Mchepuko oyeee!

Mchepuko oyeee!

Siku huyo mchepuko akifumaniwa na mmeo na akatolewa linda utaona kama ataweza kukukuna tena
 
Anachokiongea dagaa ni matokeo tuu ya mahusiano machungu kati ya wanandoa. Sijui dagaa alikutana na changamoto gani iliyompelekea kufikia maamuzi hayo....

Siku zote wewe Mwanamke mwenye ndoa omba sana akupe uwezo na ujasiri wa katatua matatizo ya ndoa yako lakini isiwe kwa kutafuta mchepuko

Ndoa ikishindikana kabisa heri kukaa pembeni kuliko hii hekaheka ya kuwa na waume wawili
 
Habari wanajamvi,

Wacha niende moja kwa moja kwenye hoja. Mimi ni mke wa mtu nina miaka kadhaa kwenye ndoa zaidi ya kumi, namuheshimu mume wangu na nampenda sana pamoja na watoto wetu, naye analitambua.

Huu ni mwaka wa sita sasa niko na mchepuko wangu na mchepuko wangu naye ni mume wa mtu, na sitegemei kumwacha. Na naweza sema jamani michepuko inaimarisha kutunza ndoa ukiwa na mchepuko wako ukakupenda na mkaheshimiana na mkawekeana misingi yenu, wacha niendelee kusema michepuko hoyee.

Sitaki ushauri wenu wa hoo sijui maradhi yapo, jibu ni kwamba tuko makini na mchepuko wangu kuliko mjuavyo, na ananikuna haswaa na ananijali sana.

Ila swali moja la kizushi, kwanini wanaume mlioko kwenye ndoa mkiwa kwenye sita kwa sita amuwapi mashamsham wake zenu ila mkitoka nje mnaonyesha ufundi ambao hamuwapi wake zenu? Hata mimi nina imani huyu mume wa mtu niliye nae ananipa mashamsham kama yote ila najua kwa mkewe atakuwa anampapasa.

Kwakweli mimi sijutii, na kama dhambi nimeshatubu sababu hata Mungu naye ni shahidi anaona ninachopata.

Wale wote wenye bibi wa kando na babu wa kando tuseme hoyeeeee.

Kwa kumalizia nasema hivi: Mchepuko wangu nampenda sana na na mume wangu nampenda na ndoa yangu siachi na yule naye namshauri sana asimwache mkewe, sisi tupo kwa ajili ya kurutubisha ndoa zetu na kujenga.

Karibuni.
Unaongeza viungo si ndio eeeenh
 
Back
Top Bottom