Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,902
- 945
MBUNGE NDAISABA RUHORO AILILIA SERIKALI BEI YA MAHINDI
Mbunge wa Jimbo la Ngara Mkoani Kagera, Mhe. Ndaisaba George Ruhoro ameiomba serikali kupitia wizara ya kilimo kunusuru zao la Mahindi ambalo bei yake inashuka siku hadi siku.
Mhe. Ndaisaba ametoa kauli hiyo baada ya wananchi kuibua kero hiyo kwenye mkutano wa hadhara alioufanya Kata ya Ngara mjini ambapo wameeleza kuwa wanatumia gharama kubwa kulima lakini bei ya mahidi kwa kilo ni shilingi 250 hadi 180 kwasasa.
Wananchi wamesema kuwa wamekuwa wakinunua mbegu kilo 2 kwa shilingi elfu 2 na gharama nyingine za uendeshaji huku wakiishia kupunjwa Bei ya sokoni.
Kufuatia kilio hicho Ndaisaba amemuomba Waziri wa kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuwatuma NFRA Wakala wa Taifa wa hifadhi ya chakula kufika wilayani Ngara ili kuweza kununua Mahindi hayo.
Kero nyingine iliyoibuliwa ni kuhusu umeme ambapo wnanachi wameomba kupewa huduma hiyo kwa Bei nafuu kutokana na maisha yao kuwa ya chini.