Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,308
- 9,737
Ndugu zangu Watanzania,
Sasa ndio nieleweke vizuri napoandika mara nyingi humu jukwaani kuwa Mdude Nyagali hayupo sawa kichwani, ana matatizo kichwani yanayohitaji matibabu ya haraka na dharura. Sasa katika mtandao wake wa Twitter ambao kwa sasa unafahamika kama X Ameweka picha ya mtoto wa Benjamini Netanyau akiwa na Baba yake waliyopiga mwaka 2017 ,na kusema kuwa ni ya mwaka huu akiagana na baba yake kwenda vitani kupigana katika vita inayoendelea kwa sasa, jambo ambalo siyo la kweli na picha hiyo siyo ya mwaka huu.
Picha hiyo ambayo ameweka katika mtandao ilipigwa wakati huo kijana huyo wa Netanyau anatoka jeshini katika mafunzo ambayo wa Israel wote hupitia kwa lazima kama sehemu ya utamaduni wao wa utayari wa kuilinda na kuipigani nchi yao ikitokea vita kama ilivyo sasa. Kwa ufupi ni kama tulivyo na mafunzo ya mujibu wa sheria ambayo hutolewa na JKT kwa vijana mbalimbali kila mwaka kwa hapa kwetu na ambayo siyo sehemu ya ajira bali ni sehemu ya kuwajengea vijana ukakamavu,utayari wa kulipigania Taifa ,uzalendo na kujifunza stadi za maisha na kujitegemea pindi warudipo mitaani kwa kuwa mfano wa kuigwa katika jamii.
Sasa yeye Mdude akabandika picha hiyo ya muda mrefu na kuleta upotoshaji wake katika karne hii ambayo teknolojia imekua kubwa sana.
Sasa kwa akili yake mbovu na fyatu na iliyokosa muelekeo amejikuta anadanganya habari hiyo kwa kufikiri wote wana akili ndogo kama yake ya kukurupuka na kutofuatilia mambo yanavyokwenda ulimwenguni. Ameweka picha hiyo katika adhima ya kuchafua watoto wa viongozi wetu kwa kusema kuwa wakati mtoto wa Netanyau anaagana na baba yake kwenda vitani watoto wa viongozi hapa nchini wanafanya ufisadi na kugawana fedha za ufisadi.
Hapo ndio muielewe vyema akili ya Mdude kuwa haipo sawa na pia kichwa chake hakipo Timamu.Ni mtu wa mihemuko,kukurupuka, kuropoka na kuongea vitu pasipo kuwa na balansi ya akili na mdomo Wake. Niwaombeni watanzania wenzangu mumpuuze Mdude kwa kutambua kuwa hajitambui na wala hajielewi na ndio maana anafanya hayo afanyayo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Sasa ndio nieleweke vizuri napoandika mara nyingi humu jukwaani kuwa Mdude Nyagali hayupo sawa kichwani, ana matatizo kichwani yanayohitaji matibabu ya haraka na dharura. Sasa katika mtandao wake wa Twitter ambao kwa sasa unafahamika kama X Ameweka picha ya mtoto wa Benjamini Netanyau akiwa na Baba yake waliyopiga mwaka 2017 ,na kusema kuwa ni ya mwaka huu akiagana na baba yake kwenda vitani kupigana katika vita inayoendelea kwa sasa, jambo ambalo siyo la kweli na picha hiyo siyo ya mwaka huu.
Picha hiyo ambayo ameweka katika mtandao ilipigwa wakati huo kijana huyo wa Netanyau anatoka jeshini katika mafunzo ambayo wa Israel wote hupitia kwa lazima kama sehemu ya utamaduni wao wa utayari wa kuilinda na kuipigani nchi yao ikitokea vita kama ilivyo sasa. Kwa ufupi ni kama tulivyo na mafunzo ya mujibu wa sheria ambayo hutolewa na JKT kwa vijana mbalimbali kila mwaka kwa hapa kwetu na ambayo siyo sehemu ya ajira bali ni sehemu ya kuwajengea vijana ukakamavu,utayari wa kulipigania Taifa ,uzalendo na kujifunza stadi za maisha na kujitegemea pindi warudipo mitaani kwa kuwa mfano wa kuigwa katika jamii.
Sasa yeye Mdude akabandika picha hiyo ya muda mrefu na kuleta upotoshaji wake katika karne hii ambayo teknolojia imekua kubwa sana.
Sasa kwa akili yake mbovu na fyatu na iliyokosa muelekeo amejikuta anadanganya habari hiyo kwa kufikiri wote wana akili ndogo kama yake ya kukurupuka na kutofuatilia mambo yanavyokwenda ulimwenguni. Ameweka picha hiyo katika adhima ya kuchafua watoto wa viongozi wetu kwa kusema kuwa wakati mtoto wa Netanyau anaagana na baba yake kwenda vitani watoto wa viongozi hapa nchini wanafanya ufisadi na kugawana fedha za ufisadi.
Hapo ndio muielewe vyema akili ya Mdude kuwa haipo sawa na pia kichwa chake hakipo Timamu.Ni mtu wa mihemuko,kukurupuka, kuropoka na kuongea vitu pasipo kuwa na balansi ya akili na mdomo Wake. Niwaombeni watanzania wenzangu mumpuuze Mdude kwa kutambua kuwa hajitambui na wala hajielewi na ndio maana anafanya hayo afanyayo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.