Mchaga huyu nimetahadharishwa

Mchaga huyu nimetahadharishwa

The navi 2

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2013
Posts
352
Reaction score
46
Kuna binti mmoja wa kichagga ananipenda sana hata wakati mwingine amekuwa akifanya mambo ya aibu ili anifurahishe.

Amekuwa akiniomba sana tufanye kazi pamoja na hata kushinda pamoja sehemu yoyote.

Lakini shida inaanza pale ambapo rafiki zangu wamekuwa wakiniambia nisimkubalie kabisa kuwa nae karibu wala kumuoa.

Kwani naweza pata shida hapo baadae..

Yaani nitawasahau ndugu zangu kabisa nimejitahidi kujitenga nae lakini amekuwa akinitafuta mara kwa mara akinijulia hali.

Hata ndugu zangu wamenikataza kumuoa huyu mtoto wa kichagga (rombo).

Kumtema moyo unauma sana maana kanifia kabisa
 
kuwa na msimamo kama mnapendana ndugu hawawezi kuzuia upendo wenu
 
Kua na msimamo wewe!kwa hyo huyo mke ni wako au wa rafiki zako/ndugu zako?
Stuff mwenzetu siku moja alituhadithia jinsi alivyokuwa na wakati mgumu ilipojulikana anataka kuoa mchaga...
Anasema alipata mashinikizo ya kila aina kutoka kwa ndugu na jamaa ya kuachana na huyo mwanamke kisa ni mchaga lakini anasema aliziba masikio walipoona ameamua kuoa kwelibwakamwambia ahakikishe mwanamke hajui mambo yake hata salary slip yake asiijue ....jamaa anasema alioa na wakaishi vizuri na mkewe na akawa ni mchakarikaji wa kutafuta pesa mambo yakakaa kwenye mstari na sasa mke wake amekuwa kipenzi kwa ndugu zake kwa jinsi anavyojitolea kuwasaidia
 
Ukishawakubalia hao ndugu zako na jamaa zako.. Watakuambia upambane umnyang'anye Diamond Wema Sepetu.UMUOE... na ukishindwa hapo, wanavunja urafiki na undugu wenu.

kazi kwako

hapana si hivo mkuu... Wanataka nioe karibu na home eti ndo wanatabia njema
 
Kua na msimamo wewe!kwa hyo huyo mke ni wako au wa rafiki zako/ndugu zako?
Stuff mwenzetu siku moja alituhadithia jinsi alivyokuwa na wakati mgumu ilipojulikana anataka kuoa mchaga...
Anasema alipata mashinikizo ya kila aina kutoka kwa ndugu na jamaa ya kuachana na huyo mwanamke kisa ni mchaga lakini anasema aliziba masikio walipoona ameamua kuoa kwelibwakamwambia ahakikishe mwanamke hajui mambo yake hata salary slip yake asiijue ....jamaa anasema alioa na wakaishi vizuri na mkewe na akawa ni mchakarikaji wa kutafuta pesa mambo yakakaa kwenye mstari na sasa mke wake amekuwa kipenzi kwa ndugu zake kwa jinsi anavyojitolea kuwasaidia

asante sana mkuu kwa ushauri wako nipo naufikilia... Maana ni hatari sana naona inaweza tokea
 
umemuongelea tu yeye kuwa anakupenda anakupa 0713, lakini haujasema wewe kama unampenda au unamtamani tu! chukua kitu cha kichaga hicho babu, rombooooo...daadek!
 
hahahahahaha. unataka umuowe kweli? umejandaa kuowa? unayo mahari ya kulipa? umemaliza shule?

1. Sina uhakika
2.hapana nataka awe mchumba kwanza
3.mahali ipo
4.nipo chuo mwaka wa pili
 
umemuongelea tu yeye kuwa anakupenda anakupa 0713, lakini haujasema wewe kama unampenda au unamtamani tu! chukua kitu cha kichaga hicho babu, rombooooo...daadek!

nampenda sana lakini wengi wananipa wasiwasi kuhusu huyu
 
Back
Top Bottom