๐— ๐—ฎ๐—ฎ๐—ณ๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐—บ๐˜ƒ๐˜‚๐—ฎ ๐——๐—ฎ๐—ฟ ๐—ป๐—ฎ ๐˜‚๐—ธ๐—ถ๐—บ๐˜†๐—ฎ ๐˜„๐—ฎ ๐˜€๐—ฒ๐—ฟ๐—ถ๐—ธ๐—ฎ๐—น๐—ถ ๐—ป๐—ถ ๐—บ๐—ฎ๐˜๐—ผ๐—ธ๐—ฒ๐—ผ ๐˜†๐—ฎ ๐—ž๐—ฎ๐˜๐—ถ๐—ฏ๐—ฎ ๐—บ๐—ฏ๐—ผ๐˜ƒ๐˜‚..

Mdude_Nyagali

Member
Dec 11, 2022
60
1,237
Baada ya mwenyekiti wa Chadema taifa kutangaza maandamano ya amani January 24, 2023 ilichukua dakika 40 tu kwa mkuu wa mkoa Dar kujibu maandamano hayo ya CHADEMA. Tena alilazimika kutumia madhabahu ya kanisa takatifu kujibu maandamano hayo kwa udharura.

Wakati tukiwa tunatafakari ushapu wa serikali kujibu/kuchukua hatua dhidi ya wapinzani wa serikali tunapigwa na butwaa kuona serikali hiyohiyo imeshindwa kuchukua hatua zozote za kukabiliana na maafa ambayo yametokana na mvua nyingi kunyesha jiji la Dar kwa siku ya pili leo. Pamoja na kwamba mvua hiyo imeharibu miundombinu ya serikali ikiwemo madaraja lakini bado serikali haijachukua hatua yoyote zaidi ya kukaa kimya.

Nilitegemea mkuu wa mkoa wa Dar angekuwa wa kwanza kutoa kauli ya serikali na hatua ambazo serikali ingechukua kukabiliana na maafa yanayotakana na mvua hiyo. Kwa bahati mbaya imekuwa tofauti RC huyo yupo yupo tu anazunguka na tumbo lake akisubiri mshahara na posho akamalizie ujenzi wa ghorofa yake. Ndio maana nasisitiza kuwa hizi nafasi ya ukuu wa wilaya na mkoa ni mzigo na hasara kwa serikali na ni zao la kuwa na katiba mbovu.

Nilitegemea nimuone waziri mkuu ambaye kitengo cha maafa kiko chini yake. Nilitegemea kuona Chopa ikiruka angani kusaidia wahanga waliokwama maeneo yenye mafuriko, lakini kwa bahati mbaya waziri mkuu yuko busy kupambana na makundi ya Urais . PM Katelefone anaamini Urais ataupata huko anakonyukana na wenzake na wala sio kwa wananchi, hii ni zao la katiba mbovu pia.

Nilitegemea ningewaona wabunge wa mkoa wa Dar wakiwa site na kufuatilia uwajibikaji wa serikali, lakini kwa bahati mbaya wabunge wako Dodoma na miongoni mwao wengine muda huu wako wanakula bia pale Dodoma hotel na hawapokei simu za wananchi wao waliokumbwa na maafa. Wanafanya hivi wakiamini kwamba ubunge wao unatoka kwa Rais na sio kwa wapiga kura ambao ni wananchi. Haya pia ni matokeo ya katiba mbovu.

Nilitegemea kumuona Rais akitembelea maeneo ambayo yameathirika kuwafariji na kuwatia moyo wahanga huku akiagiza vyombo vilivyo chini yake kuharakisha kurudisha miundombinu iliyoharibiwa kwa udharura. Kwa bahati mbaya Rais yuko busy kwa Askofu Malasusa akitafuta sifa ambazo hastahili. Rais anaamini hata wananchi wasipompigia kura yeye bado atarudi ikulu kwa nguvu za vyombo vya dola. Hili pia linatokana na katiba mbovu.

Hivyo basi kutokana na mapungu hayo maandamano ya tarehe 24 January 2024 ni muhimu mno kwani hiyo ndio njia pekee ambayo inaweza kuleta matokeo ya viongozi wa serikali kuheshimu wananchi. Nategemea wahanga wote wa mafuriko tutaonana barabarani siku hiyo tukiimba nyimbo za ukombozi kuelekea ofisi za Umoja wa Mataifa.

