Mchumba wangu ameniuliza "Lowassa ndio nani?"

Amicus Curiae

JF-Expert Member
Sep 12, 2012
4,809
6,342
Natumaini jumapili ya leo ni njema kwetu sote.

Katika harakati za kutafuta mwenza wa maisha, nimefahamiana na binti mmoja wa Kilokole ambaye ni mtoto wa Mchungaji wa moja ya Makanisa ya Kipentekoste ambapo na mimi naabudu.

Kabla sijampokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yangu, nakiri kuishi maisha yaliyotawaliwa na uzinzi na starehe za kila aina kama ulevi n.k.

Baadaye nikapata neema ya kuokoka. Nikajikuta nasali Kanisa 'X' ambamo ndio nimekutana na huyo binti wa miaka 23, mhitimu wa kidato cha 4 mwaka 2022, mrembo sana, Mcha Mungu, mwanakikundi wa kikundi cha Maombi Kanisani na muimbaji hodari wa nyimbo za Injili. Kabila ni muha.

Nina miezi 9 hapa Kanisani lakini nina miezi 2 tangu nifahamiane nae. Nimejiridhisha pasina shaka kwamba binti ni bikira. Na msimamo wake ni kwamba hatafanya zinaa mpaka siku atakayoolewa.

Baada ya kupendekeza wazo langu kwake akaomba nimpe muda wa kunichunguza. Alipojiridhisha kuhusu mwenendo wangu akaridhia ombi langu kwa sharti la kutofanya nae zinaa mpaka siku ya ndoa!

Bado hatujamshirikisha baba yake ambaye ni Mchungaji kwasababu na mimi nilimuomba anipe muda nijitafakari kama kweli niko tayari kutomuingilia kimwili kabla ya ndoa. Ukizungumza na huyu binti utagundua kwamba bado ni mshamba sana, ameshatembea mikoa 2 tu, mkoa mmoja ukiwa ni wa Shule aliyomaliza kidato cha 4.

Kwa sasa ni mjasiriamali kwasababu hakufanya vizuri kidato cha nne, malengo yake ni kusoma masomo ya uuguzi na sifa anazo.

Leo baada ya kutoka church tukaenda mahali kupata chakula cha mchana, ameniuliza swali la ajabu sana, kwamba Lowasa ni nani? Nadhani amekutana na taarifa za kifo cha Lowasa mitandaoni. At first nilidhani anatania, baadaye nikagundua alikuwa serious kwamba hamjui Lowasa!

Sasa wakuu, mwanamke wa hivi, ambaye amemaliza kidato cha 4 na amepata daraja la 3 la mwisho, inawezekanaje akawa hamjui Hayati Lowasa?

Kwa mtazamo wenu, anaweza akawa mama bora wa familia? Kiukweli ana exposure ndogo sana lakini ni mtafutaji mno. Anajielewa. Ana misimamo. Na anamtumikia Mungu katika roho na kweli.

Hebu tupeane uzoefu ili nisije nikajichanganya wakuu...
 
Hongera kwa kupata mchumba muimba kwaya aliye kwenye kikundi cha maombi church bila shaka atakua bikra mkuu
Kuhusu mambo ya wanasiasa utamchanganya huyo muulize habari za mitume na wake za manabii tu
Asante mkuu.

Bunti ni bikira kweli na ni muombaji sana, tena ni yale maombi ya kuzamia.

Nimependa hapo kwenye kumuuliza habari za mitume na manabii na sio maswala ya siasa
 
Unashangaa huyu mimi kuna jamaa tumesoma nae chuo x" hapa dar esalam (moja ya vyuo vikubwa )tumehitimu miaka ya hivi karibuni haifiki 7yrs lakini

Ajabu nae kaniuliza swali hilo , inaonesha alikuwa analifahamu jina ila akauliza kwani alikuwa ni nani nilichoka kidogo
 
Back
Top Bottom