Mdahalo: Kids Vs Spouses

lizzy pamoja na yote naamini huwa kuna chapa tayari anakuwa ameiacha kwenye maisha yako na kila ukiangalia wanao kuna kivuli kinakuja kwanza ambacho ni baba wa wanao... Huwa inakuaje pale watoto wanapokuwa wakubwa na miji yao bado huwa wanaendelea kuwa wa kwanza kuliko wenzi wetu
 
Nimei-print hii na kuitengenezea frame na kui-hang ukutani hapa ofisini
 
Ewaaaaaaaaa! Umeniwahi! Nlitaka kuchokoza hii kitu aisee! Manake nikimwona mama yangu saa hizi kabakia na mmewe, siye wanae huku tuko busy na familia zetu.

Mi kamke kangu kataendelea kuwa namba wani aisee, haka ndo ka kufa na kuzikana bana!
 
Sijawahi kufikiria kuweka kipimo kati ya watoto wetu na mke wangu - na nadhani kufanya ni DHAMBI ya Umauti [Mortal SIN] - kwahiyo mimi kwangu "they all come first" ...


Siku njema
 

Ashadii huwa napenda sana kusoma post zako kwani nanufaikaga nazo kwa sana tu. Ila hapo bold huyu baba wa binti yangu alinitelekeza kisa hiyo nyumba ndogo lol. Ila anampenda huyu binti yangu kuliko maelezo hapindui kabisa. Mimi naamini upendo kwa mtoto ni tofauti na upendo kwa mume/mke. Wako tofauti kabisa haiwezekani kulinganisha.
 
Fo most men japo ukiwauliza watakwambia ni kids in real sense ni wife ana come first; for women kids come first then husband.

Nasema hivi kwa kuwa nina mifano lukuki ambayo inaonyesha wababa wengi wakimchukia mke wanachukia na watoto; penzi kwa watoto linatokana na penzi la baba kwa mama.

Nakubali kuwa si wote; wapo wanaume wachache makini ambao hata awe na penzi kwingine watoto wake ni number one ila ni wachache sana.
 

Kwanza kabisa, shikamoo babu............🙂

Pili, Msimamo wako babu umenifurahisha sana...............hongera kwa kulitambua hilo.

Kwangu mimi, bila mume wangu hawa warembo ambao Mungu amenijalia nisingekuwa nao. So, mume wangu ana nafasi yake pekee, na watoto wangu wana nafasi yao.

Mbarikiwe wote.
 
Kajukuu hapa tunaongelea Mmeo uliyezaa naye Watoto Wako!...........Please!

Let me put like this: Inapotokea mmeo na mwanao (wa kuzaa na mmeo) lets say wanaumwa na wote wanahitaji kuwekewa figo. Utajitolea figo lako moja kwa nani?

Babu bwan a....kama nilivyosema uamuzi utakaochukuliwa hapa hautakuwa umeamuliwa kwa kigezo cha kumpenda mtoto zaidi ya mume au mume zaidi ya mtoto. Inategemea na vitu vingi babu nitajaribu kuviweka
1. Umri wa mtoto/ndoa - Inawezekana watu tukawa na maamuzi tofauti mf. mwingine anawezaamua kureason kuwa kwa kuwa ndoa bado ni changa na mtoto bado ni mdogo basi atayafanya maamuzi magumu na kumsave Spouse. Unless akubali kuwa widow at that tender age.
2. Mtoto mkubwa/ ndoa imekwenda age- unlike wanaume ambao wao wanawezaoa muda wowote, wanawake wengine hupoteza hamu ya kuolewa tena au kuwa kwenye mahusiano. So wakati ambapo mwanaume anawezaamua bora nimsave mtoto, mke nitapata mwingine, wanawake wengine husema hata nikimsave mume na kwa kuwa umri umekwenda hatutowezapata mtoto mwingine na yeye haoni posibility ya kuolewa tena- anachagua kusave mtot.

Lakini si kwa kuwa anampenda zaidi mtoto kuliko mumewe!