Lazima tutumie kila njia kuweka misingi bora ya nchi yetu kwa faida ya vizazi vijavyo.

Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Screenshot_20240121-171010_1.jpg
 
Leo nimelala sana mpaka saa nane mchana, tatizo ni hii katiba, tunahitaji katiba mpya.

Pia wife kazidisha chumvi kwemye mboga, bila katiba mpya atatuua kwa kisukari na presha
duu ss itakuwajee km mboga imezidi chumvi mkuu ndio kushinda na njaa au unapiga hvyo hvyo kibishii...
 
Katiba hii mbovu inawafanya viongozi kuwa juu ya wananchi (mabosi wa wananchi) badala ya kuwa watumishi wa wananchi.

Endapo tungekuwa na katiba nzuri viongozi wangewajibishwa kwa uzembe huu.
 
  • Thanks
Reactions: xox
Baada ya mwenyekiti wa Chadema taifa kutangaza maandamano ya amani January 24, 2023 ilichukua dakika 40 tu kwa mkuu wa mkoa Dar kujibu maandamano hayo ya CHADEMA. Tena alilazimika kutumia madhabahu ya kanisa takatifu kujibu maandamano hayo kwa udharura.

Wakati tukiwa tunatafakari ushapu wa serikali kujibu/kuchukua hatua dhidi ya wapinzani wa serikali tunapigwa na butwaa kuona serikali hiyohiyo imeshindwa kuchukua hatua zozote za kukabiliana na maafa ambayo yametokana na mvua nyingi kunyesha jiji la Dar kwa siku ya pili leo. Pamoja na kwamba mvua hiyo imeharibu miundombinu ya serikali ikiwemo madaraja lakini bado serikali haijachukua hatua yoyote zaidi ya kukaa kimya.

Nilitegemea mkuu wa mkoa wa Dar angekuwa wa kwanza kutoa kauli ya serikali na hatua ambazo serikali ingechukua kukabiliana na maafa yanayotakana na mvua hiyo. Kwa bahati mbaya imekuwa tofauti RC huyo yupo yupo tu anazunguka na tumbo lake akisubiri mshahara na posho akamalizie ujenzi wa ghorofa yake. Ndio maana nasisitiza kuwa hizi nafasi ya ukuu wa wilaya na mkoa ni mzigo na hasara kwa serikali na ni zao la kuwa na katiba mbovu.

Nilitegemea nimuone waziri mkuu ambaye kitengo cha maafa kiko chini yake. Nilitegemea kuona Chopa ikiruka angani kusaidia wahanga waliokwama maeneo yenye mafuriko, lakini kwa bahati mbaya waziri mkuu yuko busy kupambana na makundi ya Urais . PM Katelefone anaamini Urais ataupata huko anakonyukana na wenzake na wala sio kwa wananchi, hii ni zao la katiba mbovu pia.

Nilitegemea ningewaona wabunge wa mkoa wa Dar wakiwa site na kufuatilia uwajibikaji wa serikali, lakini kwa bahati mbaya wabunge wako Dodoma na miongoni mwao wengine muda huu wako wanakula bia pale Dodoma hotel na hawapokei simu za wananchi wao waliokumbwa na maafa. Wanafanya hivi wakiamini kwamba ubunge wao unatoka kwa Rais na sio kwa wapiga kura ambao ni wananchi. Haya pia ni matokeo ya katiba mbovu.

Nilitegemea kumuona Rais akitembelea maeneo ambayo yameathirika kuwafariji na kuwatia moyo wahanga huku akiagiza vyombo vilivyo chini yake kuharakisha kurudisha miundombinu iliyoharibiwa kwa udharura. Kwa bahati mbaya Rais yuko busy kwa Askofu Malasusa akitafuta sifa ambazo hastahili. Rais anaamini hata wananchi wasipompigia kura yeye bado atarudi ikulu kwa nguvu za vyombo vya dola. Hili pia linatokana na katiba mbovu.

Hivyo basi kutokana na mapungu hayo maandamano ya tarehe 24 January 2024 ni muhimu mno kwani hiyo ndio njia pekee ambayo inaweza kuleta matokeo ya viongozi wa serikali kuheshimu wananchi. Nategemea wahanga wote wa mafuriko tutaonana barabarani siku hiyo tukiimba nyimbo za ukombozi kuelekea ofisi za Umoja wa Mataifa.

