Mechi za mwisho VPL,Vita ya ubingwa na kushuka daraja

Nifah

JF-Expert Member
Feb 12, 2014
31,571
65,418
Baada ya kuunguruma kwa takribani miezi tisa (August -May),hatimaye leo tunaelekea kwenye mwisho wa msimu wa Ligi kuu ya soka Tanzania Bara (VPL)

Leo hii viwanja 8 vitawaka moto,lakini macho na masikio ya wengi vitaelekezwa Mwanza ambapo timu iliyojihakikishia ubingwa Dar Young Africans itaumana na Mbao FC inayopambana kukwepa panga la kushuka daraja.
Ikumbukwe ya kwamba timu hizi mbili zinakutana mara 2 sasa ndani ya mwezi mmoja.
Mechi iliyopita Mbao walifanikiwa kuwafunga Yanga bao 1-0 katika mchezo wa kombe la shirikisho nusu fainali. Ushindi huo uliwapa Mbao tiketi ya kushiriki fainali,huku Yanga wakielekeza machungu yao kwenye ligi kuu ya Tanzania bara ambako walishinda mechi zao zote.

Hivyo mechi ya leo ni ya kulipa kisasi kwa Yanga dhidi ya Mbao huku Mbao wakipambana kufa na kupona kubaki ligi kuu.

Uwanja wa Taifa Wekundu wa Msimbazi watawakaribisha Mwadui FC.
Mechi hii wengi wanasubiria miujiza endapo Simba wataweza kuwafunga Mwadui mabao 15 ili kuchukua Kombe la ligi kuu ambalo Watani wao Yanga wana uhakika wa kulichukua kwa mara ya tatu mfululizo.

Viwanja vingine ni
Azam Complex Mbagala ambapo Azam wataumana na Kagera Sugar

Majimaji Ruvuma
Majimaji FC vs Mbeya City

Uwanja wa Sokoine Mbeya
Tanzania Prisons vs African Lyon

Uwanja wa Kambarage Shinyanga
Stand United vs Ruvu Shooting

Mechi zote ni Saa 10:00 Jioni,tukutane hapa kwa updates.

=====================================
Updates
Mpira unaanza Kirumba Mwanza
Yanga 0-Mbao
 
Baada ya kuunguruma kwa takribani miezi tisa (August -May),hatimaye leo tunaelekea kwenye mwisho wa msimu wa Ligi kuu ya soka Tanzania Bara (VPL)

Leo hii viwanja 6 vitawaka moto,lakini macho na masikio ya wengi vitaelekezwa Mwanza ambapo timu iliyojihakikishia ubingwa Dar Young Africans itaumana na Mbao FC inayopambana kukwepa panga la kushuka daraja.
Ikumbukwe ya kwamba timu hizi mbili zinakutana mara 2 sasa katika ndani ya mwezi mmoja.
Mechi iliyopita Mbao walifanikiwa kuwafunga Yanga bao 1-0 katika mchezo wa kombe la shirikisho nusu fainali. Ushindi huo uliwapa Mbao tiketi ya kushiriki fainali,huku Yanga wakielekeza machungu yao kwenye ligi kuu ya Tanzania bara ambako walishinda mechi zao zote.

Hivyo mechi ya leo ni ya kulipa kisasi kwa Yanga dhidi ya Mbao huku Mbao wakipambana kufa na kupona kubaki ligi kuu.

Uwanja wa Taifa Wekundu wa Msimbazi watawakaribisha Mwadui FC.
Mechi hii wengi wanasubiria miujiza endapo Simba wataweza kuwafunga Mwadui mabao 15 ili kuchukua Kombe la ligi kuu ambalo Watani wao Yanga wana uhakika wa kulichukua kwa mara ya tatu mfululizo.

Viwanja vingine ni
Azam Complex Mbagala ambapo Azam wataumana na Kagera Sugar

Majimaji Ruvuma
Majimaji FC vs Mbeya City

Uwanja wa Sokoine Mbeya
Tanzania Prisons vs African Lyon

Uwanja wa Kambarage Shinyanga
Stand United vs Ruvu Shooting

Mechi zote ni Saa 10:00 Jioni,tukutane hapa kwa updates.
one love,we will be together...
 
Simba wasubiri point zao za Uswizi wawe mabingwa.
Kuongoza kooote ligi leo wanasubiri point za KAMATI
Hahaha halafu leo nilikumbuka hili,Simba walianza ligi kuu kwa mbwembwe sana.
Kumbuka wakati tunaanza mzunguko wa pili ilifikia tofauti ya points 8 tofauti kati yetu na wao...

Yanga naifananisha na mimi binafsi,naweza kukuacha ujione mshindi ila nina mipango yangu ambayo utakuja kushtuka tu nimekupiga gape ambalo hutoweza kuliziba asilani,daima naamini ktk ushindi wa mwishoni...usio na kelele.
Naipenda Yanga.
 