Lakini bado bwana trade-off ni ngumu bana
Leo nadhani nimekunywa gongo hata sijui ninachoandika hapa au ni kwa vile ninaamini kuwa havilingani!
 
Kwangu (no matter what), mke wangu (my sweet love, soul-mate) ni primary...wengine wote wakiwemo watoto wangu, wazazi na ndugu ni secondary and tertiary!!

Nitasema hivyo hadi pumzi yangu ya mwisho!!
 

MJ1,
Nakubaliana na wewe hapo kwenye red, 100%. Kila mmoja ana nafasi tofauti kabisa.

Ubarikiwe
 
naomba nikupinge kidogo iyo ni imani tuliojiwekea nafikiri MJ1 amegusia mahali ati baba/mama akipenda watoto na kufanya kila kitu in real sense anampenda mkewe mie nakataa mpaka mwisho ukiona umefika level maisha yako yanakuwa influenced zaid na watoto na priorities kwako ni wao lazima some perc ya mapenzi yatakuwa yamepungua kama si kupotea kabisa na kuna mambo mengi utakuwa unampunja mwenza wako bila kujua au kujua
 
Chauro,

Nimekupenda ghafla bin vuu!!!

Ubarikiwe sana!


Chauro,upendo haubagui,kwamaana halisi ya upendo ni kuwa hakuna aliezaidi ya mwingine,labda kwa tafsiri potofu ya upendo!

Kumpenda sana mke na kumpa nafasi ya kwanza si kubagua....After all, huwezi kupenda vitu au watu wote kwa kiwango sawa...Labda Mungu tu ndiye tunaamni anatoa equal share ya upendo!

Babu DC
 
Na mimi nimelikemea kuwa its not right! Ni kujinyima haki yako kama mke! Wababa wengine wanakukaripia, unalalamika nini, kwani situnzi watoto?! Watoto ni watoto, mke ni mke kila mtu anayo haki yake unayotakiwa kumtimizia the same applies kwa mwanamke..... hakuna eti oh nampenda sana mwanangu kuliko baba yake no way bana.........unless sasa tuingize vigezo vingine ndani ya hii linear equestion

Upendo wa watoto = Upendo wa spouse
Unless uanze kuingiza confronting variables kama labda spouse alishawahi kukuumiza, kucheat n.k then unawezasema unawapenda watoto zaidi ya spouse.
 
Kwangu mimi spouse comes first before kid. Swala la kizushi kwa wababa,ikitokea wife wako yuko labor na something happens and you as the hubby/dad unatakiwa uchague kuokoa maisha ya mmoja,who wil u save?wife au kid?

Hahahahahahahah,

Mbona hilo ni swali dogo sana...Hivi unawezaje kulinganisha mtu unayemjua na mgeni??

Zamani zetu walikuwa wanatufundisha kuwa,..... as longer as kiwanda hakijifungwa....bidhaa nyingine zitatengenezwa tu...Kwa hiyo ni wazi kwamba huwezi kukimbia na bidhaa ukaacha kiwanda...!! .....Sina hakika kama vijana wa siku hizi bado wanayaamini hayo!

Babu DC
 
Thinking by head not by heart nilichosema ni kweli kwa asilimia kubwa.

What you can argue ni kuwa siyo right lakini ndio reality.

Ni wanaume wangapi umeshawaona waliobobea kwa vimada wakakumbuka kuwa wana watoto???

Ni wamama wangapi wenye vidumu wakakumbuka wana watoto??

Ukijaribu kupima hapo ndo utajua nasema nini.

Nachosema si kuwa ni right but that is the way it is.
 
The biggest mistake i see in some few mothers.

Kuna wamama wanaweka uhusiano wao na watoto wao ahead kuliko uhusiano wake na mume wake.

