Mbunge wangu Mwigulu Nchemba njoo jimboni - spesho kwa wanairamba Magharibi

patriq

Senior Member
Apr 17, 2012
145
53
Wapendwa wanairamba, kuna hii ishu ya mheshimiwa wetu, mashuhuri kama campaign manager wa ccm, kaingia mitini akifanya kazi ya kutafutia wengine ubunge wakati hali ya iramba magharibi inazidi kuwa mbaya kimaendeleo. Naleta hoja kwenu kwamba tumuulize mheshimiwa ahadi alizotuahidi wakati wa kampeni zake atazitimiza lini? Au anasubiri 2015 aje tena kudai kwamba hakutimiza ahadi zote hivyo tumpe miaka mingine mitano ili atimize?

Nashauri tumwajibishe ili tabia hii ya umeneja aachane nayo, tusipoangalia atakapokuja tukamwongezea miaka mitano tena, ataingia mitini na atakaporudi atakuwa si meneja tena bali campaign director. Mheshimiwe jitokeze jf utueleze mikakati yako ukifahamu kwamba jimbo tulikuazima kwa imani kwamba utashirikiana nasi kuleta maendeleo lakini tangu tukuazime hatujawahi hata kukuona ukitueleza mikakati ya maendeleo zaidi ya kushuhudia matusi igunga na alumeru mashariki, ukitoa hoja zilizo sinyaa kwa kukosa nguvu, come up mheshimiwz na useme kitu.

Vinginevyo 2015 utaungana na mwenzio aliyekuachia kijiti kwani hatuna utani tena katika maendeleo. Haiwezekani wewe uwe campaign manager wa ulaji wa wenzio wakati unatakiwa uwe campaign manager wa maendeleo yetu. Njoo tazama shule zetu za sekondari zinavyofelisha watoto kila mwaka, vitabu, uwajibikaji "tile ka kintu uwe wi kalansile du mu ukampeni meneja" we hope you will see this and give us your stand before we start seeking for alternatives. C4m daima.
 
Usilalamike ndugu mlichezea bahati wakati wa kupiga kura mkachakugua rangi ya bendera badala ya mtu atakaye waonyesha njia kuelekea maendeleo. nawaasa msifanya makosa come 2015
 
Kofia,chumvi,fulana,mataputapu na vitenge mlivyohongwa vitawagharimu hadi 2015,mh yupo bize kurejesha mihela yake aliyowahonga,na kwa hali ilivyo kuna uwezekano mkubwa asirudishe zote hadi 2015,vumilieni tu maumivu hayo hadi2015,yakizidi muoneni daktari(Nguvu ya umma) kwa matibabu zaidi,teh!
 
kofia,chumvi,fulana,mataputapu na vitenge mlivyohongwa vitawagharimu hadi 2015,mh yupo bize kurejesha mihela yake aliyowahonga,na kwa hali ilivyo kuna uwezekano mkubwa asirudishe zote hadi 2015,vumilieni tu maumivu hayo hadi2015,yakizidi muoneni daktari(nguvu ya umma) kwa matibabu zaidi,teh!

nawapata wakuu, kiukweli labda wapo walioambulia lakini sisi hatukulamba hata kidogo kwa sababu damu yetu haina harufu ya dhambi ya rushwa. Tulimwamini aliposimama na kuongea kwani hatukuwa tunamfahamu vema, ila tunaapa sasa atavuna alichoweka, kaka jitokeze utoe mstakabali wa jimbo.
 
Heshima mbele mkuu Patrique, mimi nilishatubu kutumiwa kama ATM ya mwigulu kumwaga pesa kipindi cha Mwigulu, leo hii nipo huru na makamanda.

Huyu jamaa ni empty kabisa, anatanguliza sana pesa kwa wapiga kura, ukifanya nae appointment anakimbilia kukupa nauli kubwa, hii ni kuwafundisha u-ombaomba Wanyiramba, sisi tunajipanga kuanzisha M4C specific kwakukomboa Wanyiramba wenzangu, tuwatie moyo wa subira mpaka 2015
 
Mkuu hapo hakuna kumsubiri huyo, M4C inashika kasi,

Endeleza libeneke huko..

Kazi ni kwako mkuu!
 
