Mbunge wa Momba, David Silinde rasmi ahamia CCM

Mbunge wa Momba, David Silinde rasmi ahamia CCM

idawa

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2012
Posts
25,298
Reaction score
38,438
2389921_SILINDE_JUNI_0.jpg

Mh.Silinde leo ameomba rasmi kujiunga na Chama Mapinduzi, na amesema yupo tayari kukitumikia Chama Cha Mapinduzi kwa nguvu zote.

Spika Ndugai amemkaribisha na kumhamisha kwenye viti vya Upinzani kumpeleka kwenye viti vinavyokaliwa na wabunge wa CCM.

Hivyo kuanzia leo rasmi Silinde ni mbunge wa CCM na atakaa upande wa wabunge wa CCM. Davidi amekuwa mbunge kwa tiketi ya CHADEMA tangu mwaka 2010

Mbunge huyo alijiuzulu nafasi zote za uongozi ndani ya CHADEMA mwezi Mei, baada ya wabunge wenzake kumtaka kufanya hivyo kwa kutotii agizo la kutokwenda bungeni

Wakati anajiuzulu alisema wananchi ndio walimtuma bungeni, hivyo hata akikosa udhamini wa CHADEMA, atatumia chama kingine

Live kutoka bungeni.

Pia soma
Silinde: Maamuzi ya kutufukuza ni ya kitoto. Kuna udikteta CHADEMA, Mbowe ajitafakari na kuachia Uenyekiti

Mbunge wa Momba, David Silinde awatolea uvivu CHADEMA, asema yeye hapelekeshwi na Mbowe bali wapiga kura wa Momba

Spika Ndugai: Hakuna Mbunge aliyefukuzwa Ubunge. Vikao vya majungu havifanyi kazi hapa, Msajili tazama vyama vya namna hii
 
Kwanini Police washiwashike hao walinzi?
 
Ni swala la muda tu (kwa hizi hama hama) itatokea bonge la disapontment kwa mashabiki wa siasa..hasa siasa za upinzani.
 
Back
Top Bottom