Kuna tatizo gani kwenye hili

1. Two married people are one flesh. A parent and a child don't have that relationship
2. To exalt the child over your spouse is to teach your child the spouse is not important
3. Children learn early if they can pit against the other

Haya huwa sio makosa ya mama

1. Sometimes a dad is elusive and stays in the background on purpose, hataki kujishugulisha na kujihusisha na watoto
2. Sometimes the in-laws interfere heavily with a mother and father God's given right to raise their own children
3. And yes, sometimes mothers express more love and attention to the kids than to dad

The Bible is clear on how husbands and wives are to be considered the male and the female side of the same person. One flesh. One unit. That's why the devil didn't touch Job's wife. She was part of him and God said for the devil not to kill Job, therefore he couldn't kill his wife, either.
 
hv wanaume wanagawaje malove yao
wife?%
nyumba ndogo%?
Makid%? Hapo tena anagawa maana watoto wa kike hawawezi kupendwa sawa na wakiume
.

Hapo hakuna mgawo wa aina yoyote....Number moja na queen wao ni mama watoto......Then watoto wanamwibia mama vipande kidogo kidogo kidogo vya upendo....(ki ukweli wana aina yao ya upendo..may be nitapata nafasi ya kuulezea baadaye!!). Hakuna upendo wowote kwa nyumba ndogo...Ni usanii na maslahi tu....!!! Labda wadau watanipinga kwa disqualify base yangu ya lack of experience!



For those who are still hunting....you are, the best and a rare catch!

Babu DC
 
Nakubaliana na wewe 100%

Labda tuanzishe thread ya ni jinsi gani wanandoa wataweza kugawa penzi jinsi inavyopaswa kwa wenza na watoto wao.

Reality inaonyesha wengi wanashindwa kubalance.

Na tunakubali kuwa si sawa kufanya hivyo

Sasa what is the cause and solution ni more important than kupretend kama hili tatizo halipo.

One may say kuwa nampenda mume wangu kwa sababau ni baba wa watoto wangu and bla bla bla; but what she does is not what she says.

Na mwingine anaweza akasema my wife comes first and bla bla bla lakini kimatendo ni opposite especially atakapo kuwa kwenye conflict na mkewe.

Kwa hiyo tuongelee uhalisia hata kama tunakubali wote kuwa si tunavyotaka iwe; ili tusolve tatizo baada ya kujua kiini.

Mfano mimi kuna kitu nili observe; wamama wengi ambao wame loose trust kwa waume zao hasa kwa sababu ya serial cheating wanapeleka mapenzi yao kwa watoto. Nina rafiki yangu umwambii kitu kuhusu watoto wake. Na sababu inaweza kuwa ni uhakika wake kuwa the kids will always be hers but not the husband.
 
Umekwepa swali ehhh??

Nwy tunarudi pale pale kwenye THAMANI babu!!
Kusema hivyo hakuna maana kwamba upendo ndio unaolinganishwa bali thamani/maana/umuhimu na mengineyo.
MTM anachomaanisha (samahani kama nitakua nimekosea) ni kwamba iwapo itatokea mtu akataka kuumiza familia yake na akawa kwenye nafasi ya kuweza kulinda upande mmoja atalinda watoto. Mapenzi ya mke bado yapo pale pale...na ya watoto yako pale pale ila anachoangalia ni nani ambae hataki katu katu kumpoteza. Yani yupi ni irreplaceable kwake...thamani/muhimu zaidi.



Kajukuu hapa tunaongelea Mmeo uliyezaa naye Watoto Wako!...........Please!

Let me put like this: Inapotokea mmeo na mwanao (wa kuzaa na mmeo) lets say wanaumwa na wote wanahitaji kuwekewa figo. Utajitolea figo lako moja kwa nani?

If mine is a match to both...DEFINATELY MTOTO!!Mume atatafutiwa nyingine!!
 
Sijawahi kufikiria kuweka kipimo kati ya watoto wetu na mke wangu - na nadhani kufanya ni DHAMBI ya Umauti [Mortal SIN] - kwahiyo mimi kwangu "they all come first" ...


Siku njema

Ni ya kweli hayo mzee wa Bugene???
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…