Mchumba wangu ana karama ya unabii, ananitisha!

Mchumba wangu ana karama ya unabii, ananitisha!

Hongera ila pole pia, maana waonaji wanakuwa na mambo ya Rohoni zaidi kuliko mwilini.

Jiandae maana suala la sex huwa hawana mpango sana.

Hivyo ujipange .

NB: Mimi pia nipo hivyo naona vitu vingi sana, ila sipo kama zamani.

Kifupi mume wangu hanielewi maana ndoa na tendo sioni thamani yake.
 
Wakuu habarini za wakati huu...

Niliwahi kuleta Uzi humu kuhusu mchumba wangu ambaye ni Mcha Mungu, bikira, mpole, mkarimu, mzuri n.k.

Nimegundua kwamba huyu mwanamke ana karama ya unabii pia (muonaji). Zamani manabii waliotwa waonaji.

Kwanini nimefikia hii conclusion? Mjomba wangu alikuwa anaumwa, yaani kaka yake mama yangu. Siku Moja kabla ya kifo cha mjomba wangu, mchumba wangu akanipigia simu kunimbia anaona huzuni KUBWA Kwa mama yangu, kesho yake mjomba akafariki, kweli mama aliumia sana!

Mimi ni Wakili, nilikuwa na kesi Tanga Jana, kabla sijaondoka akanipigia simu kuniambia anaona vita KUBWA kwenye hiyo kesi, na ananiona Niko hospitalini! Baada ya kesi, ule upande wa pili wakaniomba tuonane nje ya Mahakama nikiwa na mteja wangu ili tufute kesi tuyazungumze, kweli tukaenda kuonana nao, nikawekewa sumu kwenye kinywaji changu, nikapelekwa hospitalini kweli na nikalazwa, Sasa hivi ndio wameni-discharge.

Hayo ni machache tu kati ya mengi. Ama kweli, ukimtanguliza MUNGU mbele HUWEZI kuikataa taasisi ya NDOA. NDOA ni baraka.

Huyu nikimuoa inabidi niwe makini sana [emoji28]

Muwe na jioni njema.
Mshatoboa kimaisha. Anzisheni kanisa
 
Wakuu habarini za wakati huu...

Niliwahi kuleta Uzi humu kuhusu mchumba wangu ambaye ni Mcha Mungu, bikira, mpole, mkarimu, mzuri n.k.

Nimegundua kwamba huyu mwanamke ana karama ya unabii pia (muonaji). Zamani manabii waliotwa waonaji.

Kwanini nimefikia hii conclusion? Mjomba wangu alikuwa anaumwa, yaani kaka yake mama yangu. Siku Moja kabla ya kifo cha mjomba wangu, mchumba wangu akanipigia simu kunimbia anaona huzuni KUBWA Kwa mama yangu, kesho yake mjomba akafariki, kweli mama aliumia sana!

Mimi ni Wakili, nilikuwa na kesi Tanga Jana, kabla sijaondoka akanipigia simu kuniambia anaona vita KUBWA kwenye hiyo kesi, na ananiona Niko hospitalini! Baada ya kesi, ule upande wa pili wakaniomba tuonane nje ya Mahakama nikiwa na mteja wangu ili tufute kesi tuyazungumze, kweli tukaenda kuonana nao, nikawekewa sumu kwenye kinywaji changu, nikapelekwa hospitalini kweli na nikalazwa, Sasa hivi ndio wameni-discharge.

Hayo ni machache tu kati ya mengi. Ama kweli, ukimtanguliza MUNGU mbele HUWEZI kuikataa taasisi ya NDOA. NDOA ni baraka.

