tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,835
- 18,249
Katika hali isiyokuwa ya kawaida na ambayo ni kinyume na mafundisho ya kidini (kiislamu na kikristo), mchungaji mmoja wa kike amewashauri wachumba kutestiana mitambo kabla ya kuingia kwenye ndoa.
Mshauri huyo wa ndoa alitokea kutoa mwanga zaidi kuhusu ni kwa nini kutalikiana kumekuwa jambo la kawaida katika jamii ya leo. Mchungaji mmoja wa kike kutoka nchini Ghana ambaye pia anajiongeza kama mshauri wa masuala ya ndoa, Dkt Nana Yaa Prempeh amekuwa gumzo mitandaoni baada ya kuwashauri akina dada nini cha kufanya kabla ya kukubali kuingia katika ndoa.
Kaitka video ambayo imesambaa mitandaoni, mchungaji huyo alikuwa akizungumza kwenye runinga moja nchini humo wakati alifunguka kwamba yeye ni mmoja wa wanawake wenye filosofia ya ‘kuona na kuhakikisha uume unafanya kazi kabla ya kuamua ndoa’.
Mchungaji huyo amesema ndoa nyingi zinavunjika siku hizi baada ya mmoja wa wanandoa kugundua mitambo ya mwenzake haimridhishi hivyo kupelekea ndoa nyingi kukata roho.
“Mimi ni miongoni mwa wanawake wa Mungu ambaye nadhani kabla ya kuolewa na mwanaume lazima uuone uume wake. Lazima uione, lazima uishike, lazima uisikie na uhakikishe inafanya kazi.”
Baada ya maneno hayo kutamkwa bila kutarajia mtangazaji wa kike aliyekuwa anaongoza mahojiano hayo, aliomba kunywa maji na mchungaji huyo alimuuliza mbona kama ameshtushwa na maneno yake.
“Ah, mbona unakuwa na wasiwasi hivyo?” mchungaji huyo alimuuliza mtangazaji naye akamjibu, “ngoja kwanza ninywe maji kidogo.”
Hii hapa chini ni video hiyo ambayo imezua taharuki mitandaoni kuhusu baadhi ya mafundisho ambayo watumishi wa Mungu wanafundisha siku hizi hasa katika suala zima la muunganiko wa mume na mke kuanzisha familia.
View: https://youtu.be/7XGaqwJw-tw
Mshauri huyo wa ndoa alitokea kutoa mwanga zaidi kuhusu ni kwa nini kutalikiana kumekuwa jambo la kawaida katika jamii ya leo. Mchungaji mmoja wa kike kutoka nchini Ghana ambaye pia anajiongeza kama mshauri wa masuala ya ndoa, Dkt Nana Yaa Prempeh amekuwa gumzo mitandaoni baada ya kuwashauri akina dada nini cha kufanya kabla ya kukubali kuingia katika ndoa.
Kaitka video ambayo imesambaa mitandaoni, mchungaji huyo alikuwa akizungumza kwenye runinga moja nchini humo wakati alifunguka kwamba yeye ni mmoja wa wanawake wenye filosofia ya ‘kuona na kuhakikisha uume unafanya kazi kabla ya kuamua ndoa’.
Mchungaji huyo amesema ndoa nyingi zinavunjika siku hizi baada ya mmoja wa wanandoa kugundua mitambo ya mwenzake haimridhishi hivyo kupelekea ndoa nyingi kukata roho.
“Mimi ni miongoni mwa wanawake wa Mungu ambaye nadhani kabla ya kuolewa na mwanaume lazima uuone uume wake. Lazima uione, lazima uishike, lazima uisikie na uhakikishe inafanya kazi.”
Baada ya maneno hayo kutamkwa bila kutarajia mtangazaji wa kike aliyekuwa anaongoza mahojiano hayo, aliomba kunywa maji na mchungaji huyo alimuuliza mbona kama ameshtushwa na maneno yake.
“Ah, mbona unakuwa na wasiwasi hivyo?” mchungaji huyo alimuuliza mtangazaji naye akamjibu, “ngoja kwanza ninywe maji kidogo.”
Hii hapa chini ni video hiyo ambayo imezua taharuki mitandaoni kuhusu baadhi ya mafundisho ambayo watumishi wa Mungu wanafundisha siku hizi hasa katika suala zima la muunganiko wa mume na mke kuanzisha familia.
View: https://youtu.be/7XGaqwJw-tw