mafutamingi
JF-Expert Member
- Feb 14, 2011
- 2,772
- 2,171
Napendekeza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimtunuku Mbwana Samatta shahada ya udaktari ya heshima (Honoris Causa) kutokana na mchango wake
mkubwa katika tasnia ya mchezo wa soka. Mchango wake unatokana na mambo yafuatayo:-
1. Amekuwa mtanzania wa kwanza kucheza kwenye ligi ya daraja la kwanza ya Uingereza (EPL), ligi ambayo inashika namba moja kwa
umashuhuri ulimwenguni
2. Amekuwa Mtanzania wa kwanza kucheza katika ligi ya mabingwa ya klabu za Ulaya na kufanikiwa kufunga goli dhidi ya klabu ya Liverpool,
moja ya timu bora sana nchini Uingereza
3. Amekuwa Mtanzania wa kwanza kucheza kwenye uwanja wa Wembley, uwanja mashuhuri sana wa mpira wa miguu jijini London
Nimependekeza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuwa mpaka sasa ni chuo pekee nchini kinachotoa shahada katika tasnia ya michezo.
Haitakuwa ajabu kwa Mbwana Samatta kutunukiwa heshima hii. Hivi sasa Chuo Kikuu cha Manchester kimeamua kumtunuku mchezaji kijana wa Manchester United
Marcus Rashford degree ya udaktari kutokana na mchango wake katika soka na pia kusaidia watoto maskini.
Nawasilisha
mkubwa katika tasnia ya mchezo wa soka. Mchango wake unatokana na mambo yafuatayo:-
1. Amekuwa mtanzania wa kwanza kucheza kwenye ligi ya daraja la kwanza ya Uingereza (EPL), ligi ambayo inashika namba moja kwa
umashuhuri ulimwenguni
2. Amekuwa Mtanzania wa kwanza kucheza katika ligi ya mabingwa ya klabu za Ulaya na kufanikiwa kufunga goli dhidi ya klabu ya Liverpool,
moja ya timu bora sana nchini Uingereza
3. Amekuwa Mtanzania wa kwanza kucheza kwenye uwanja wa Wembley, uwanja mashuhuri sana wa mpira wa miguu jijini London
Nimependekeza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuwa mpaka sasa ni chuo pekee nchini kinachotoa shahada katika tasnia ya michezo.
Haitakuwa ajabu kwa Mbwana Samatta kutunukiwa heshima hii. Hivi sasa Chuo Kikuu cha Manchester kimeamua kumtunuku mchezaji kijana wa Manchester United
Marcus Rashford degree ya udaktari kutokana na mchango wake katika soka na pia kusaidia watoto maskini.
Nawasilisha