Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Up Date
===
"Vyama vya siasa ama siasa ni kama ilivyokuwa dini, isipokuwa tunafofautiana tu katika itikadi lakini lengo letu ni moja tu kuhakikisha tunaleta maendeleo"
"Kwanza nilikuwa nawaza ni maaskofu gani wataweza kuvaa viatu vya Desmond Tutu aliyepata tuzo ya Nobel, sasa naanza kuona kumbe Tanzania wapo maaskofu hao."
"Kwanza natoa shukrani kwa viongozi wa dini waliofanya kazi ya kupiga kelele kubwa sana baada ya tukio langu kutokea."
"Kutoka ofisini kwangu hadi Kituo cha Polisi ni mita 300 na kutoka ofisini kwangu hadi kwenye makazi ya polisi ni mita 50 na wakati askari wanafanya gwaride nikiwa ofisini kwangu nawasikia na lengo la mimi kupiga kelele ilikuwa ni kutaka msaada"
"Wale watu hawakuwa na hoja walichokifanya mmoja wa wale watu akawaambia wenzake shika kwanza simu na begi lake hivyo ndivyo vitu vya muhimu, hapo ndipo nikaanza kuwatilia shaka"
"Mtekaji mmoja akajitambulisha kuwa yeye ni Polisi wamekuja kunichukua ili wakanihoji. Unajua mimi siku zote ni mdadisi na nikamhoji yule bwana, unanichukua kwa kosa gani, akasema wewe unatuhumiwa kwa kumtukana na Rais na Serikali huko mitandaoni"
"Mh. HecheJohn na godblesslema waliwahi kunifanyia mpango nikaishi Nairobi, kutokana na aina ya maisha ambayo naishi lakini nikakataa kwa sababu ninayofanya ni kwa mujibu wa Katiba ya nchi"
"Tangu Rais ameingia madarakani mimi nimekuwa mkosoaji mkubwa wa Serikali na ndiyo maana nawaambia kutekwa kwangu ni kutokana na itikadi za kisiasa
"Katika Ofisi yangu nimetengeneza grili ili nikuhudumie ukiwa nje ya grili na nilifanya hivi ili polisi wakija kunikamata bila kufuata utaratibu wa kisheria nitoe taarifa na niripoti kwenye mitandao ya kijamii"
"Mimi sikupotea, nilitekwa na kutekwa kwangu kumetokana na masuala ya kisiasa kutokana na itikadi yangu"
"Sisi hatuamini katika kutekana, tunaamini katika kujenga hoja"
"Mmoja wa wale watekaji akanishikia bastola na mimi kwakuwa nilishaanza kuona harufu ya kifo nikasukuma ile bastola"
"Kitu cha kushangaza kelele zangu za kutaka msaada zikaishia kujaza watu na siyo askari"
"Nikiwa kwenye gari watekaji walinipiga kwa chupa za bia, wakawa wanasema unatuuliza maswali ya kijinga! unatuomba vitambulisho sisi"
"Nikiwa ndani ya ile gari nikawa naendelea kupambana, na ili kujua kama kulikuwa na gari mbili mmoja alimpigia simu dereva wa gari nyingine akimwambia kuwa hiyo gari inayotufuatilia iwekwe kati"
"Mmoja ya wale watu watatu akatoa silaha aina ya bastola halafu akaikoki na ikatoa mlio ili kuwatisha wananchi waliokuwa wanataka kunipa msaada ili waogope"
"Nilipigwa mpaka macho yakavimba na kichwa kikavimba kama mapapai ya Tukuyu maana kile kipigo cha Polisi sijui kinaingia mara ngapi kwa kipigo cha hawa jamaa"
"Wale watekaji wakasema sisi siyo wale wa mara ya kwanza waliokuchukua wakakutesa uchi na kukupeleka Oysterbay na tutakuonyesha sasa"
"Tunapozungumzia Uchumi hatuzungumzii barabara, hatuzungumzii Ndege, Mwalimu nyeree aliomba Uhuru ili sisi tuwe na uhuru wa kuhoji, uhuru wa kujitawala sisi wenyewe"
"Vitu vinavyothibitisha kuwa tukio langu la kutekwa ni la kisiasa, ni tweets zangu za mara ya mwisho kuhusu yule wakili aliyepotea, Ziara ya Rais Mbeya alipokuwa uyole na kuhusu ripoti ya IMF"
"Mimi nilikata tamaa ya kuendelea kuishi na nilishaomba sala ili Mungu aipokee roho yangu, mwacheni Mungu aitwe Mungu, Mungu ni fundi"
"Wasamalia wema walivyonipeleka kwa mwenyekiti wa kijiji, kitu cha kwanza niliomba maji, mwisho wa siku wakesema umekula nikasema nimekula jioni ya leo nikijua ni siku hiyo hiyo, wakasema wewe si umepotea toka juzi, wakaniandalia kwanza uji"
"Moja ya vitu ambavyo vinashangaza, sikuguswa maeneo mengine zaidi ya kupigwa kichwani, lakini cha kushangaza baada ya kupata fahamu nikakutwa nina majeraha mikononi na kwa mujibu wa wataalamu ni majeraha yaliyotokana na kufungwa pingu"
"Mpaka napoteza fahamu sikuwa na majeraha mgongoni lakini nilipofika hospitali nikakutwa nina vidonda mgongoni"
"Je mimi kuhoji tu pesa iliyotumika kutengeneza vitambulisho vya wajasiriamali imetoka wapi ndiyo natumika na Mabeberu kweli?"
"Kama siyo tukio la kisiasa kwanini wang'ang'anie begi langu ambalo lina nyaraka zangu nilizowashtaki Polisi, kwanini waniambie niwaite Umoja wa Mataifa waje wanisaidie, kwanini waniambie Mbowe aje anisaidie"
"Kama kuhoji kuhusu matumizi Serikalini ni kutumika na Mabeberu wacha nitumike"
"Mtu ambaye mimi kwangu ni mtuhumiwa namba moja kutokana na tukio langu la kutekwa ni RPC wa Songwe ambaye sasa kwa sasa amehamishwa, na huyu yupo kwenye orodha ya watu niliowashtaki"
Kuhusu kubadili msimamo wake Mdude amesema, "Kazi ya sikio haiwezi kuwa kazi ya pua, sikio litabaki kufanya kazi yake na pua itabaki kufanya kazi yake, siwezi kubadili msimamo wangu mimi ndivyo nilivyo"
"Mwizi huwa hajichunguzi, kama kweli wanalichukulia kwa uzito suala la kutekwa kwangu kwanini wasiite FBI waje kuchunguza mara moja?"