Midavudavu
JF-Expert Member
- Jan 23, 2012
- 287
- 59
Yupo katekista mmoja alikuwa mlevi sana wa pombe. Hata hivyo ulevi wake haukuwa kikwazo katika kazi zake za kuchunga kondoo wa Bwana, aliaminiwa kanisani. Jirani na kanisa analofanyia kazi katekista huyo mlevi kulikuwa na makaburi ambayo yalizungushiwa uzio. Basi siku moja Palitokea wezi wawili ambao usiku wa saa 6 waliiba maembe jirani na makaburi hayo.
Waliweka maembe haya katika viroba na kukubaliana kuwa waende makaburini kugawana sawa kwa sawa. Kwa kuwa makaburi hayo yalikuwa njiani wakakubaliana wakati wanagawana maembe watumie lugha tofauti ili kama wapita njia wakiwasikia wasijue nini kinafanyika. Wakaweka maembe juu ya kaburi na kuanza kugawana moja moja huku wakisema "wangu huyu" na mwingine anasema "wangu huyu".
Ikatokea wakati katekista mlevi anapita akasikia sauti zikitokea makaburi za "wangu huyu", "wangu huyu". Akakimbia hadi jirani na nyumba moja ya kanisa alikokua anakaa mchungaji wake na kumuamsha. Akumwambia amka leo kuna balaa makaburini shetani na Mungu wanagawana watu; wabaya kwa shetani wema kwa Mungu. Mchungaji akamwambia muongo wewe, huo ulevi wako twende na mimi nikashuhudie.
Basi wakaenda, walipofika wakasimama nje ya geti la kuingilia makaburi. Mchungaji naye akasikia sauti zile za "wangu huyu, wangu huyu". Sasa kumbe wale wezi wakati wanapita pale getini na maembe walidondosha mawili, hivyo walipomaliza kugawana yale waliyokuwa nayo wakasema twende getini tukawachukue na wale wawili tuliowaacha.
Hapo ikawa kizaazaa na paytashika kati ya Mchungaji na Ketekista walitimua mbio kukimbilia kanisani . Walijua sasa muda wao wa kuishi dunia ulikuwa umekwisha na ni zamu yao kugawanywa. Cha ajabu japo mchungaji alikuwa mzee kuliko katekista lakini alikuwa wa kwanza kufika kanisani.
Jamani mbinguni kunatisha kama hujajiandaa, hata wachungaji wanapakimbia kwenda.
Waliweka maembe haya katika viroba na kukubaliana kuwa waende makaburini kugawana sawa kwa sawa. Kwa kuwa makaburi hayo yalikuwa njiani wakakubaliana wakati wanagawana maembe watumie lugha tofauti ili kama wapita njia wakiwasikia wasijue nini kinafanyika. Wakaweka maembe juu ya kaburi na kuanza kugawana moja moja huku wakisema "wangu huyu" na mwingine anasema "wangu huyu".
Ikatokea wakati katekista mlevi anapita akasikia sauti zikitokea makaburi za "wangu huyu", "wangu huyu". Akakimbia hadi jirani na nyumba moja ya kanisa alikokua anakaa mchungaji wake na kumuamsha. Akumwambia amka leo kuna balaa makaburini shetani na Mungu wanagawana watu; wabaya kwa shetani wema kwa Mungu. Mchungaji akamwambia muongo wewe, huo ulevi wako twende na mimi nikashuhudie.
Basi wakaenda, walipofika wakasimama nje ya geti la kuingilia makaburi. Mchungaji naye akasikia sauti zile za "wangu huyu, wangu huyu". Sasa kumbe wale wezi wakati wanapita pale getini na maembe walidondosha mawili, hivyo walipomaliza kugawana yale waliyokuwa nayo wakasema twende getini tukawachukue na wale wawili tuliowaacha.
Hapo ikawa kizaazaa na paytashika kati ya Mchungaji na Ketekista walitimua mbio kukimbilia kanisani . Walijua sasa muda wao wa kuishi dunia ulikuwa umekwisha na ni zamu yao kugawanywa. Cha ajabu japo mchungaji alikuwa mzee kuliko katekista lakini alikuwa wa kwanza kufika kanisani.
Jamani mbinguni kunatisha kama hujajiandaa, hata wachungaji wanapakimbia kwenda.