Landala
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 997
- 473
Mbunge wa zamani wa jimbo la Musoma mjini kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Vedasto Mathayo ameomba arudishiwe madawati yake yenye thamani ya shilingi milion 18 aliyoyatoa kwa shule mbali mbali wakati akiwa mbunge.
Mwandishi wa Tanzania Daima alipongea naye kwa njia ya simu alilithipitisha hilo na kusema kuwa yupo mbioni kwenda mahakamani,mbunge huyo wa zamani aliangushwa kwenye uchaguzi mkuu uliopita na mbunge wa sasa kupitia Chadema mheshimiwa Vincent Nyerere.
Habari zaidi zinasema mbunge huyo wa zamani wa Ccm bwana Mathayo ameamua kuchukua uamuzi huo kutokana na wananchi wa jimbo la Musoma mjini kutomchagua tena kuwa mbunge kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana, hivyo ameamua kuwakomoa wananchi kwa kumyima kura na kuamua kumchagua mbunge wa Chadema.
Mbunge huyo wa zamani ambaye ni mfanyabiashara wa mafuta amesema aliyanunua madawati hayo kwa sh elfu 40,000 kwa kila dawati na jumla alitumia shilingi milioni 18. Anataka arudishiwe madawati au alipwe milioni 18.
Source: Tanzania Daima.
Mwandishi wa Tanzania Daima alipongea naye kwa njia ya simu alilithipitisha hilo na kusema kuwa yupo mbioni kwenda mahakamani,mbunge huyo wa zamani aliangushwa kwenye uchaguzi mkuu uliopita na mbunge wa sasa kupitia Chadema mheshimiwa Vincent Nyerere.
Habari zaidi zinasema mbunge huyo wa zamani wa Ccm bwana Mathayo ameamua kuchukua uamuzi huo kutokana na wananchi wa jimbo la Musoma mjini kutomchagua tena kuwa mbunge kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana, hivyo ameamua kuwakomoa wananchi kwa kumyima kura na kuamua kumchagua mbunge wa Chadema.
Mbunge huyo wa zamani ambaye ni mfanyabiashara wa mafuta amesema aliyanunua madawati hayo kwa sh elfu 40,000 kwa kila dawati na jumla alitumia shilingi milioni 18. Anataka arudishiwe madawati au alipwe milioni 18.
Source: Tanzania Daima.