Huyu nikimuoa inabidi niwe makini sana [emoji28]

Muwe na jioni njema.
kuna mambo mawili, ni mchumba wako maana yake ni girlfriend huwa mnafanya uasherati pamoja au ni mchumba yule aliyeokoka ambaye mnasubiri hadi ndoa ndio mshirikiane tendo? kama hajaokoka na huwa mnafanay dhambi ya uasherati, pole sana, upo na muonaji ambaye ni sawa tu na mganga wa kienyeji, kwasababu Roho wa Mungu huwa hakai mahali pachafu penye uzinzi na uasherati. wapo waonaji wengi tu wenye mapepo ya kuona na kutabiri, wengine ni wajukuu wa waganga wa kienyeji hivyo wanarithishwa mikoba tangu utotoni, wengine mashetani ya ukoo yamewavamia, watu wa aina hiyo nawajua wengi sana na wanaweza kukuambia kitu ambacho ni cha kweli kitatokea. kwahiyo kama hamjaokoka, ni kwamba unashirikiana na mtu mwenye mapepo na yatakuingia na wewe kwasababu wewe na yeye ni mwili mmoja kutokana na mnavyoingiliana. ila kama ameokoka, na wewe umeokoka, mshikilie huyo awe mkeo. ni lulu hao.
 
Hongera ila pole pia, maana waonaji wanakuwa na mambo ya Rohoni zaidi kuliko mwilini.

Jiandae maana suala la sex huwa hawana mpango sana.

Hivyo ujipange .

NB: Mimi pia nipo hivyo naona vitu vingi sana, ila sipo kama zamani.

Kifupi mume wangu hanielewi maana ndoa na tendo sioni thamani yake.
Dona, unanitisha [emoji848]
 
kuna mambo mawili, ni mchumba wako maana yake ni girlfriend huwa mnafanya uasherati pamoja au ni mchumba yule aliyeokoka ambaye mnasubiri hadi ndoa ndio mshirikiane tendo? kama hajaokoka na huwa mnafanay dhambi ya uasherati, pole sana, upo na muonaji ambaye ni sawa tu na mganga wa kienyeji, kwasababu Roho wa Mungu huwa hakai mahali pachafu penye uzinzi na uasherati. wapo waonaji wengi tu wenye mapepo ya kuona na kutabiri, wengine ni wajukuu wa waganga wa kienyeji hivyo wanarithishwa mikoba tangu utotoni, wengine mashetani ya ukoo yamewavamia, watu wa aina hiyo nawajua wengi sana na wanaweza kukuambia kitu ambacho ni cha kweli kitatokea. kwahiyo kama hamjaokoka, ni kwamba unashirikiana na mtu mwenye mapepo na yatakuingia na wewe kwasababu wewe na yeye ni mwili mmoja kutokana na mnavyoingiliana. ila kama ameokoka, na wewe umeokoka, mshikilie huyo awe mkeo. ni lulu hao.
Mkuu amesema ni bikra
 
kuna mambo mawili, ni mchumba wako maana yake ni girlfriend huwa mnafanya uasherati pamoja au ni mchumba yule aliyeokoka ambaye mnasubiri hadi ndoa ndio mshirikiane tendo? kama hajaokoka na huwa mnafanay dhambi ya uasherati, pole sana, upo na muonaji ambaye ni sawa tu na mganga wa kienyeji, kwasababu Roho wa Mungu huwa hakai mahali pachafu penye uzinzi na uasherati. wapo waonaji wengi tu wenye mapepo ya kuona na kutabiri, wengine ni wajukuu wa waganga wa kienyeji hivyo wanarithishwa mikoba tangu utotoni, wengine mashetani ya ukoo yamewavamia, watu wa aina hiyo nawajua wengi sana na wanaweza kukuambia kitu ambacho ni cha kweli kitatokea. kwahiyo kama hamjaokoka, ni kwamba unashirikiana na mtu mwenye mapepo na yatakuingia na wewe kwasababu wewe na yeye ni mwili mmoja kutokana na mnavyoingiliana. ila kama ameokoka, na wewe umeokoka, mshikilie huyo awe mkeo. ni lulu hao.
Sijawahi kumuingilia na namuomba MUNGU kwamba nisimuingilie hadi ndoa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom