Nikianza na wabunge baada ya Jemedali kijana makonda kujitoa mhanga kupambana na wauza unga ,nyiyi kwa mara ya kwanza tuliwaona mkiungana katika bunge tukufu kubariki propaganda za makaburu kumzima makonda. Naona mmefaulu ila jiulizeni kwa faida ya nani na ninawambieni siku mwanao akirudi likizo ni teja ndo utakumbuka tujipe mda.
Pili wewe mwanadamu ambaye unasari kila siku ilikuwa ni aibu kubwa tena sana mbele ya Mungu kuacha vita ya kusaport jitihada za kijana wenu na kuhamia upande wa wapiga dili kisa ushabiki wa vyama, kwa akili ya kawada vyeti feki, au kusoma kwa jina la m2 hata kama ni kweli na kuzuia uuzaji wa unga unaoangamiza taifa letu bila, kubebewa akili lipi kama taifa inabidi tusimame na tulikemee la kwanza kwa mstakabali wa nchi hii. leo hii unaamka m2 mzima na familia yako mnashabikia habari za vyeti badala ya kupambana na wauza madawa? hivi tumelaniwa na nani?
Tatu niwakumbushe wanasiasa uchwara mlioamua kuyumbisha nchi hii kwa kuchafua majina ya watu na kuzima ndoto zao wakifukuzwa upande wa pili mnawakaribisha upande wenu na kuiacha jamii imeduwaa!! hizo siasa kwamwe haziwezi kukiondoa chama tawala madarakani ila zinadumaza upinzani ambao ni kiungo muhimu kwa msitakabali mwema wa nchi yetu, leo hii mmegeuka genge la kuficha wahalifu mliowatuhumu nyiyi hata kama ni pesa msihujumu nchi yenu kiasi hicho ioneeni huruma Tanzania.
Mwisho tunajua waunza unga mnapesa nyingi mnaweza kununua media zote mkapotosha lengo kwa propaganda, ila kumbukeni mfanyayo kuwageuza watoto wa wenzenu mateja huku nyie mkienda mitamboni kujigamba kwamba hamtumii hata kama mlipimwa Mungu atalipa, ijazeni nchi yetu mateja na nyinyi jengeni magorofa na mruke na mahelkopita ila Mungu siku atalipigania taifa lake. Hongereni kwa kumzima makonda na niwatakieni biashara njema ya uuzaji madawa ya kulevya
wasalaaam
WAZIWAZI