio wa kuvunja heshima zenu kiwango hicho?

Ndio maana mnaweza kununulika kiasi cha kuandika au kutoandika atakacho mtoa pesa.

Ukienda kama kule Mwanza unakuta waandishi wamebakia kupigana majungu kiasi hata wenyewe hawaelewani kisa kugombea mshiko.

Jibadilisheni muheshimiwe!

View attachment 1154274
 
Back
Top Bottom