Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,863
- 930
Mbunge wa Jimbo la Igunga Nicholaus George Ngassa, amewataka Wananchi wa Jimbo la Igunga kutembea kifua mbele kwa kuwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imejipambanua kushughulikia kero za Wananchi, kuimarisha huduma za jamii na kujenga uchumi jumuishi unaogusa maisha ya Watanzania.
Mheshimiwa Ngassa (MB) amesema hayo alipokuwa akizungumza na Wananchi wa Kata ya Mwamashiga kwenye Ziara ya kikazi aliyoifanya Siku ya Jumapili tarehe 26 Machi, 2023.
Aidha Mhe. Jonathan Ntambi, Diwani wa Kata ya Mwamashiga amemuomba Mhe.Ngassa (MB) afikishe shukrani za dhati kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa Fedha za Miradi ya Maendeleo kwa ajili ya Wananchi wa Kata ya Mwamashiga.
"Kazi na Maendeleo"
Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge,
Jimbo la Igunga.
27 Machi, 2023