Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Msambaa mmoja aliomba lifti katika Fuso iliyokuwa imebeba sanduku tupu la kuzikia.akiwa safarini,mvua ikaanza kunyesha,msambaa akafunua sanduku akazama ndani,kisha akajifunika kujizuia na mvua.Hawakufika mbali,mdigo naye akaomba lifti.Mdigo alipopanda nyuma ya fuso,kuliona sanduku,alipata woga mkuu,akakaa nalo mbali kabisa akijua ndani kuna maiti.Mara baada ya mvua kukata,msambaa ndani ya sanduku alikohoa kidogo kisha akausukuma mfuniko wa sanduku ili atoke.Kilichotokea ni balaa.....Mdigo alijirusha nje akijuwa marehemu kafufuka,fuso nayo ilikuwa 120,mdigo mpaka leo hana meno ya barazani yani ana dental formula ya njiwa!