Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 80,839
- 93,626
Wabunge kama kibajaji unategemea kuna akili humo ndani?Inaudhi sana, nashindwa kuelewa kwann serikali isifanye biashara za uzalishaji ipate hela waache kutukamua kiasi hiki. Nchi nzima kila kona traffic polisi wanavizia madreva wawanyuke notifications
Hizo mnatakiwa mfunge, hiyo teknolojia ni ya karne ya 15Hv mafuta ni kwa ajili ya vyombo vinavyotembea barabarani tu?? Vipi cc wenye mashine za kusaga??
Sijuwi umeshiba maharage ya wapi !!!!!Ni ujinga kusema road licence iende kwenye mafuta, petrol na diesel haitumiwi na magari tu. Lakin pesa itakuwa kubwa sana.
Kwani ukipaki gari nani aliesema lazima uilipie Road licence, ukipaki gari nenda TRA sitisha usajili mpka utakapoirudisha na haitakuwa ikihesabu.
Mtu anashindwa kulipa pesa ndogo tu ya road licence ulinunia gari ya nini? Ninyi ndio mnanunia matairi ya elfu 20 expired mitaani ilimradi watu wakuone tu na gari
Huu mchango ni wa kijinga, charges za mafuta zitakuwa juu na zitagusa wasio na magari pia. ROAD LICENCE ibaki kama ni kuomba basi ifutwe kabisa ila sio kwenda kwenye mafuta.
Kama gari lako limepaki ukitaka lisihesabu nenda tra wape plate namba zao waambie nimepaki gari, ukirudi itaanzia ulipoishia
katoa mfano tu, sio pendekezo...akili hizi !!!1 pole pole tu tutafikaWe jamaa vipi ww?hela yote hiyo?unataka tutiane umaskini?waweke shilingi tu kwa liter
Hii si itawafanya baadhi ya wamiliki wa magari na vyombo vya barabarani kwenda na vidumu kununua mafuta ya vyombo vyao huko ili kukwepa hiyo increment?Kutakuwa na vituo vya aina mbili. Vtuo vya mafuta vya wenye vyombo vya moto (gari,pkpk nk), Na vituo vya mafuta kwa ajili ya majenereta na vifaa vingine visivyotembea baraabarani????
hoja ya maana sana hii ila imekosa wachangiaji ingekuwa udaku ingekuwa na page kadhaa
Tatizo wataingia tamaa ya kuweka hela kuubwaaaa,, kumbe hata wakiweka shilingi 30 tu kwa lita ni hela kubwa kuliko road license yenyewe!Katika mambo muhinu yatakayoleta pesa bila shida ni hilo na uhalisia let's say hata wakiweka shilingi hamsini tu watapata income kubwa sana! basi inayotumia 600 lts a day italipa 30000 Kwa siku times 30 Kwa mwezi pekee itakua 900000 Kwa mwaka ni hela ya kutosha! na wakifanya hivyo hata machines zisizo fika barabarani zitachangia pato kubwa LA taifa! imaging machines za migodini per day wanatumia mpaka Lita 10000 plus hivi watasumbuana na daladala kweli! please wabunge amkeni itasaidia all way out
Mfano mzuri tu ni wenzetu Uganda waliweka kwenye mafuta na imewaletea mafanikio sana hakuna kukimbizana
Hii ni moja ya michango bora katika Bunge linaloendelea sasa. Hamna gari inayostahili kulipia road licence kama haipo barabarani, cha ajabu wamiliki wenye magari yasiyotembea kwa ubovu ama ajali yangali yanachajiwa road licence na penalty juu na zaidi ya yote hata kama gari langu ni zima ila siko barabarani kwa muda tajwa ya nini nilipie road licence?
Wenye mamlaka jiongezeni kidogo tu, hamna gari itakayokuwa barabarani bila nishati na kadiri mtu atakavyotumia barabara ndivyo jinsi itakovyombidi kununua nishati husika na ndivyo jinsi atakavyolipia barabara na probably kipato cha serikali kitaongezeka zaidi.
Hongera mtoa hoja, hongera wabunge wote mwitikio wenu tumeuona, kazi kwenu serikali!!
=====
Serikali imeahidi kuifanyia marekebisho sheria inayoagiza tozo ya umiliki wa vyombo vya moto (road license) ili kuondoa kero kwa wananchi.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji amesema hayo bungeni leo (Ijumaa) alipojibu swali la Dk Raphael
Chegeni aliyetoa pendekezo hilo ili kodi hiyo iendane na matumizi halisi ya vyombo vya moto barabarani.
"Tozo hii ipo kisheria. Serikali imesikia mapendekezo ya wabunge na itaangalia namna nzuri ya kuboresha ukusanyaji wa mapato hayo," amesema Dk Kijaji.
Wabunge wengi, akiwamo Spika wa Bunge Job Ndugai wamependekeza kufutwa kwa kodi hiyo inayowaathiri zaidi walioegesha magari kwa muda mrefu kutokana na ubovu au ajali.
Yani huyo kessy simpendagi hata cjasoma, aliyosoma anifupishie ila huyu mda mwingi huwa ni mento