Mbunge wa Ngara (CCM), Ndaisaba Ruhoro anadaiwa kulazimisha picha zake zibandikwe maeneo yenye mkusanyiko wa watu

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,024
1,618
1686039235956.png

Picha hizo zinaelezwa kubandikwa maeneo ambako kuna picha za Rais na sehemu ambazo hakuna picha za kiongozi mkuu wa nchi kwa madai yeye ndiye kiongozi wa Ngara.

Mbunge huyo amekiri kuwepo na picha zake nyingi maeneo tofauti zikiwemo nyumba za watu na kutaja sababu kuwa inatokana na mapenzi waliyonayo wananchi kwake, hivyo haoni kosa kwa watu kufanya hivyo.

Ruhoro analalamikiwa kulazimisha wenye maduka, migahawa, saluni na taasisi nyingine kuwa na picha zake ilihali maeneo mengi yamebandikwa picha za Rais na viongozi wa juu.

Katika maeneo mengi ya Ngara ambayo gazeti hili lilipita, picha za mbunge huyo zinaonekana kupamba maduka na maeneo yenye mikusanyiko kwa kuwekwa kwenye vioo kama ilivyo kwa picha za Rais na kutundikwa kwenye kuta kama ishara ya kiongozi wa eneo husika.

Mmoja wa wafanyabiashara wa maduka mjini Ngara alikiri kwenye maduka yake mawili ameweka picha za mbunge huyo, lakini akaeleza kuwa si kwa utashi wake, bali anasukumwa na biashara yake.

“Sijazungumza na Ruhoro mwenyewe kuhusu hili, lakini wapambe wake wanaleta picha kwamba lazima ubandike kwenye eneo la wazi na bila kufanya hivyo usije kulaumu. Ndugu yangu utafanyaje kama ni wewe maana hawa ndiyo waamuzi wa kila kitu. Wananchi tunataka maendeleo sio kulazimishwa kubandika picha za wanasiasa kwenye biashara zetu,” alisema mfanyabiashara huyo ambaye hakutaka kutajwa jina gazetini.

Kwa mujibu wa mfanyabiashara huyo, picha za mbunge zinatengenezewa Ngara hakuna malipo kwa mmiliki wa ofisi zinapobandikwa, jambo ambalo linawakwaza zaidi.

Baadhi ya wananchi walisema kwa sasa picha hizo zinasambazwa vijijini hasa maeneo yaliyochangamka na mtindo ni ule ule wa wahusika kulazimisha picha ya mbunge huyo kuwekwa eneo la wazi.

Akitoa ufafanuzi wa picha hizo kusambazwa jimboni, Ruhoro alisema hakuna shida wala kosa, kwani wanaozisambaza ni wananchi wenyewe kwa mapenzi yao.

Chanzo: Mwananchi
 
Hayo ni maelekezo ya mganga wa kienyeji wa mheshimiwa mbunge ili kipindi kijacho achaguliwe tena
 
Back
Top Bottom