Who Cares?
JF-Expert Member
- Jul 11, 2008
- 3,507
- 3,378
mmmmh inawezekana ulipokuwa arusha alikuwa na michepuko mingi so anakuzuga kuwa anadaiwa kumbe anaogopa kugonganisha
DMkuu huyo bibie ana tatizo la kisaikolojia na pengine linatokana na tamaa.Nina girlfriend nipo naye kwa miaka Tisa sasa. Nimeanza naye mahusiano akiwa na miaka 19. Nampenda na ananipenda. Namuhudumia vzuri tu. Na tayari nimemchumbia. Zamani hakuwa na tabia za kukopa vitu na kubaki na madeni. Ila sasa imekuwa balaa.
Nilipoingia kwenya ajira nilianzia kazi ofisi zetu za Arusha yeye akabaki Dar na hapo ndipo alipobadili tabia ambayo hakuwa nayo mwanzo. Japo nilikiwa mbali hakuna kilichobadilika kwa kumjali kwa matumizi yake. Ila sijui tabia ya kukopa kaitoa wapi Na nilishamkataza na nikamuambia akiwa na shida ruksa kuniambia na analijua hilo. Ila anapenda tu kukopa.
Baadae nikahamia kikazi kurudi mjini DSM. Yaani kila njia tukipita japo ni ndani ya gari ataniambia hapa tusipite na tukipita usishushe kioo flani ataniaona. Nikimtaiti anasema ananidai nilikopa wigi.
Hii tabia inanishinda sasa. Anadaiwa hadi kwenye vibanda vya baga. Saluni nyingi haendi ameacha madeni. Maduka zaidi ya sita maeneo ya kwao mikocheni anadaiwa. Wanafunzi aliomaliza nao udsm mwaka huu karibia mashosti wake wote wanamdai. Nishafanya juhudi zote kumkataza na kuyalipia madeni yake ila anarudia na anakopa tena.
NIFANYEJE?
Hii ni kweli kabisa.
Kuna mama mmoja namjua alifiwa na mdogo wake wa kike zamani kidogo.
Basi akawaongoza ndugu zake [siblings] katika juhudi za kwenda kwa waganga ili waweze kumrudisha [waliambiwa na mganga eti hakufa bali alichukuliwa ng'witunga, ni kama msukule flani hivi] huyo marehemu ndugu yao.
Mwisho wa siku wakaishia tu kuliwa hela zao na huyo ndugu yao wala hakurudi.
Pia, ninadhani hata huu utitiri wa akina ustaadhi wanaobandika matangazo yao kwenye mistimu na miti huwa wanawalenga zaidi akina na mama na akina mama/ wadada ndo wateja wao wakubwa.
Uchumba hauji automatically bana, kuna taratibu za kufuata. Au mi ndio sielewi haya mambo?Duuh mkuu huwa inaanza ugirlfriend na boyfriend, then nadhan baada ya muda automatically mnaenda uchumba...
Ila miaka tisa ya ugirlfriend?
Uchumba hauji automatically bana, kuna taratibu za kufuata. Au mi ndio sielewi haya mambo?
Halafu mnaweza kuwa kwenye mahusiano tangu wadogo. Wengine walianzia primary school kabisa huko. Hiyo miaka isikuogopeshe.
Ni 'baga' bana.
Umesema uchumba sugu umenikumbusha kanisani sa ivi wanaita uzinzi sugu, wanawaencourage wafunge ndoa.
Ngoja tupime uchumba wake na safari za vasco da gama kukaaa angani nafikiri vinashabihiana aiseeee
Ha haa vasco da gama nadhana yeye ana 10+1 maana juz juz tu alikuwa southafrica
Ha ha ha...kuna jamaa mmoja mdau wa Bagamoyo aliniambia kuna waganga wawili Bagamoyo wateja wao zaidi ya 90% ni wanawake. Na matatizo yao ni ishu za mahusiano!!!
Yaani tusipokuwa makini tutalishwa mpaka kinyesi