Josaje Mtui
JF-Expert Member
- Oct 1, 2016
- 2,459
- 2,140
Mitungiii,kama ukitaka kuvinjari nasi basi mfukoni mwako uwe saaaafi
Atasema nimeongea na bwana wa majeshi......sasa nimewasamehe.....kila mmoja akalete box la bapa....Baadae atasema NIMEWASAMEHE
Wao waumini wake watauza madawa ya Kulevya. Imeandikwa "mtawatambua kwa matunda yao".Yaani hafikirii hata kuuza nyanya na vitunguu vinavyolika na watu wote anawaza gongo tu. Sijui waumini wake watauza nini akiacha kuhubiri.
NotedFake labda kwani bila kupanda mbegu hupati huduma wakati Yesu alitoa/anatoa bure na watumishi wa Mungu watoe BURE isipokuwa sadaka ni halali yao.
Dar es Salaam. Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo, maarufu Mzee wa Upako amesema waandishi wote wanaoandika habari za kumchafua watakufa kabla ya kufika Machi mwakani.
Kauli hiyo aliitoa jana ikiwa ni mwendelezo wa mahubiri yake ya nne katika wiki ya tatu mfululizo, akijibu yaliyoandikwa kwenye vyombo vya habari kuhusu kumfanyia fujo jirani yake na kulewa.
“Kila mwandishi aliyeniandika vibaya ikifika mwezi wa tatu akiwa hai, mimi naacha kuhubiri, nafunga virago nakwenda kuuza gongo, sasa Mungu ndiye ataamua kwamba ama niache kuhubiri mimi au wewe ufe …najua hata leo mpo humu mmekuja na mnasikiliza tu,” alisema.
Haya sasa wale wote mliosambaza taarifa za Mzee Wa upako ambazo anadai zililenga kumchafua mjiandae mwakani. je na wewe umo kati yao?
Mzee wa Upako: Wote Walionichafua WATAKUFA Mwakani......Wasipokufa Ntaanza Kuuza Gongo | MPEKUZI
Duh....
Na sisi tulio comment JF kuhusu yeye tutakufa?
Waandishi wakashtaki kutishiwa kuuliwa. ....
Sasa hii hatari viongozi wa dini mnaelekea wapi?
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo, maarufu Mzee wa Upako amesema waandishi wote wanaoandika habari za kumchafua watakufa kabla ya kufika Machi mwakani.
Kauli hiyo aliitoa jana ikiwa ni mwendelezo wa mahubiri yake ya nne katika wiki ya tatu mfululizo, akijibu yaliyoandikwa kwenye vyombo vya habari kuhusu kumfanyia fujo jirani yake na kulewa.
“Kila mwandishi aliyeniandika vibaya ikifika mwezi wa tatu akiwa hai, mimi naacha kuhubiri, nafunga virago nakwenda kuuza gongo, sasa Mungu ndiye ataamua kwamba ama niache kuhubiri mimi au wewe ufe …najua hata leo mpo humu mmekuja na mnasikiliza tu,” alisema.