mchumihalisi
Member
- Oct 8, 2015
- 28
- 98
Moja kati ya taarifa nilizovutiwa nazo baada ya kuingia mtandaoni ni kuhusu kinachoitwa ‘Umafia Mkubwa katika uuzwaji wa Korosho, Viongozi kuwanyonya Wakulima’ Sababu kuu za kunivutia ni sababu Korosho iliwahi kuingia kwenye mzozo mkubwa sana na Rais aliyepita wa awamu ya tano Mh. Magufuli kiasi cha kuamua kupeleka Wanajeshi kwa ajili ya kuhakikisha Korosho zile zinanunuliwa na Serikali na kunakua hakuna longolongo tena.
Baada ya kusoma ‘Ripoti’ hio inayosema Mbunge wa Ruangwa anakula dili na Kampuni ya STABANZA na Mh Mbunge anapata Shilingi 1,000 kwa Kilo nikajiuliza huyo mnunuzi anapata kiasi gani? Muuzaji Je? Na Je ‘Kangomba’ iliwahi kufika mwaka wowote wa mtu kupata hata 500 tu kwa Kila Kilo inayonunuliwa? Watu wa kusini mtujuze.
Kubwa zaidi mtoa maada anaonekana ana chuki binafsi na Mbunge wa Ruangwa sababu ukitazama akaunti yake haina hata siku 3 toka ifunguliwe, Lakini post zake zote zimekua za kumchafua zaidi 'Mbunge huyu' wa Wana ruangwa Je hii tuiite kama dhamira ya kuamua kumvuruga Mbunge kugombana na Wapiga kura wake mpaka kwa Mwenyekiti wa Chama chake Taifa?
Sisi watu wa nje tunaona mafanikio ya Mbunge wa Ruangwa yanayoletwa na Serikali ya CCM kwenye kuhakikisha Wananchi wanapatiwa maendeleo chini ya Amiri Jeshi Mkuu Samia Suluhu Hassani. Mianya ya wapiga dili ikizibwa tusianze kugombanisha Viongozi na Wananchi. Hii nchi inahitaji maendeleo na bila kuwa na Viongozi wakali wanaosimamia haki na maslahi ya Wananchi maendeleo hatuwezi kuyapata.
Bravo Mbunge wa Ruangwa
Baada ya kusoma ‘Ripoti’ hio inayosema Mbunge wa Ruangwa anakula dili na Kampuni ya STABANZA na Mh Mbunge anapata Shilingi 1,000 kwa Kilo nikajiuliza huyo mnunuzi anapata kiasi gani? Muuzaji Je? Na Je ‘Kangomba’ iliwahi kufika mwaka wowote wa mtu kupata hata 500 tu kwa Kila Kilo inayonunuliwa? Watu wa kusini mtujuze.
Kubwa zaidi mtoa maada anaonekana ana chuki binafsi na Mbunge wa Ruangwa sababu ukitazama akaunti yake haina hata siku 3 toka ifunguliwe, Lakini post zake zote zimekua za kumchafua zaidi 'Mbunge huyu' wa Wana ruangwa Je hii tuiite kama dhamira ya kuamua kumvuruga Mbunge kugombana na Wapiga kura wake mpaka kwa Mwenyekiti wa Chama chake Taifa?
Sisi watu wa nje tunaona mafanikio ya Mbunge wa Ruangwa yanayoletwa na Serikali ya CCM kwenye kuhakikisha Wananchi wanapatiwa maendeleo chini ya Amiri Jeshi Mkuu Samia Suluhu Hassani. Mianya ya wapiga dili ikizibwa tusianze kugombanisha Viongozi na Wananchi. Hii nchi inahitaji maendeleo na bila kuwa na Viongozi wakali wanaosimamia haki na maslahi ya Wananchi maendeleo hatuwezi kuyapata.
Bravo Mbunge wa Ruangwa