Lazima tutumie kila njia kuweka misingi bora ya nchi yetu kwa faida ya vizazi vijavyo.

Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.View attachment 2878690
RC alishasema Maji yatamsaidia kuhamisha watu mabondeni na kwenye njia za maji
 
MH. RAIS SAMIA HASSAN : WANANCHI HUKO TEGETA MUHAME


View: https://m.youtube.com/watch?v=9pLYYuIefJI

Mheshimiwa rais ametoa tamko hilo leo jumapili 21 January 2024 kwa wakaazi wa jiji la Dar es Salaam .... kwa muda sasa TMA Mamlaka ya Hali ya Hewa ilitoa tahadhari na sasa madhara yake tunayaona

Nimewaelekeza mawaziri husika kukaa kwa utayari kwenda kuangalia hali ilivyo ili kukabiliana na madhara haya


Wananchi waondoke kwenye kingo za vijito na mito ili kuepusha taifa kukubwa na maafa ....

MAONI YA RAIA : MAJIJI MENGINE WAMEWEZA KUKABILIANA NA KINGO ZA MITO KUMOMONYOKA

Picha hapa chini kingo za mto mkubwa wa usiokauka mto Siene katika jiji la Paris unaopitisha meli za cruise
1705849244099.png


Picha hapa chini za kingo za mto mdogo tena wa msimu wa mto Gide kitongoji cha Ubungo jijini Dar es Salaam

1705849300546.png

Wanafunzi wa kitivo cha uhandisi chuo kikuu tajwa kongwe UDSM kwa kushirikiana na halmashauri ya Ubungo TAMISEMI wangeweza kutumia kodi za wananchi vizuri na wanafunzi wa UDSM kujifunza kwa vitendo kujenga kingo hatimaye majina yao kuingia ktk rekodi kumbukizi tukuka kuwa elimu imewezesha kutatua changamoto katika jamii .


Kifusi cha mchanga uliosombwa toka kingo za mto Msimbazi kikiwa kimechotwa na kuwekwa kando eneo la Jangwani DSM
1705849452902.png

Jangwani Dar es Salaam

Picha chini ufukwe wa Ocean Road barabara ya Barrack Obama jijini Dar es Salaam wenye mawimbi makubwa toka bahari ya Hindi yanayotishia kusababisha kumomonyoka kwa ardhi na barabara pembezoni mwa bahari ukiimarishwa na kunakishiwa vibaraza vya kutembelea
1705850626638.png

Ocean Road Barack Obama Road DSM
 
Dharura kama hizi wangetumia majeshi yetu pale panapohitajika, lakini badala yake wanayanoa kwa ajili ya tarehe 24/1
 
Baada ya mwenyekiti wa Chadema taifa kutangaza maandamano ya amani January 24, 2023 ilichukua dakika 40 tu kwa mkuu wa mkoa Dar kujibu maandamano hayo ya CHADEMA. Tena alilazimika kutumia madhabahu ya kanisa takatifu kujibu maandamano hayo kwa udharura.

Wakati tukiwa tunatafakari ushapu wa serikali kujibu/kuchukua hatua dhidi ya wapinzani wa serikali tunapigwa na butwaa kuona serikali hiyohiyo imeshindwa kuchukua hatua zozote za kukabiliana na maafa ambayo yametokana na mvua nyingi kunyesha jiji la Dar kwa siku ya pili leo. Pamoja na kwamba mvua hiyo imeharibu miundombinu ya serikali ikiwemo madaraja lakini bado serikali haijachukua hatua yoyote zaidi ya kukaa kimya.

Nilitegemea mkuu wa mkoa wa Dar angekuwa wa kwanza kutoa kauli ya serikali na hatua ambazo serikali ingechukua kukabiliana na maafa yanayotakana na mvua hiyo. Kwa bahati mbaya imekuwa tofauti RC huyo yupo yupo tu anazunguka na tumbo lake akisubiri mshahara na posho akamalizie ujenzi wa ghorofa yake. Ndio maana nasisitiza kuwa hizi nafasi ya ukuu wa wilaya na mkoa ni mzigo na hasara kwa serikali na ni zao la kuwa na katiba mbovu.