Mkuu, kwani mwigulu alipambana na nani wakati wa uchaguzi 2010, au utuweke wazi kuwa wewe ni gamba original. tuambie jumla ya wagombea na vyama walivyotokea, ikiwezekana tuambie mwigulu alishinda kwa kura ngapi, na alifuatiwa na nani.
 
mwigulu yupo dar anakula bata pale lumumba upepo coco beach,nyie kuleni mapama na matogo.ccm wameshindwa 51yrs ije leo
 
Nina uhakika wananchi wa Iramba Magharibi wamejutia kosa lao..na wameanza kuunga mkono mabadiliko.
Mwaka 2015 msifanye kosa...ubashiri wangu unaonyesha Dkt.Kitila Mkumbo atakuja kuomba ridhaa kwenu ya kuwaongoza.
Ikitokea hivyo kweli msimwangushe.
 
Mtoa hoja wewe ndio haupo Iramba, Mwigulu tar 23 alikuwa Ng'anguli, Maluga na Kitusha, Tar 24 alikuwa Uwaza na Galangala, tar 25 alikuwa kisharita na kijiji kimoja kati pale, na sisi vijana wa standi na kwenye pikipiki alituwezesha vitendea kazi, sokoni amefuta ushuru wa bidhaa ndogondogo. Mnyonge mnyongen ila haki yake mpeni, Mwigulu ni ZAIDI YA MBUNGE ANAFAA HATA UONGOZ MKUBWA ZAIDi. Anayebisha na anayejidanganya kupitia humu atapata majibu tokea kwa wanyiramba wenyewe. Kwa hili mwigulu wala usijibizane na wenye wivu
 
Yupo Busy na Shughuli za Chaguzi ndogo na Shughuli za Chama na jamii ya Dsm Kwa kifupi imekula kwenu fanyeni utaratibu mwingine yupo busy atakuja kuwaona 2015.
DSC_6688.jpg
 
Kwanza sijilaumu kuwa na mbunge weak kama huyo kwa sababu ckumpgia kura na kura yangu ilienda CDM japo hazikutosha,,siongei unafiki nilijitahidi pamoja na jamaa zangu wachache kuelimisha watu kuipgia kura CDM 2010 ila tatizo wanyiramba wenzangu wengi hawakuwa wameelimika vzr mwaka huo,naamini ths tym watakuwa wameelimika,..binafsi sioni haja ya mwigulu kuja eti tumsikilize ama cvyo eti 2015 hatutamchagua...suala hapa ama aje ama asije hana ubunge 2015...nawasilisha.
 
Poleni wanairamba Magharibi lakini, kama alivyowahi kusema Jenerali Ulimwengu, yabidi mjue kwamba mchagua hovyo hastahili huruma yoyote anapoanza kulalamika hovyo. Mlifanya uamuzi wa kipuuzi kwa kuchagua hovyo na sasa mnaonja machungu yake na kuanza kulalamika hovyo... upuuzi ni ghali na gharama yake hivi sasa hailipwi na wapuuzi peke yao bali Wanairamba wote. Amkeni tafadhali!
 
Mtoa hoja wewe ndio haupo Iramba, Mwigulu tar 23 alikuwa Ng'anguli, Maluga na Kitusha, Tar 24 alikuwa Uwaza na Galangala, tar 25 alikuwa kisharita na kijiji kimoja kati pale, na sisi vijana wa standi na kwenye pikipiki alituwezesha vitendea kazi, sokoni amefuta ushuru wa bidhaa ndogondogo. Mnyonge mnyongen ila haki yake mpeni, Mwigulu ni ZAIDI YA MBUNGE ANAFAA HATA UONGOZ MKUBWA ZAIDi. Anayebisha na anayejidanganya kupitia humu atapata majibu tokea kwa wanyiramba wenyewe. Kwa hili mwigulu wala usijibizane na wenye wivu

hata ulie lie jua kwamba M4C ni kama tsunami na itafika huko iramba na hakuna gamba hata mmoja atakayesalimika.
Mlamkiego mbwaneee.............!
 
Mbona niko Iramba mpaka sasa au siku hizi Iramba iko humu jamvin. Ndg yangu ungenialika jamvini maana jimbon nilishakuja mara tu baada ya bunge. Pia kwa kuwa ni maalumu kwa wanairamba narudia tena sio muda mwafaka kwa mtu yeyote anayeipenda iramba kujadili uchaguzi wa2015 muda huu. Kwa sasa tujadili mi utekelezaji na mipango ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali. Kuhuusu 2015 wanairamba watatoa majibu. Mimi sina hofu nasema tena kama CCM ITAPATA JIMBO MOJA TU 2015 BASI ITAKUWA IRAMBA.AJE YEYOTE CDM MNAYEMWAMINI ILI KUSIWEPO KISINGIZIO. NITAFANYA KAMPENI SIKU TATU TU.
 
Back
Top Bottom