Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,900
- 944
Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya, Mhe. Masache Kasaka amewasihi waumini wa dini ya kikristo kusoma maandiko ya kibiblia na kuyatendea kazi ikiwemo agizo la kutii wenye mamlaka na kuwaombea kama viongozi wa dini na Serikali.
Mbunge Masache amepata nafasi ya kutoa nasaha hiyo aliposhiriki ibada katika kanisa Katoliki Kigango cha Chalangwa, ambapo amenukuu andiko kutoka kitabu cha Tito. 3:1 kinachosema "Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema"
Pia, Mhe. Masache amechangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa kanisa unaondelea, huku akisisitiza wanawake wajitokeze kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ngazi ya Serikali za mitaa.
Mbunge Masache amepata nafasi ya kutoa nasaha hiyo aliposhiriki ibada katika kanisa Katoliki Kigango cha Chalangwa, ambapo amenukuu andiko kutoka kitabu cha Tito. 3:1 kinachosema "Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema"
Pia, Mhe. Masache amechangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa kanisa unaondelea, huku akisisitiza wanawake wajitokeze kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ngazi ya Serikali za mitaa.