Acha usanii wa CCM mkuu. Nilikaa MT kwa muda wa miezi mitatu na kushuhudia samaki nchanga walivyo na wanavyoliwa. Kwa bahati mbaya kwa pale mjini hakuna kitu kama hiki ila vijijini na si kila sehemu, kuna sehemu zake. Kikubwa zaidi, samaki nchanga anakuwa kababuliwa huyu wako hajababuliwa yaani kama vile umemuokota chumbani kwako baada ya kula sumu na kumuweka kwenye sahani ili udanganye watu. Mwisho huyu samaki wako ni samaki buku ama samaki wale wa ndani, kule MT wanakula samaki nchanga wa porini ambao ni wadogo kimaumbile si kama huyu wa bongo movie a.k.a. ki-CCM (kisanii), na kama kweli ungemla huyu leo hii wala usingepata muda wa kuja hapa kutuambia hivyo kwani ungekuwa aidha Muhimbili au ulishakufa tayari baada ya kula sumu uliyompa huyu msanii mwenzako.