Nilitegemea nimuone waziri mkuu ambaye kitengo cha maafa kiko chini yake. Nilitegemea kuona Chopa ikiruka angani kusaidia wahanga waliokwama maeneo yenye mafuriko, lakini kwa bahati mbaya waziri mkuu yuko busy kupambana na makundi ya Urais . PM Katelefone anaamini Urais ataupata huko anakonyukana na wenzake na wala sio kwa wananchi, hii ni zao la katiba mbovu pia.

Nilitegemea ningewaona wabunge wa mkoa wa Dar wakiwa site na kufuatilia uwajibikaji wa serikali, lakini kwa bahati mbaya wabunge wako Dodoma na miongoni mwao wengine muda huu wako wanakula bia pale Dodoma hotel na hawapokei simu za wananchi wao waliokumbwa na maafa. Wanafanya hivi wakiamini kwamba ubunge wao unatoka kwa Rais na sio kwa wapiga kura ambao ni wananchi. Haya pia ni matokeo ya katiba mbovu.

Nilitegemea kumuona Rais akitembelea maeneo ambayo yameathirika kuwafariji na kuwatia moyo wahanga huku akiagiza vyombo vilivyo chini yake kuharakisha kurudisha miundombinu iliyoharibiwa kwa udharura. Kwa bahati mbaya Rais yuko busy kwa Askofu Malasusa akitafuta sifa ambazo hastahili. Rais anaamini hata wananchi wasipompigia kura yeye bado atarudi ikulu kwa nguvu za vyombo vya dola. Hili pia linatokana na katiba mbovu.

Hivyo basi kutokana na mapungu hayo maandamano ya tarehe 24 January 2024 ni muhimu mno kwani hiyo ndio njia pekee ambayo inaweza kuleta matokeo ya viongozi wa serikali kuheshimu wananchi. Nategemea wahanga wote wa mafuriko tutaonana barabarani siku hiyo tukiimba nyimbo za ukombozi kuelekea ofisi za Umoja wa Mataifa.

Lazima tutumie kila njia kuweka misingi bora ya nchi yetu kwa faida ya vizazi vijavyo.

Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.View attachment 2878690
Dar hakuna mafuriko ila kuna watu wameyafuata maji kwenye njia zake. Mlishaambiwa na mkuu wa mkoa kwamba muamue kukaa na maji au myapishe. Halafu watu wa dar wanajionaga wajanja lakini cha ajabu hawajui wapi pa kujenga na wapi ni njia ya maji ๐Ÿ˜ค๐Ÿ˜ค๐Ÿ˜ค๐Ÿ˜ค
 
Leo nimelala sana mpaka saa nane mchana, tatizo ni hii katiba, tunahitaji katiba mpya.

Pia wife kazidisha chumvi kwemye mboga, bila katiba mpya atatuua kwa kisukari na presha
Do you even know the essential elements for sustainable and inclusive development? Do you know it cannot be achieved without a good constitution? Do you know, actually you are right with your comments although you though that you are mocking us? Kulala sana ni kwa sababu pengine wewe ni fisadi ambaye haoni umuhimu wa kufanya kazi kwa sababu anakula vya bure.
 
Shida sio katiba, je hiyo mpya itajiendesha yenyewe. Africa kusini ni Moja ya nchi zenye katiba Bora Duniani. Lakini viongozi wenyewe wanapiga chenga na kuikimbia.
 
Leo nimelala sana mpaka saa nane mchana, tatizo ni hii katiba, tunahitaji katiba mpya.

Pia wife kazidisha chumvi kwemye mboga, bila katiba mpya atatuua kwa kisukari na presha
Haichekeshi.
 
CCM ni mtoto aliedekezwa na dola baada ya kuhakikishiwa hata aharibu vipi dola itamlinda!!

Matokeo take kabweteka hasikilizi wananchi

Lakini kamadola ingekua inafanya tathmini ya ccm kama inastahili ama lah,vyama vingine vingepewa navyo vionyeshe uwezo na ccm chama changu kingekua chama Bora kikiogopa kupoteza dola!!

Adui mkubwa wa CCM ni Dola yenyewe kuilinda na kuidekeza madhara take ndio haya,haisikilizi kero za wananchi na wanalea wezi ndani ya chama!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom