Mbunge Lema Anena ya Moyoni

Mbunge Lema Anena ya Moyoni

Hii kesi... ni kwamba washtaki ndo wameomba kesi ifutwe (withdraw charges) au lema ameweza ku prove kuwa yy ni innocent!?? Naombeni mnieleweshe wadau
 
Hii kesi... ni kwamba washtaki ndo wameomba kesi ifutwe (withdraw charges) au lema ameweza ku prove kuwa yy ni innocent!?? Naombeni mnieleweshe wadau
wanasheria wa upande wa CCM/ serikali waliomba ifutwe...
 
Lema anatia aibu wana Arusha!!!

Arusha kutenda kosa sio kosa, ila kurudia kosa ndio kosa; Huyo Lema mkimchagua tena mtakuwa mmefanya kosa kubwa sana.
mkuu nenda kagombee naye ili umshinde mkuu!
 
hakuna aliyebakwa yule mdada ni biashara yake hiyo. Hata wewe kama unataka huduma unaweza kuwasiliana naye haina kinyongo andaa helayako tu.

You are right. Lukosi alifikiri angetajirika kutoka kwa cdm. Imekula kwake. Labda wanaweza kutajirika wiki hii maana Taswira a.k.a Nchemba anaenda huko na hela za ufisadi.
 

mahakama imejiridhisha kuwa mkuu wa mkoa wa arusha alikuja kwenye tukio kama anekwenda kwenye send off party ndiomaana Lema ameibuka mshindi.

Kisheria mahakama haikupata hata nafasi ya kujiridhisha ila kwa kesi kufutwa na upande wa mashtaka kuridhika ni tafsiri ya kuwa wao kama walalamikaji (ni pamoja na mkuu wa mkoa mwenyewe) wanakubaliana na kauli kuwa ni kweli mkuu wa mkoa alienda kama anakwenda kwenye send off party
 
Lema anatia aibu wana Arusha!!!

Arusha kutenda kosa sio kosa, ila kurudia kosa ndio kosa; Huyo Lema mkimchagua tena mtakuwa mmefanya kosa kubwa sana.

Lema alishasema wazi. Adui mkubwa ni uoga. Acheni kuonea wananchi wasiojua haki zao.
Swali. Waziri mkuu ametengua uamuzi gani alivyokwenda Ngorongoro? Wenyewe kwa wenyewe hamjitambui mnafanya nini. Shame on you and you and you.
 
Nawapenda sana Wana Arusha, Allah awalinde dhidi ya madhalimu ya kiccm kama pale Soweto, mungu ibariki Chadema,mungu ibariki Tanzania!
 
Sijaona mtu jasiri kama Mhe. Lema aliwahi kukataa dhamana na kwenda mahabusu kama alivyoamriwa na polisi!!!, huyu ni mwanamapinduzi wa kweli, nawaonea wivu sana wana Arusha mjini. Mimi kwetu Misugwi Mwz eti mawe matatu hovyo tulichemsha bora ya Shibiriti.
 
...ukweli Lema maneno yake yanaishi,trust me kauli hizi ni za kimapinduzi na ni nadra sana kupatikana na daima zitakumbukwa katika harakati za kuikomboa tanganyika...

Nakubaliana nawe kuwa maneno ya Lema ni nadra kuyapata kwa viongozi wa siku za leo ambao kuwaza na kufikiri kabla ya kusema ni msamiati mgumu kwao.

Kufutwa kwa kesi hiyo siyo ushindi dhidi ya lema tu bali ni ushindi kwa wapenda haki wote na ni aibu kwa wale wanaotumia madaraka kunyanyasa watu wanaodhaniwa ni wanyonge. Nasema hivyo kwa kuwa kesi yenyewe ilikuwa ya kukomoana na kuonyeshana mabavu tu ya nani ni nani katika jamii.

Jambo moja ninalofurahi na ninaloamini viongozi wanaotumia mabavu hawana nafasi katika kizazi cha digitali kwani sifa moja ya kizazi cha digitali ni uwazi na ukweli na ya pili ni heshima na kuheshimiwa. Wakiendelea kutumia mabavu na kuonyesha ubabe kwa kuwa tu ni wateule wa Rais basi watabaki na Rais na watu watachukua ustaarabu wao wa maisha kama inavyofanyika sasa Arusha. Wajifunze kusoma alama za nyakati.
 
Dr Slaa alisema hizi ni dalili za utawala unaoanguka! Mi sielewi maccm yanadhani yatmuongoza nani miaka miwili ijayo, maana yanagombana na waandishi wa habari kwa kufungia magazeti na kuwang'oa kucha na meno, yanagombana na wafanyakazi, yamegombana na wakulima, yamegombana na wanafunzi, yanabomoa nyumba za watu nk nk nk!
Mwisho umefika na utawala unaaguka!
 
Jamani mwenye copy ya mashitaka naomba atuwekee tujikumbushe kidogo. Nilipoisoma mwanzo sikuamini kuna waendesha mashitaka wa serikali vihiyo namna hii. I hope they are not my classmates.
 
Jamani mwenye copy ya mashitaka naomba atuwekee tujikumbushe kidogo. Nilipoisoma mwanzo sikuamini kuna waendesha mashitaka wa serikali vihiyo namna hii. I hope they are not my classmates.

Mkuu ukikubali kutumiwa na ccm lazima ujitie uchizi kiasi, wanaokutumia wao wenyewe "tabula rasa" unatarajia utawatumikia ukiwa na akili zako!? I bet ni qualified learned brothers ila ndo vile tena wamekubali kuingia katika mtego wa mashetani..
 
Vipi ile ya kubaka chizi nayo ameshinda?


Kama kesi hiyo ipo kwanini serikali haijachukua hatua hadi leo au ndio kusema ni mfumo wa kulindana. mm naona madai hayo ni ya uongo, kama kweli alibaka angekuwa tayari amekamatwa na polisi wa kimataifa ambao wanaruhusiwa kuingia nchi yoyote kumkamata mtu yeyote kwa kushirikiana na vyombo vya nchi hiyo na kumfikisha mahakamani katika nchi husika.

Mbona balozi wa Tanzania New York aliyemdhalilisha msichana wa kazi, alishitakiwa na kupigwa faini kubwa, iweje Mhe. Lema ashindikane kushitakiwa?

mm naona hizo ni propaganda na siasa za maji taka za ccm wala hakuna ubakaji wala hakubaka mtu

kuhusu Dr. Slaa, si dhani kuwa dhambi zake ni nyingi kiasi hicho, yy haya aliyofanya hayaathiri maisha ya mtu yeyote lkn ccm walichofanya kinatisha hata kukizungumzia, wengine wamevunja ndoa za watu, wengine wanatembea na wake za watu, wengine wana nyumba ndogo kibao, wengine wauza unga yaani dawa za kulevya, Richmond, Dowans, EPA, IPL, kiwira, bulyankulu, meno ya tembo, utoroshaji wa wanyama hai, n.k. Makamba mnajua kilichomfukuza kazi ya ualimu kigoma, msifuate mkumbo, tafitini kabla ya kusema na kuandika

mnakumbuka kifo cha mwangosi nyororo Iringa, Dr Ulimboka kutezwa, kibanda, kesi ya ugaidi ya Rwakatare na CDM n.k. nani aliyeidanganya serikali na kusababisha hasara kubwa aliyeshitakiwa?fikiria mafuta ya kujaza helikopa yalipatikana na kuwasafirisha washiakiwa watano 3 tu kutoka DSM hadi Shinyanga, mwisho wa siku Mahakama inasema haioni gaidi yeyote mbele yake kwa mujibu wa sheria. kisha jaji akawaonya wanasiasa waache kutumia siasa kuwabambikia watu kesi? je kwann aliyewabambikia kesi hajashitakiwa? kama watz tulitarajia tungepewa taarifa ya kina kuhusu suala hili. ila sina hakika kama walirudishwa kwa helikopta hadi Dsm

mm sitaamini propaganda dhaifu dhidi ya Mhe. Lema hadi pale atakaposhitakiwa na kutiwa hatiani

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika, Wabariki na watu wake wawe na fikra za utafiti ili wapate maendeleo ya kweli na kuondokana na umasikini
 
Mkuu wa mkoa alikwenda kwenye tukio lile la mauaji ya mwanafunzi wa chuo cha uhasibu kama anakwenda kwenye send-off. Ndivyo ilivyo.

CC: HAMY-D

Lema ni mtu wa kuhurumiwa, lakini wanao mshabikia ni wa kuhurumiwa zaidi. Mkuu Arushaone usijishushe kwa kumshabikia Lema, una heshima humu JF.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom