Kila dini ina utaratibu wake:Mbona kwenye mada hukuweka wazi kua ww na mchumba wako mna imani tofauti?Kwenye Mada kunaonesha wote wawili mna imani moja,ni Waislam; Huku unabadilisha,oh.mm mkristo.Kama mna imani tofauti mbona mmeshamkwaza Ostazi,kitakachofuata hapo Ostaz hatofungisha ndoa na atawafukuzeni tu ili mkajipange upya kwenye suala la imani/dini.
Mwanamke wa kiislam atakasirika pale tu atakapoletewa mke wa tano,Hapo ndo utajua hasira za mwanamke wa kiislam..Hiyo timu ya wake 4 itakua wamoja na mtiti wake atakaoupata mume atajuta kuzaliwa.
Ktk imani ya Kiislam mwanaume akitaka kuoa mke wa pili,Uamuzi wa kuoa sio lazima amweleze/amshirikishe mke wake wa kwanza,(kutoa taarifa ni hiari ya mwanaume).Mke wa kwanza anaweza akapewa taarifa tu wakati jamaa ameshaoa;na huyo mke wa kwanza hana haki yoyote ya kukasirika au kuhoji kisheria,ila kama ana yake moyoni atatakiwa kuongea/kumuuliza mumewe kimapenzi wakiwa ndani ili kujua zaidi.Alikutaarifu kua baada ya mda ataoa mke wa pili kwa vile alishaamini kua wewe umeshabadili dini na unaelewa mafunzo ya kiislam,(na unaendelea kujifunza) ungekua ni mwanamke wa kiislam tokea zamani wala asingekueleza maana angejua unaelewa kila kitu.