Hahaha halafu leo nilikumbuka hili,Simba walianza ligi kuu kwa mbwembwe sana.
Kumbuka wakati tunaanza mzunguko wa pili ilifikia tofauti ya points 8 tofauti kati yetu na wao...

Yanga naifananisha na mimi binafsi,naweza kukuacha ujione mshindi ila nina mipango yangu ambayo utakuja kushtuka tu nimekupiga gape ambalo hutoweza kuliziba asilani,daima naamini ktk ushindi wa mwishoni...usio na kelele.
Naipenda Yanga.
Wahuni wa kariakoo wanavyochambuliwa na shabiki wa simba.
Hao akina Aveva wanawadanganya mashabiki kuwa watazipata Uswizi points,yaani wamezikosa Kaitaba,wamezikosa KAMATI YA SAA 72 NDO WAZIPATE ULAYA
 

Attachments

  • VID-20170517-WA0014.mp4
    2.2 MB · Views: 28
Hahaha halafu leo nilikumbuka hili,Simba walianza ligi kuu kwa mbwembwe sana.
Kumbuka wakati tunaanza mzunguko wa pili ilifikia tofauti ya points 8 tofauti kati yetu na wao...

Yanga naifananisha na mimi binafsi,naweza kukuacha ujione mshindi ila nina mipango yangu ambayo utakuja kushtuka tu nimekupiga gape ambalo hutoweza kuliziba asilani,daima naamini ktk ushindi wa mwishoni...usio na kelele.
Naipenda Yanga.
umeona eeh yanga ni kama man u ya alex ferguson
 
TFF iwe makini na mechi za leo hasa kwa wale wanaopambana kubakia Ligi Kuu.

Mechi ya Toto na Mtibwa itazamwe kwa jicho la umakini sana.

Uzuri Azam Tv atarusha mubashara mechi sita kati ya 8 zitakazochezwa leo.

Cha kushangaza mechi ya Mtibwa na Toto hawaionyeshi.
 
Mipira ya Bongo ovyooo kaz ipo pale kwa QUEEN ELIZABETH
Je Arsenal ataingia top 4 au je Liverpool ataendelea kushikilia nafasi ya 4?
 
  • Thanks
Reactions: SDG
TFF iwe makini na mechi za leo hasa kwa wale wanaopambana kubakia Ligi Kuu.

Mechi ya Toto na Mtibwa itazamwe kwa jicho la umakini sana.

Uzuri Azam Tv atarusha mubashara mechi sita kati ya 8 zitakazochezwa leo.

Cha kushangaza mechi ya Mtibwa na Toto hawaionyeshi.
Mubaashara ni game 5 (xtra, 1,2, hd na zbc2) na game 3 wataleta kwa mkatiko
 
TFF iwe makini na mechi za leo hasa kwa wale wanaopambana kubakia Ligi Kuu.

Mechi ya Toto na Mtibwa itazamwe kwa jicho la umakini sana.

Uzuri Azam Tv atarusha mubashara mechi sita kati ya 8 zitakazochezwa leo.

Cha kushangaza mechi ya Mtibwa na Toto hawaionyeshi.

Tanzania Prison wamevuta sarafu mapema sanaaaaa kwa habari ambazo nimezipata kwa swahiba wangu wa African Lyon ivyo wanaingia pale Sokoine Stadium na matokeo mfukoni labda kama jana kuwe na mabadiliko.
 
Timu zote zipo viwanjani Yanga wakiwa CCM Kirumba kumenyana na Mbao FC...Simba wapo jiji Dar wakiwakaribisha Mwadui FC.

Bodi ya Ligi imechonga makombe mawili ya ligi moja lipo Dar Taifa lingine liko Kirumba Mwanza..

Sababu ya kufanya hivyo ni mkaribiano wa point kati ya Simba na Yanga....Yanga ana point 68, Simba anapoint 65... hivyo Yanga akifungwa simba itabidi ishinde kwa magoli zaidi ya 12 kwa sifuri ili awe bingwa.

f6d0a08dd24eec18e7f38c56f6b8cbef.jpg


Mbao FC 1 vs 0 Yanga

Simba 2 vs 1 Mwadui FC

Majimaji 2 vs 1 MBC

Mtibwa 3 vs 1 Toto

Ndanda 2 vs 0 Jkt Ruvu.

Azam 0 vs 1 Kagera.

TZP 0 vs 0 AFL
*************************
Mechi zote zimemalizika.

Yanga Bingwa ........

Zilizoshuka daraja..

1, Afrika Lion
2,Toto Africa
3, JKT Ruvu
e9b284c47c56056b999153f3d562009d.jpg

19628bab9546599329b33d6ca6f49200.jpg
 
Back
Top Bottom