Ulivyoanza kueleza, na kutambua sisi wanaume tulivyo (kuwahurumia wanawake), nilianza kufikiria namna gani utafanya ili utengane naye bila ya kumwumiza zaidi. Lakini baadaye umetamka kuwa ulikuja kugundua kuwa alikuwa na wanaume wengine, hii inamaanisha hana shida ya mtu wa kumliwaza kama ilivyokuwa hapo mwanzo.
Maadam umekwishamsaidia kwenye mahafali yake, ni dhahiri anajua kuwa huna chuki naye.
Je wewe ni muumini wa dini yoyote?
Kaa naye na umweleze kwa upole but with firm statement and decision kuwa haitawezekana kuendelea na mahusiano hayo milele. Sasa ni wakati wa yeye pia kuanza mahusiano yenye kutengeneza familia yake, kwa kuendelea kuwa nawe milango hiyo yote inakuwa imefungwa.
Lakini muhimu zaidi ni kuwa ungependa uwe mwaminiu kwa familia yako ambayo ni haki yao.