Mbwa Mwitu na Mwana Kondoo

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,238
12,753
SIKU moja mbwa wa mwitu alikuja anywe katika kijito cha maji, akamkuta mwana kondoo mchanga akasimama karibu na kijito. Mbwa wa mwitu akataka kugombana naye apate kumua. Akamwambia, “Mbona unaborugaboruga matope nisipate maji safi?” Kondoo mchanga akamwambia. “Gissi gani nikutilie taka majini, yakiwa yanashuka kwako kunifikia mimi?” Mbwa wa mwitu akamwambia, “Uthubutuje kunywa wewe, kabla sijanywa mimi?” Akamwambia mwana kondoo. “Mimi sinywi maji, maziwa ya mamangu yanitosha.” “Bassi,” akamwambia mbwa wa mwitu, “mbaya wee, mwaka jana umenitukana.” Eeh Bwana” akamwambia mwana kondoo, “Mwaka jana nalikuwa sijazaliwa.”

Mbwa wa mwitu akakasirika sana akamwambia, “Kama si wewe, ndiye baba yako, sijui kuwapambanua, mmestahili kufa wote.” Akamkakata, akamue, akamla.
 
SIKU moja mbwa wa mwitu alikuja anywe katika kijito cha maji, akamkuta mwana kondoo mchanga akasimama karibu na kijito. Mbwa wa mwitu akataka kugombana naye apate kumua. Akamwambia, “Mbona unaborugaboruga matope nisipate maji safi?” Kondoo mchanga akamwambia. “Gissi gani nikutilie taka majini, yakiwa yanashuka kwako kunifikia mimi?” Mbwa wa mwitu akamwambia, “Uthubutuje kunywa wewe, kabla sijanywa mimi?” Akamwambia mwana kondoo. “Mimi sinywi maji, maziwa ya mamangu yanitosha.” “Bassi,” akamwambia mbwa wa mwitu, “mbaya wee, mwaka jana umenitukana.” Eeh Bwana” akamwambia mwana kondoo, “Mwaka jana nalikuwa sijazaliwa.”

Mbwa wa mwitu akakasirika sana akamwambia, “Kama si wewe, ndiye baba yako, sijui kuwapambanua, mmestahili kufa wote.” Akamkakata, akamue, akamla.
we jamaa umelewa
 

IMBU NA NG’OMBE​

HAPO kale imbu alikaa kitako katika pembe lake ng’ombe, akamwambia, nimekaa kitako pembeni mwako ukiniona mzito mno uniambie niende zangu.” Ng’ombe akamwambia, “Singalijua uliko, usiponiambia.” Akapunga kitwa akamdaka imbu kwa ulimi.
 
Yaani mleta maada ni darasa la saba (in Mwakyembe Voice)

PAKA ASIYE NA MKIA​

PAKA aliyekwenda akamate kuku akanaswa na mtego, akapata kuokoka, ila mkia wake akakatika na mtego. Alipofika kwake akaona killa paka akimtazama hucheka kwa sababu hana mkia. Bassi walipokusanyika paka wote wafanye shauri, yule akasimama akawaambia, “Nina neno moja, mikia yetu inatutaabisha sana, tukitaka kujificha tunduni mkia hutoka, tukienda hatuna buddi kuurudisha nyuma au kuuvuta juu, hatuwezi kuuficha, hatta tukiona panya, tunaupigapiga mkia, naye hutusikia hukimbia, marra kwa marra, tumenaswa kwa mkia mtegoni. Mimi naona afadhali tujikate wote mkia tusitaabike tena nao.” Paka mzee akamwambia, “Tangu lini umeona mkia ndiyo taabu? Nathani tangu ulipokupotea tu.”
 
Back
Top Bottom