buswelu moja
JF-Expert Member
- Aug 24, 2014
- 226
- 183
MBUNGE CATHERINE MAGIGE YUKO MAJI YASHINGO UCHAGUZI UWT ARUSHA.
Wadau wa JF,
Wakati uchaguzi wa UWT wilayani Arusha ukitaraji kufanyika kesho hali imeelezwa kuwa mbaya sana kwambunge wa viti maalumu mkoani Arusha,Bi Catherine Magige.
Hali hiyo imemlazimu achanganyikiwe na kuanza kugawa fedha kwa wajumbe kutoka wilaya za mkoa wa Arusha kama njuguna taarifa za ndani zinadai tayari milioni 20 tangu jana imekuwa ikisambazwa na wapambe wake kwa wajumbe hao.
Lakini kituo ni kwamba le Magige amelazimika kumwangukia mkuu wa mkoa wa Arusha,Daud Felix Ntimbenda amwokolee jahazi linalotaraji kuzama kesho.
Inadaiwa kuwa Magige anamtumia mkuu wa mkoa huyo kuwatisha baadhi ya wagombea na wajumbe akiwemo hasimu wake Violet Mfuko ambaye anampa joto Magige kwenye uchaguzi wa kesho na inasemekana kama haki ikitendea basi ataibuka kidedea.
Magige,anapita mitaani akitamba kwamba ana mahusiano ya kimwili na RC huyo hivyo amemwahidi kumbeba katikauchaguzi wa kesho hizi taarifa zimesambaa kwa kasi hapa Arusha.
Tukio jingine ni kwamba mwenyekiti wa UVCCM,Robinson Meitinyiku wa hapa mkoani Arusha pamoja na yule wa UWT,Flora Zelothe wanatengenezewa zengwe na Magige kwakuwa wamekuwa wakiendesha harakati za kutaka kumwangusha katika uchaguzi wakesho.
Taarifa zinadai kuwa leo Robinsonalish atakiwa kwa RC ARUSHA kwamba yeye ndiye anayesambaza picha ya Catherine akiwa na Bernad Membe ambaye alihaidi kumsaidia katika uchaguzi wa kesho huku Zelothe akifuatwa ofisini na maofisa wa Takukuru kwa madai kuwa anagawa rushwa kama mojawapo ya vitisho na kuna taarifa kwamba maofisa hao wamemnyang'anya simu zake zote za mkononi.
Kituko kingine kuna mtumishimmojawapo wa idara ya uhamiaji mkoani Arusha aliyetambulika kwa jina moja la Ally amesimamishwa kazi kwa amri ya mkuuwa mkoa wa Arusha kwa madai kuwa yeye ndiye anasambaza ujumbe wa kumchafuaMagige na kesho ameitwa kwenye kikao cha maadili hapo ofisini kwao.
Kuna mengi tutasikia uchaguzi wasafari hii lakini kinachoonekana Catherine ataangukia pua kwa kuwa tangu apeweubunge alikimbia Arusha na sasa amerudi tena kuomba ridhaa wajumbe wamesema NO.
Inasemekana mchuano wa kesho ni kati ya Catherine na Viola kwani Zelothe ambaye ni mkiti wa UWT anamuunga mkono Viola.
Kesho ni kesho tutawapasaha mengiwadau wa jukwaa hili lakini taaarifa za kuelekea uchaguzi zinakuja kila hatuakuanzaia sasa hivyo mkae mkao wa kula.
CHANZO: MDAU WA ARUSHA
Pichani chini ni Violet Mfuko (aliyevaa miwani),Flora Zelothe (aliyeshikilia kipaza sauti) na Catherine Magige akiwa bungeni kwenye vikao vilivyopita vya Bunge la Jamhuri.
Wadau wa JF,
Wakati uchaguzi wa UWT wilayani Arusha ukitaraji kufanyika kesho hali imeelezwa kuwa mbaya sana kwambunge wa viti maalumu mkoani Arusha,Bi Catherine Magige.
Hali hiyo imemlazimu achanganyikiwe na kuanza kugawa fedha kwa wajumbe kutoka wilaya za mkoa wa Arusha kama njuguna taarifa za ndani zinadai tayari milioni 20 tangu jana imekuwa ikisambazwa na wapambe wake kwa wajumbe hao.
Lakini kituo ni kwamba le Magige amelazimika kumwangukia mkuu wa mkoa wa Arusha,Daud Felix Ntimbenda amwokolee jahazi linalotaraji kuzama kesho.
Inadaiwa kuwa Magige anamtumia mkuu wa mkoa huyo kuwatisha baadhi ya wagombea na wajumbe akiwemo hasimu wake Violet Mfuko ambaye anampa joto Magige kwenye uchaguzi wa kesho na inasemekana kama haki ikitendea basi ataibuka kidedea.
Magige,anapita mitaani akitamba kwamba ana mahusiano ya kimwili na RC huyo hivyo amemwahidi kumbeba katikauchaguzi wa kesho hizi taarifa zimesambaa kwa kasi hapa Arusha.
Tukio jingine ni kwamba mwenyekiti wa UVCCM,Robinson Meitinyiku wa hapa mkoani Arusha pamoja na yule wa UWT,Flora Zelothe wanatengenezewa zengwe na Magige kwakuwa wamekuwa wakiendesha harakati za kutaka kumwangusha katika uchaguzi wakesho.
Taarifa zinadai kuwa leo Robinsonalish atakiwa kwa RC ARUSHA kwamba yeye ndiye anayesambaza picha ya Catherine akiwa na Bernad Membe ambaye alihaidi kumsaidia katika uchaguzi wa kesho huku Zelothe akifuatwa ofisini na maofisa wa Takukuru kwa madai kuwa anagawa rushwa kama mojawapo ya vitisho na kuna taarifa kwamba maofisa hao wamemnyang'anya simu zake zote za mkononi.
Kituko kingine kuna mtumishimmojawapo wa idara ya uhamiaji mkoani Arusha aliyetambulika kwa jina moja la Ally amesimamishwa kazi kwa amri ya mkuuwa mkoa wa Arusha kwa madai kuwa yeye ndiye anasambaza ujumbe wa kumchafuaMagige na kesho ameitwa kwenye kikao cha maadili hapo ofisini kwao.
Kuna mengi tutasikia uchaguzi wasafari hii lakini kinachoonekana Catherine ataangukia pua kwa kuwa tangu apeweubunge alikimbia Arusha na sasa amerudi tena kuomba ridhaa wajumbe wamesema NO.
Inasemekana mchuano wa kesho ni kati ya Catherine na Viola kwani Zelothe ambaye ni mkiti wa UWT anamuunga mkono Viola.
Kesho ni kesho tutawapasaha mengiwadau wa jukwaa hili lakini taaarifa za kuelekea uchaguzi zinakuja kila hatuakuanzaia sasa hivyo mkae mkao wa kula.
CHANZO: MDAU WA ARUSHA
Pichani chini ni Violet Mfuko (aliyevaa miwani),Flora Zelothe (aliyeshikilia kipaza sauti) na Catherine Magige akiwa bungeni kwenye vikao vilivyopita vya Bunge la Jamhuri.