Mdude Nyagali kufungua kesi mahakamani kwa hati ya dharura kuhusu pesa za wahanga tetemeko Kagera

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Najiandaa kufungua kesi mahakama kuu kwa hati ya dharura kuishtaki serikali kwa kutapeli pesa za wahanga wa tetemeko Kagera.

Nimesikitika sana baada ya serikali iliyovunja rekodi ya kukusanya mapato/kodi mpaka kuvuka malengo kukosa fedha za kujenga miundombinu ya serikali iliyoharibiwa na tetemeko Kagera na badala yake serikali imetapeli pesa ambazo zilichangwa na mashirika na watu mbalimbali kwa ajili ya kusaidia wananchi wa Kagera walioathirika na tetemeko hilo.

Yaani ni sawa na waumini kuchanga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kanisa/msikiti halafu mchungaji au imam anachukua fedha hizo na kujengea nyumba yake binafsi wakati huo mchungaji au imam anapata posho ambazo angetumia kujengea nyumba yake, huo ni utapeli.

Nilitegemea serikali ingetumia pesa za serikali kujenga miundombinu kwa pesa za mfuko wa maafa ambazo hutengwa kila mwaka na serikali kwa ajili ya maafa.
Sikutegemea serikali kukosa fedha na badala yake kutapeli fedha zilizochangwa na mashirika na wananchi mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wenzao walioathirika na tetemeko hilo.

Na kama lengo la serikali ilikuwa ni hilo basi serikali ingekuwa wazi tangu mwanzo kwamba inaomba michango kwa ajili ya kurejesha miundombinu ya serikali na sio inaomba michango kwa ajili ya kuwasaidia wananchi walioathirika na tetemeko,huo ni ulaghai.

Utapeli huu wa serikali una utofauti gani na utapeli wa kuwaudhia watu dhahabu feki?mecury feki?.Nawaomba watanzania mniunge mkono nimedhamilia kwa hili ni lazima tufike mahakamani kwa kuwa mimi ni miongoni mwa watu waliochangia.

Mdude Nyagali
Sumu ya nyigu

TETEMEKO KAGERA.jpg
 
Bila kujenga hospitali na mashule hao wahanga watatibiwa na kusomea wapi! Ugonjwa wa ubinafsi uliozoeleka miongoni wa wanasiasa sasa umeamia kwa raia.
 
Mungu mkubwa tuzidi kumuombea jamani, maana kumbe majizi yanajulikana na jizi kuu ni............................
 
Bado naendelea kuitafakari Serikali yetu sijui tunakoelekea aiseeeeee
 
Bila kujenga hospitali na mashule hao wahanga watatibiwa na kusomea wapi! Ugonjwa wa ubinafsi uliozoeleka miongoni wa wanasiasa sasa umeamia kwa raia.
Acheni utoto na wewe kwani hyo pesa tulichanga ili ijenge hospitali na shule au tuliwachangia wananchi na kama kujenga hizo shule na hospitali hilo ni jukumu la Serikali watoe kwenye kitengo cha maafa.
 
Najiandaa kufungua kesi mahakama kuu kwa hati ya dharura kuishtaki serikali kwa kutapeli pesa za wahanga wa tetemeko Kagera.

Nimesikitika sana baada ya serikali iliyovunja rekodi ya kukusanya mapato/kodi mpaka kuvuka malengo kukosa fedha za kujenga miundombinu ya serikali iliyoharibiwa na tetemeko Kagera na badala yake serikali imetapeli pesa ambazo zilichangwa na mashirika na watu mbalimbali kwa ajili ya kusaidia wananchi wa Kagera walioathirika na tetemeko hilo.

Yaani ni sawa na waumini kuchanga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kanisa/msikiti halafu mchungaji au imam anachukua fedha hizo na kujengea nyumba yake binafsi wakati huo mchungaji au imam anapata posho ambazo angetumia kujengea nyumba yake, huo ni utapeli.

Nilitegemea serikali ingetumia pesa za serikali kujenga miundombinu kwa pesa za mfuko wa maafa ambazo hutengwa kila mwaka na serikali kwa ajili ya maafa.
Sikutegemea serikali kukosa fedha na badala yake kutapeli fedha zilizochangwa na mashirika na wananchi mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wenzao walioathirika na tetemeko hilo.

Na kama lengo la serikali ilikuwa ni hilo basi serikali ingekuwa wazi tangu mwanzo kwamba inaomba michango kwa ajili ya kurejesha miundombinu ya serikali na sio inaomba michango kwa ajili ya kuwasaidia wananchi walioathirika na tetemeko,huo ni ulaghai.

Utapeli huu wa serikali una utofauti gani na utapeli wa kuwaudhia watu dhahabu feki?mecury feki?.Nawaomba watanzania mniunge mkono nimedhamilia kwa hili ni lazima tufike mahakamani kwa kuwa mimi ni miongoni mwa watu waliochangia.

Mdude Nyagali
Sumu ya nyigu

View attachment 433977
masikini afu jana kuna mmoja alisema atajiua kwa ajili hili hili. sijui alitimiza azma yake? I hope not.
 
kwan sirikali imesema nia kiac gan kilichangwa na wadau wote wa nje na wa ndani? mwenye kujua official figure iliotolewa na sirikali naomba anijuze
 
Bilicanas pale kwenye mjengo wetu mwambie M/kiti wako alipe deni au asepe zake tutatimba fasta na wahanga.
Wananchi wa Kagera wanalalamika zile pesa zao za rambi rambi ambazo walipewa mmezila laana hiyo hatowaacha salama.
 
Bila kujenga hospitali na mashule hao wahanga watatibiwa na kusomea wapi! Ugonjwa wa ubinafsi uliozoeleka miongoni wa wanasiasa sasa umeamia kwa raia.
Serikali ni nijukumu lake kujenga izo hospital na shule kupitia kamati ya maafa ambazo hela zake hutengwa kila mwaka wa fetha unapochangia mada lazma uje kile unacho kisema sio kuropoka tu.pesa zilizochangwa sio za serikali ni zawananchi wa kawaida na mashirika kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wenzao na sio serikali ambayo inavyanzo vingi vya mapato
 
Back
Top Bottom