Kamanda
Lukolo mimi nipo Mongolandege.
Mstahiki meya wa manispaa ya Ilala
Jerry Silaa kama kuna mambo umejaribu kumtumia yakafanikiwa basi una bahati nzuri.
Mimi niliwahi kumfuatilia sana kuhusu ufunguzi wa zahanati ya Mongolandege, ambayo ujenzi wake ulikamilika mwishoni mwa mwaka 2010 kabla ya uchaguzi mkuu lakini haukuwahi kutoa huduma kwa takribani mwaka mzima hadi pale wananchi walipopiga kelele sana.
Baada ya kubana nae, nakumbuka alinijibu siku moja kuwa kuendesha manispaa kubwa kama ilala ni sawa na kuendesha meli, kwakweli nilicheka tu kimya kimya. Nikajiuliza kama Jery alikuwa anatambua ukubwa na uzito wa kazi ya umeya aliyokuwa anaililia.
Anyway, hata hivyo zahanati imefunguliwa mwaka jana, ingawa haina vifaa tiba, wameleta wauguzi na manesi kama watatu au wanne ambao wanatibu kwa "kupiga ramli" kwakuwa hakuna kifaa chochote cha kufanyia kipimo, hata kipimo cha maleria hakuna. Na kichekesho zaidi ni kwamba zahanati hiyo inafunguliwa Jumatatu hadi Jumamosi, na siku za Jumapili inafungwa!!! Sasa jiulize kama jumapili watu hawaumwi ama hawahitaji matibabu???... eti meya aliyeshindwa kazi naye anafanya kampeni za kutaka kuwa mbunge.
Btw, tutafutane weekend moja tuone ni namna gani tunaweza kuunganisha nguvu na viongozi wa Chadema jimbo la Ukonga ili tuhakikishe kuwa 2015 hatupotezi jimbo kwa kuliacha kwa wauza sura wa magamba, ambao wamethibitika pasipo shaka kuwa hawawezi kutukwamua kamwe.