Mchungaji aanzisha TUISHENI ya bure kanisani kwa wanafunzi wa sekondari

Heci

JF-Expert Member
Aug 14, 2016
3,485
5,818
77066789_2296936567079268_4370651130925940736_n.jpg

Mchungaji Kiongozi Wa Kanisa La Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika Wa Kimara,Dar es Salaam
Mchungaji Wilibrod Mastai ambaye pia ni Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wa KKKT Dayosisi ya mashariki na Pwani (Utawala,Utumishi na Milki) ametangaza mkakati wa kutoa mafunzo ya ziada ya bure kwa wanafunzi wa sekondari kwa kuwatumia walimu ambao ni washarika kanisani hapo.

Lengo la Mpango huo ni kuinua Kiwango cha Ufaulu kwa wanafunzi wa sekondari sambamba na ushauri nasaha.

Katika kile kinachoonekana kupata mwitikio Kwa Washarika walimu zaidi ya 30 walijitokeza huku mchungaji akielezea kuwa anaamini kutakuwa na matokeo mazuri .

Aliwataka Wazazi,Walezi na Washarika wa kanisa hilo wenye watoto wanaosoma kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne kuwaandikisha kwa ajili ya masomo ya muda wa ziada yatakayotolewa bure kila Jumamosi.

"Tumekuwa tunawaombea Wanafunzi Wetu kila inapofikia kipindi cha mitihani ya Taifa,Lakini nimeona kwamba kuna haja ya kutathimini na kusaidia maandalizi yao kwa kuwatumia walimu wetu ambao ni washarika hapa,pia kuna wataalam wa masuala ya ushauri nasaha watakuwepo ili kuwasaidi vijana kujitambua na kuendelea kuwa na maadili mazuri kwa manufaa ya kanisa na Taifa kwa Ujumla.
 
Ni wazo zuri sana saaaaaaaaaana...linafaa kuigwa na madhehebu mengine na kwa mfumo huu tutazalisha sio tu wanafunzi wenye ufaulu mkubwa bali pia kizazi kinachojitambua na chenye msimamo kupitia hiyo session ya ushauri na saha...Hongera sana baba Mastahi hakika una maono ya mbali sana na yanayofaa kupigiwa chapuo na sekta za elimu hapa nchini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lengo la Mpango huo ni kuinua Kiwango cha Ufaulu kwa wanafunzi wa sekondari sambamba na ushauri nasaha

Hongera kama kweli toka rohoni agenda ni hiyo, ila hao walimu wasiwe wameshinikizwa kwasababu binafsi, italigharimu kanisa
 
Hongera kama kweli toka rohoni agenda ni hiyo, ila hao walimu wasiwe wameshinikizwa kwasababu binafsi, italigharimu kanisa
Wenye imani haba hapa sio mahali penu.
Namjua Mastai napajua Kimara Korogwe. In case hupajui. Ni yale majengo kushoto kwako ukitokea Kimara Bucha kabla hujafika Kimara Korogwe.
 
Hongera kama kweli toka rohoni agenda ni hiyo, ila hao walimu wasiwe wameshinikizwa kwasababu binafsi, italigharimu kanisa
KAZI ya Mungu haina kushinikizwa, unajitolea tu, na hamna ambaye amewahi kupata hasara kwa kumtolea BWANA
 
Hii inafaa kuigwa
Naunga mkono .Kanisa Lina wasomi wengi Ni njia yao pia ya kubarikiwa kwa kutoa huduma za kijamii.Kusaidia vijana.Vijana wanahangaika Sana wasio na uwezo wanashindwa kupata tuition na ushauri nasaha hivyo kupelekea kufeli mitihani
 
Ukristo ni Mafanikio ya mwilini na rohoni pia
Mungu ndiye aliumba mwili ,nafsi na Roho .Vyoye vinatakiwa kufanikiwa sio kimoja kimoja Kama ambavyo viongozi wengine wa dini husisitiza kuwa mtu anatakiwa kufanikiwa kiroho tu wakati Mungu aliumba mwili,Roho na nafsi .Nampongeza Sana huyo mchungaji.Yuko sawa na imani yangu kwenye hili
 
W
Mungu ndiye aliumba mwili ,nafsi na Roho .Vyoye vinatakiwa kufanikiea sio kimoja kimoja Kama ambavyo viongozi wengine wa dini husisitiza kuwa mtu anatakiwa kufanikiwa kiroho tu wakati Mungu aliumba meili,Roho na nafsi .Nampongeza Sana huyo mchungaji.Yuko sawa na imani yangu kwenye hili
Well said 🙏
 
Hiyo jumamosi bora wangefanya kupumzika tu nyumbani na kuongea na wazazi wao.
Kwani jumatatu hadi ijumaa ni shule, jumapili ni siku ya sabato na jumamosi tena iwe ni kujifunza!!!! too much
Huyo mtoto atakua kabanwa sana.

Kipindi cha dini shuleni,
Ibada za nyumbani,
Ibada ya jumapili.
Zinatosha kwa mwanafunzi kujifunza neno la Mungu.

Hiyo jumamosi bora wangefanya huduma kwa wazazi jinsi ya kulea mtoto na kufatilia masomo ya mtoto shileni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom