Mbunge Ally Kessy: Road licence ihamishiwe kwenye mafuta(petrol & diesel)

KIMIYAKIMIYA

JF-Expert Member
Mar 2, 2014
230
309
Hii ni moja ya michango bora katika Bunge linaloendelea sasa. Hamna gari inayostahili kulipia road licence kama haipo barabarani, cha ajabu wamiliki wenye magari yasiyotembea kwa ubovu ama ajali yangali yanachajiwa road licence na penalty juu na zaidi ya yote hata kama gari langu ni zima ila siko barabarani kwa muda tajwa ya nini nilipie road licence?

Wenye mamlaka jiongezeni kidogo tu, hamna gari itakayokuwa barabarani bila nishati na kadiri mtu atakavyotumia barabara ndivyo jinsi itakovyombidi kununua nishati husika na ndivyo jinsi atakavyolipia barabara na probably kipato cha serikali kitaongezeka zaidi.

Hongera mtoa hoja, hongera wabunge wote mwitikio wenu tumeuona, kazi kwenu serikali!!


=====

Serikali imeahidi kuifanyia marekebisho sheria inayoagiza tozo ya umiliki wa vyombo vya moto (road license) ili kuondoa kero kwa wananchi.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji amesema hayo bungeni leo (Ijumaa) alipojibu swali la Dk Raphael Chegeni aliyetoa pendekezo hilo ili kodi hiyo iendane na matumizi halisi ya vyombo vya moto barabarani.

"Tozo hii ipo kisheria. Serikali imesikia mapendekezo ya wabunge na itaangalia namna nzuri ya kuboresha ukusanyaji wa mapato hayo," amesema Dk Kijaji.

Wabunge wengi, akiwamo Spika wa Bunge Job Ndugai wamependekeza kufutwa kwa kodi hiyo inayowaathiri zaidi walioegesha magari kwa muda mrefu kutokana na ubovu au ajali.
 
Katika mambo muhinu yatakayoleta pesa bila shida ni hilo na uhalisia let's say hata wakiweka shilingi hamsini tu watapata income kubwa sana! basi inayotumia 600 lts a day italipa 30000 Kwa siku times 30 Kwa mwezi pekee itakua 900000 Kwa mwaka ni hela ya kutosha! na wakifanya hivyo hata machines zisizo fika barabarani zitachangia pato kubwa LA taifa! imaging machines za migodini per day wanatumia mpaka Lita 10000 plus hivi watasumbuana na daladala kweli! please wabunge amkeni itasaidia all way out
 
Katika mambo muhinu yatakayoleta pesa bila shida ni hilo na uhalisia let's say hata wakiweka shilingi hamsini tu watapata income kubwa sana! basi inayotumia 600 lts a day italipa 30000 Kwa siku times 30 Kwa mwezi pekee itakua 900000 Kwa mwaka ni hela ya kutosha! na wakifanya hivyo hata machines zisizo fika barabarani zitachangia pato kubwa LA taifa! imaging machines za migodini per day wanatumia mpaka Lita 10000 plus hivi watasumbuana na daladala kweli! please wabunge amkeni itasaidia all way out
We jamaa vipi ww?hela yote hiyo?unataka tutiane umaskini?waweke shilingi tu kwa liter
 
Hii ni hoja yenye mashiko, ni changamoto kubwa kuwa na watoza kodi wasiojua kazi yao, nchi yetu inahitaji mageuzi makubwa kwenye kodi zinazotozwa na viwango vyake.
 
huo ndio ukweli..waitoe waihamishie kwenye mafuta...nitafurah san hili liifanyika
 
Naunga mkono hoja, ni kweli tozo la R/L lihamishiwe kwenye mafuta kwani hakuna gari itakayotembea bila mafuta, lakini huu utaratibu wa sasa unaumiza sana kwa wenye magari yaliyosimama bila kutumika kutokana na sababu mbalimbali.
 
kama huna gari au ijawahi kukukuta uwezi elewa maana ya huu mchango ila ki ukweli kuna haja ya kufanyia kazi hili jambo,je wataelewa na wanavyo penda kukusanya pesa bila kujali hali
 
Yani huyo kessy simpendagi hata cjasoma, aliyosoma anifupishie ila huyu mda mwingi huwa ni mento
 
Back
Top Bottom