Mchumba 'angu amemegwa halafu ka confess


Mh. KKN, Ushauri huu ni ushauri ndio lakini kwa mwenzetu aliyeamua kusamehe utampotosha.Tukiwa na kawaida ya kulipiza kisasi kila tunapokosewa haitasaidia.Tujifunze kusamehe japo ni kugumu.Mwisho wa siku the reward is huge.

Ndugu uliyeumizwa... uelewe tu kwamba maisha si safari fupi na rahisi. Ni ndefu na ngumu.Si ajabu kwa kumsamehe utakuwa umemrekebisha once and for all.Jiulize wewe..mara ngapi unakosa? ingekuwa vipi kama usingesamehewa?
 

This is an interesting discussion.Inanifanya nianze kujiuliza maswali mengi. Ina maana wanaume wanapo cheat wake zao tena time and again.. hawajui inavyouma? Au inauma tu pale mwanaume akiwa cheated? Tena basi hapa ni girlfriend kacheat..je angekuwa mke ingekuwaje?
 
Ni heri kila mtu abaki peke yake na auamini moyo wake tuuu!!! Dunia hii ishafika mwisho, walichoweka mbele wapenzi ni uongo wingi. Na hakuna such a thing called true love, labda ule Mlav wa pale cross unaweza kuitwa hivyo.
 

hii yako sasa inabadilika, sidhani kama tunachokiangalia hapa ni maumivu kiasi gani jinsia moja inapata kutoka kwa jinsia nyingine katika mahusiano. Hapa nadhani tunaongelea ni jinsi gani tunaweza kumsaidia huyu jamaa ambae kasamehe ila bado moyoni anajihisi mdhaifu kwa yote yaliyopelekea mchumba wake kumegwa.

Kingine ni kwamba Revenge may be a short time solution lakini je katika future kila mmoja akiwa analipiza kisasi hiyo ndoa itasimama kweli?? Fikiria leo imetokea kwa mchumba na unataka ufanye revenge je ukioa na ikatokea wewe umemega nje na kufumaniwa hiyo revenge yake utaipokea??

Tuwe makini tusije tukapotezana hapa
 

Im not advocating for revenge Mkuu!(See my post number 81 above!)

My post here depicts my reflection on what most people have said regarding kumegwa kwa huyo mdada as if CHEATING BY A WOMAN NDO unforgiveable SIN ILA BY MEN IS A mischief which can be easily handled.I just wanted to get a feel of what the position should be for both men and women.
 
unashangaa nini, hiyo ni kawaida kwa walio wengi waume na wake kubanjua/kubanjuliwa nje, uzuri wengi huwa hawakamatani/hawafumaniani na usithubutu kufanya juhudi za kutaka kumfuma mwenzio, utakufa moyo. Hiyo chukulia ni kawaida kama kumwa malaria na endelea na safari yenu, hakuna garantii kama utakayempata mwingine atakuwa ni safi kabisa.
 
unashangaa nini, hiyo ni kawaida kwa walio wengi waume na wake kubanjua/kubanjuliwa nje, uzuri wengi huwa hawakamatani/hawafumaniani na usithubutu kufanya juhudi za kutaka kumfuma mwenzio, utakufa moyo. Hiyo chukulia ni kawaida kama kumwa malaria na endelea na safari yenu, hakuna garantii kama utakayempata mwingine atakuwa ni safi kabisa.
 
Ndugu yangu huyo hakufai kama ameweza kufanya mambo haya ktk uchumba atayafanya sana ktk maisha ya ndoa kwasababu ktk ndoa kuna kupanda na kushuka,
pia wewe mwenyewe utaishi kwa mashaka hebu fikiria siku umemkuta anasalimiana na mmoja wa hao jamaa mawazo yako yatakupeleka wapi? utakachowaza ni kuwa wanaendeleza
 
Huyo mwanamke ni malaya, na umalaya ni tabia, na tabia ni mazoea.
Ukioa huyo mwanamke basi uwe tayari kuibiwa kila wakati. Ana tabia na mazoea ya kugawa uroda, kumbuka kichaa hakiponi bali kinatulia kwa muda.
Achana naye mara moja, wadada wakumwaga wapo tele tena kwa mafungo huna haja ya kuumiza kichwa kwa hicho kicheche.
 
Piga konde moyo na umwambie ukweli mchumba wako kwamba wewe na yeye basi. Ameshakuonyesha yeye ni mtu wa tabia gani. Vitendo alivyovifanya anaweza kuvirudia tena baada ya kufunga ndoa naye. Najua utaumia sana kwa sababu unampenda, lakini ni wakati muafaka wa wewe kuanza kutafuta mchumba mwingine.
 
Chichi mdogo wangu, pole kwa yaliyokusibu. Huyo unayemwita ni mchumba wako hakufai. Kama ameonjwa na watu zaidi ya wawili inawezekana hao ndio uluowagundua si ajabu wakawepo wengine. Kuna msemo usemayo "Mavi ya Kale Hayanuki". Hata kama mtaoana siku wakikutana wataambiana tukumbushane. I advice you this, find another fiancee.
 
PUNDIT,
You are right my friend!!!these days evryone is a player...both men and women...In this game there is only one rule DO NOT GET CAUGHT!!! Very sad...No trust! even between husband and wife. Human beings have lost their ability to be honourable and have some integrity.

Woi what is the world coming to?? Sometimes it is better to be without a Mchumba.
 
Mdogo wangu Chichi, kama ulivyopewa ushauri na wana JF walionitangulia, nazidi kukusitizia kuwa huyo mchumba achana naye kwani si vizuri kuingia kwenye ndoa huku imani yako kwa mwenza wa maisha ina baka la kukosa uaminifu. Kama katika hatua ya uchumba tyu umekuwa na uhakika wa watu wawili wanaofisadi penzi lenu, nahisi wakati mmeshaoana na ndoa itakapofikia plateau ataweza rudia tabia ya ugawaji wa penzi nas hii si picha nzuri. Licha ya matazamio hayo, kuishi na mtu ambaye una ushahidi wa usaliti kutayumbisha ndoa yenu kwani kila kukitokea kitu (mfano kukawia kurudi, kuongea na simu kwa sauti ya chini, message kwa wingi etc) utahisi ameranza tena. Hitimisho: acha na huyuo mchumba tafuta mwingine na ukimpata nendeni ANGAZA/VCT mukajihakikishe afya zenu, fungeni ndoa kwa misingi ya dini yenu na muishi kwa furaha muzae matunda mema.
 
Mi nafikiri kwa kuwa ameconfess basi huyo ni mwaminifu msamehe labda alipitiwa tu....LAKINI NA WAWILI!!! ....Mhmhh
 

Huyu anakufundisha kulipiza visasi,hakuna kitu kibaya kama hiki nakwambia.

hapa kila mtu atakupa ushauri wake lakini at the end of the day ni wewe wakufanya maamuzi,by the way ulishafanya maamuzi ya kumsamehe sasa sijui nini tena? labda ulikuwa unataka kujipima kama maamuzi uliyofanya ni sahihi ama laa.

Pole sana kwa yaliyokukuta hata hivyo.
 
Inaonekana mapema kuwa huyo mchumba wako ana safu mbovu ya ulinzi kumegwa na watu wawili? Lazima atakusumbua sana
 
well: kama lait ningekuwa katika nafasi uliyokuwa nao wewe basi ningewachana na huyo bint lakini huo ni uwamuzi wako kwani siku zote mdanganyaji anabakia kuwa danganyaji na hata kama utafunga hiyo ndowa kuna wale ambao kwa njiamoja au nyingine watakuwa na uwezo mkubwa wa kupalilia hiyo bustani ya mke wako zaidi ukumbuke kina binadamu tuna kitu kinaitwa (FANTASY)inawezekana unampenda na yeye anasema ankupenda lakini amekuwa na FANTASY ya mtu fulani au hata katika mapichi ya chumbani yanamridhisha zaid kwahuyo mwingine zaidi kuliko wewe sasa jee utakuwa tayari kukabiliana na hali hiyo ipo siku atakuja kuliza kilio cha mbwa mdomo juu na hapo utakuja wachukia wasichana wote
 
Inawezekana uamuzi wa kumsamehe huyo mchumba wako ulitokana na sababu zifuatazo (na labda si matakwa ya nafsi yako):
  1. Ulishakaa nae kwa muda mrefu (miaka 2) - hivyo unakua kama umewekeza kitu fulani kwake.
  2. Ulishamtambulisha kwa wazazi na ndugu - hivyo ni vigumu kuwaeleza kwamba uhusiano umevunjika.
  3. Ulishapanga kuingia kwenye ndoa muda si mrefu ujao - hivyo ni vigumu kuanza upya, yaani umebanwa na muda.
Nakushauri unapafanya uamuzi piga moyo konde ili uweze kukabiliana na matatizo yatakayosababishwa na uamuzi wako. Itakuumiza ila itajenga kwa muda mrefu zaidi, achana na huyo binti .... anza upya, usiogope kuchelewa (ukapata faraja ya nafsi kwa siku zijazo), usiogope kuwaeleza ndugu kwamba its not working with her.
MWISHO: MWAMUZI WA JAMBO HILI NI WEWE MWENYEWE!
 

Data: 50% ya wake za watu wanamegwa nje ndo maana 50% ya wana ndoa ni HIV ++ve
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…