Mbunge Kasaka: Jengeni Imani na Serikali Iliyopo Madarakani

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,903
945
Mbunge wa Jimbo la Lupa wilayani Chunya, mkoani Mbeya, Mhe. Masache Njeru Kasaka amewataka wananchi wa Jimbo hilo kuiamini Serikali Kwa kuwa imeendelea kutekeleza ahadi mbalimbali zilizoahidiwa mwaka 2020

F8FdUTSXMAA0q4y.jpg
Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilayani Chunya amesema, Wilaya ya Chunya imetengewa fedha zaidi ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya kununua vifaa tiba kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na kuahidi zahanati ya Kijiji cha Nkwangu kata ya Upendo kuwa mmoja wa wanufaika wa vifaa hivyo ili kusogeza huduma za kiafya karibu na maeneo yao.

F8FcmhUXEAA8srV.jpg

"Mimi na viongozi wenzangu hatujawaangusha na hatutawaangusha maana tukiwaangusha maana yake tumemwangusha Mhe. Rais Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, jambo ambalo sisi watumishi wenu mliotutuma kuwasemeeni maeneo mbalimbali hatuwezi kufanya hivyo maana hata ninyi ni mashahidi kwamba ahadi tulizo ahidi tunaendelea kuzitekeleza" - Mhe. Masache Kasaka, Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilayani Chunya.

F8FdUfbXgAAupWy.jpg

Mbunge wa Jimbo la Lupa wilayani Chunya Mhe. Masache Kasaka, amewataka wananchi wa Jimbo la Lupa kuendelea kuiamini Serikali anayosema imeendelea kutekeleza ahadi mbalimbali zilizoahidiwa mwaka 2020 kupitia ilani ya CCM ikiwemo ujenzi wa zahanati, uboreshaji sekta ya elimu na miundombinu ya barabara.
 

Attachments

  • F8FcnczXMAAiyHE.jpg
    F8FcnczXMAAiyHE.jpg
    66.6 KB · Views: 1
Imani inajengwa na serikali iliyo madarakani kwa wananchi, sio kulazishwa

Leo PhD ya heshima, serikali yote , wasanii wanajazana India, hii kwangu ni mpya,

Mikata inaingiwa ya ajabu,

Viongozi wajiongezea posho ,mishahara, wananchi hoi, mkiwambia wajiajiri , iyo imani kwa serikali inatoka wapi?
 
Waiamini kivipi?. Wakati ripoti za CAG wamezificha wamebakia kuombeana msamaha.
 
Imani inajengwa na serikali iliyo madarakani kwa wananchi, sio kulazishwa

Leo PhD ya heshima, serikali yote , wasanii wanajazana India, hii kwangu ni mpya,

Mikata inaingiwa ya ajabu,

Viongozi wajiongezea posho ,mishahara, wananchi hoi, mkiwambia wajiajiri , iyo imani kwa serikali inatoka wapi?
Serikali inasimamia usalama wako..... bado huiamini

Serikali ilikufukuzia magaidi wa Kibiti ili unywe kahawa na kukaa VITI VIREFU kwa amani....bado huiamini...

Imekujengea barabara kwa kodi zetu sote ukazitumia barabara hizo.. bado huiamini
 
Serikali inasimamia usalama wako..... bado huiamini

Serikali ilikufukuzia magaidi wa Kibiti ili unywe kahawa na kukaa VITI VIREFU kwa amani....bado huiamini...

Imekujengea barabara kwa kodi zetu sote ukazitumia barabara hizo.. bado huiamini
Azory Gwanda, Ben Saana8 wako wapi? Waliotaka kumuua Lissu ni akina nani? Tuna serikali au genge la wahuni? Watu wanaumizwa kwenye Nchi yao kama wanyama halafu unaleta ufala hapa
 
Huyo mbunge yeye anauhakika na posho za kila mwezi na pindi miaka 5 ya ubunge wake kufika kikomo anachukua zaidi ya milion 200 kwa huo mda mfupi ambazo hata mfanyakazi alietumikia taifa miaka zaidi ya 40 anakutana na kikotoo.
 
Serikali inasimamia usalama wako..... bado huiamini

Serikali ilikufukuzia magaidi wa Kibiti ili unywe kahawa na kukaa VITI VIREFU kwa amani....bado huiamini...

Imekujengea barabara kwa kodi zetu sote ukazitumia barabara hizo.. bado huiamini
Huo ni wajibu sio hisani. Tuamini majizi kivipi?
 
Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilayani Chunya amesema, Wilaya ya Chunya imetengewa fedha zaidi ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya kununua vifaa tiba kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na kuahidi zahanati ya Kijiji cha Nkwangu kata ya Upendo kuwa mmoja wa wanufaika wa vifaa hivyo ili kusogeza huduma za kiafya karibu na maeneo yao.
Tatizo la hawa watu siku hizi ni kupandia kwenye majina ya wengine waliowahi kuwa watu wa kuheshimika katika jamii.

Sasa huyu na Njeru Kasaka wapi na wapi?

Watu wataiamini vipi serikali iliyopo madarakani. Waache kuona madudu yanayofanyika, wao waamini tu basi?

Njeru Kasaka halisi, aliweza kusimama na kusema jambo, na watu nchi nzima wakasikiliza.
Leo anaibuka Njeru mwingine, sijui anao uhusiano gani na Njeru mwenyewe, na kuanza kutoa hadithi za ajabu!
 
Mbunge wa Jimbo la Lupa wilayani Chunya, mkoani Mbeya, Mhe. Masache Njeru Kasaka amewataka wananchi wa Jimbo hilo kuiamini Serikali Kwa kuwa imeendelea kutekeleza ahadi mbalimbali zilizoahidiwa mwaka 2020

Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilayani Chunya amesema, Wilaya ya Chunya imetengewa fedha zaidi ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya kununua vifaa tiba kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na kuahidi zahanati ya Kijiji cha Nkwangu kata ya Upendo kuwa mmoja wa wanufaika wa vifaa hivyo ili kusogeza huduma za kiafya karibu na maeneo yao.


"Mimi na viongozi wenzangu hatujawaangusha na hatutawaangusha maana tukiwaangusha maana yake tumemwangusha Mhe. Rais Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, jambo ambalo sisi watumishi wenu mliotutuma kuwasemeeni maeneo mbalimbali hatuwezi kufanya hivyo maana hata ninyi ni mashahidi kwamba ahadi tulizo ahidi tunaendelea kuzitekeleza" - Mhe. Masache Kasaka, Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilayani Chunya.


Mbunge wa Jimbo la Lupa wilayani Chunya Mhe. Masache Kasaka, amewataka wananchi wa Jimbo la Lupa kuendelea kuiamini Serikali anayosema imeendelea kutekeleza ahadi mbalimbali zilizoahidiwa mwaka 2020 kupitia ilani ya CCM ikiwemo ujenzi wa zahanati, uboreshaji sekta ya elimu na miundombinu ya barabara.
Kinacho jenga imani ya wanachi ni matendo ya haki na usawa ..... siyo matamshi ...... hawa watu wakisha Shiba maharage wanakosaga la kusema
 

MBUNGE KASAKA: JENGENI IMANI NA SERIKALI ILIYOKO MADARAKANI

Mbunge wa Jimbo la Lupa wilayani Chunya, mkoani Mbeya, Mhe. Masache Njeru Kasaka amewataka wananchi wa Jimbo hilo kuiamini Serikali Kwa kuwa imeendelea kutekeleza ahadi mbalimbali zilizoahidiwa mwaka 2020

View attachment 2778839
Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilayani Chunya amesema, Wilaya ya Chunya imetengewa fedha zaidi ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya kununua vifaa tiba kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na kuahidi zahanati ya Kijiji cha Nkwangu kata ya Upendo kuwa mmoja wa wanufaika wa vifaa hivyo ili kusogeza huduma za kiafya karibu na maeneo yao.

View attachment 2778841

"Mimi na viongozi wenzangu hatujawaangusha na hatutawaangusha maana tukiwaangusha maana yake tumemwangusha Mhe. Rais Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, jambo ambalo sisi watumishi wenu mliotutuma kuwasemeeni maeneo mbalimbali hatuwezi kufanya hivyo maana hata ninyi ni mashahidi kwamba ahadi tulizo ahidi tunaendelea kuzitekeleza" - Mhe. Masache Kasaka, Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilayani Chunya.

View attachment 2778843

Mbunge wa Jimbo la Lupa wilayani Chunya Mhe. Masache Kasaka, amewataka wananchi wa Jimbo la Lupa kuendelea kuiamini Serikali anayosema imeendelea kutekeleza ahadi mbalimbali zilizoahidiwa mwaka 2020 kupitia ilani ya CCM ikiwemo ujenzi wa zahanati, uboreshaji sekta ya elimu na miundombinu ya barabara.
Hawa kenge magamba, wakisha Shiba, wanaiona serikali kama vatican ya Roman Catholic, wajenge Imani, serikali imekuwa taasisi ya kidini,kanisa, au dhehebu, Dini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom