Mbunge akitekeleza majukumu ya jimbo anatoa msaada?

Mbopo

JF-Expert Member
Jan 29, 2008
2,532
413
Juzi juzi nilisoma habari katika moja ya magazeti ya kila siku, likiripoti kwamba Mbunge wa Mvomero Mheshimiwa Amos Makalla ametoa msaada wa mipira 23 pamoja na seti za sare za michezo kwa vikundi vya vijana ambao ni wapiga kura wa jimboni kwake. Hili neno msaada lilinipa maswali kidogo hasa nikizingatia kwamba moja ya majukumu ya mbunge ni kutekeleza ahadi za chama chake kama zilivyoainishwa katika ilani yao ya uchaguzi, lakini vile vile kutekeleza ahadi zake mwenyewe. Mbunge pia ana wajibu wa kuhakikisha ustawi wa wananchi wa jimbo lake kwa kipindi chote cha ubunge wake. Sasa iweje kutekeleza majukumu haya kuwe ni msaada wakati aliomba kuchaguliwa na kuwaongoza wananchi wake ili atoe huduma hizo?

Hii ikanikumbusha hoja ambayo aliitoa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Africa Mashariki wa Uganda (wakati huo) Eliya Kategeya ambaye alisema kwamba wapiga kura wa Afrika wanahitaji kupewa elimu ya uraia ili wajue haki na wajibu wao na akatoa mfano wa wapiga kura wa huko Uganda ambavyo wanaandaa nyimbo na sherehe za kumpongeza na kumshukuru mbunge au waziri aliyefanikisha ujenzi wa barabara, bila kujua kwamba ujenzi huo umefanikishwa kwa kodi zao hao wananchi na kwamba sasa wanalipwa kutokana na kodi zao hizo. Kwa hakika elimu ya uraia inahitajika pia hata kwa waandishi wanaoripoti matukio ya namna hii.
 
Mbopo, natamani ungeona jinsi wabunge wetu wanavyojipiga kifua na kutoa jeuri kwamba yeye anafanya hivyo kwa mapenzi mema kwa wananchi wao wakati ukifika wakati wa kura za maoni au uchaguzi wanapiga magoti wakiomba waongezewe muda kwa sababu kuna mipango waliyopanga na inahitaji muda kuitekeleza. Bure kabisa!
 
Hata hao wabunge wenyewe wanastahili kupewa elimu ili kujua kwamba hawafanyi favour yoyote kwa kufanya hayo wanayofanya. Na ndiyo maana wakishindwa kutekeleza tunawalaumu na kuwapiga chini.
 
Hapa tatizo kubwa ni kwa wananchi kudhani kuwa mbunge ni mfadhili wa kuwasaidia au kuwatatulia matatizo yao. Hii inasababishwa na fulana, khanga na kofia tunazogawiwa kila wakati wa kampeni za uchaguzi.
Mbunge akishachaguliwa anakuwa kimbilio la wananchi kutaka wasaidiwe kusomeshewa watoto wao, na matatizo kadha wa kadha. Ndiyo maana wabunge wetu siku hizi wakishindwa kwenye uchaguzi basi hung'oa vitasa kwenye ofisi, au hudai madawati waliyochonga walipokuwa madarakani.
 
Hapa tatizo kubwa ni kwa wananchi kudhani kuwa mbunge ni mfadhili wa kuwasaidia au kuwatatulia matatizo yao. Hii inasababishwa na fulana, khanga na kofia tunazogawiwa kila wakati wa kampeni za uchaguzi.
Mbunge akishachaguliwa anakuwa kimbilio la wananchi kutaka wasaidiwe kusomeshewa watoto wao, na matatizo kadha wa kadha. Ndiyo maana wabunge wetu siku hizi wakishindwa kwenye uchaguzi basi hung'oa vitasa kwenye ofisi, au hudai madawati waliyochonga walipokuwa madarakani.

You are very right mkuu. Tena wanavyokasirika utadhani ubunge ni mali yao binafsi na wengi wao huishia kuondoka kwa kisukari au presha baada ya hapo.
 
Elimu ya uraia yahitajika sana ili wananchi waelewe wajibu wa viongozi wanaowachagua...wananchi wamejenga hulka ya kuchagua watu wenye uwezo wa fedha kuwa viongozi wao na wanaishia kuwababaikia badala ya kuwatumikisha kulingana na nafasi walizochaguliwa.
 
Hapa Dar mbunge wetu alitoa ahadi ya mambo ambayo angeyatekeleza katika siku 100 za kwanza za ubunge wake. Walipomfuata siku 200 baadaye na kumuuliza kulikoni akawajia juu na kuwambia kwamba hata mimba ikitunga huchukua miezi tisa ndiyo mtoto anazaliwa. Akawataka waache kumkera maana hata suti 4 hajanunua toka achaguliwe.
 
Hao wana Mvomero wamepewa mipira na jezi ili wachezecheze na kusahau shida zao na ikifika 2015 wawe wapole na watoe tena kura zao. Hii ndo bongo bana, tumia ujinga na umaskini wa wananchi wako uwatawale milele. Well done Brother Amos Makala, Big up sana.
 
Elimu ya uraia yahitajika sana ili wananchi waelewe wajibu wa viongozi wanaowachagua...wananchi wamejenga hulka ya kuchagua watu wenye uwezo wa fedha kuwa viongozi wao na wanaishia kuwababaikia badala ya kuwatumikisha kulingana na nafasi walizochaguliwa.

Very true. Kama huna hela wewe huna sifa ya kuwa kiongozi bora na vile visenti vya wakati wa uchaguzi ndiyo huwa kitanzi cha wapiga kura na jamaa wanakuwa wajeuri kila wakifuatwa.
 
Hao wana Mvomero wamepewa mipira na jezi ili wachezecheze na kusahau shida zao na ikifika 2015 wawe wapole na watoe tena kura zao. Hii ndo bongo bana, tumia ujinga na umaskini wa wananchi wako uwatawale milele. Well done Brother Amos Makala, Big up sana.

Lakini moyoni mwao hawana hata chembe ya huruma wanapoona watu waliowafikisha hapo walipo wakokosa mahitaji ya msingi kama maji na huduma za matibabu wakati wao wanaishi maisha ya kifahari ambayo yametokana na wananchi hao? Sasa huo mpira wakiumia wanatibiwaje? Wamuogope Mungu!
 
Very true. Kama huna hela wewe huna sifa ya kuwa kiongozi bora na vile visenti vya wakati wa uchaguzi ndiyo huwa kitanzi cha wapiga kura na jamaa wanakuwa wajeuri kila wakifuatwa.

hali hii inawapa kiburi sana 'viongozi' wa aina hii na ndio chanzo cha kutokupiga hatua kimaendelo.
 
Hakuna kitu huwa kinaniudhi kama magazeti ya bongo ambavyo huwa yanaripoti kuhusu hii the so called misaada ya wabunge, na most likely ni kwa baraka zao: Mfano

1. Makala amimina misaada Mvomero

2. Zungu amwaga misaada Ilala

3. Serukamba aitikisa Kigoma kwa misaada..........etc etc etc.

Kazi ya mbunge facilitation, na tunahitaji wabunge wanaothink big!!!!!!! Hzi biashara za visima, sijui amemwaga misaada eti kwa kusaidia SACCOS sh. laki mbili, au kutembelea yatima anybody able can do it! Tunahitaji wabunge watakaofacilitate mbinu mpya za kilimo, upatikanaji wa mabwawa makubwa ya umwagiliaji, Ubununifu kwa ajira za vijana na si hawa wa kumimina na kumwaga misaada.
 
Msaada wa mipira! duh ndio maana kwetu vunjo upumbavu wa misaaada kama hiyo hatuitaki kamwe a wabunge wetu wanajua hilo.
 
Hakuna kitu huwa kinaniudhi kama magazeti ya bongo ambavyo huwa yanaripoti kuhusu hii the so called misaada ya wabunge, na most likely ni kwa baraka zao: Mfano

1. Makala amimina misaada Mvomero

2. Zungu amwaga misaada Ilala

3. Serukamba aitikisa Kigoma kwa misaada..........etc etc etc.

Kazi ya mbunge facilitation, na tunahitaji wabunge wanaothink big!!!!!!! Hzi biashara za visima, sijui amemwaga misaada eti kwa kusaidia SACCOS sh. laki mbili, au kutembelea yatima anybody able can do it! Tunahitaji wabunge watakaofacilitate mbinu mpya za kilimo, upatikanaji wa mabwawa makubwa ya umwagiliaji, Ubununifu kwa ajira za vijana na si hawa wa kumimina na kumwaga misaada.

Ndugu yangu utahangaika sana kupata wabunge wenye ubunifu huo na ukibahatika basi hata asilimia 0.5 ya wabunge wote haifiki. Lakini kama ulivyosema, ukiwa na waandishi ambao wanapakatwa na wabunge matokeo yake ni haya na siku ukiona mwandishi anamkosoa mbunge basi ujue wamekorofishana kwa mambo binafsi na hasa mshiko. Aibu kubwa sana na ni changamoto kwa wamiliki wa vyombo vya habari!
 
Juzi juzi nilisoma habari katika moja ya magazeti ya kila siku, likiripoti kwamba Mbunge wa Mvomero Mheshimiwa Amos Makalla ametoa msaada wa mipira 23 pamoja na seti za sare za michezo kwa vikundi vya vijana ambao ni wapiga kura wa jimboni kwake. Hili neno msaada lilinipa maswali kidogo hasa nikizingatia kwamba moja ya majukumu ya mbunge ni kutekeleza ahadi za chama chake kama zilivyoainishwa katika ilani yao ya uchaguzi, lakini vile vile kutekeleza ahadi zake mwenyewe. Mbunge pia ana wajibu wa kuhakikisha ustawi wa wananchi wa jimbo lake kwa kipindi chote cha ubunge wake. Sasa iweje kutekeleza majukumu haya kuwe ni msaada wakati aliomba kuchaguliwa na kuwaongoza wananchi wake ili atoe huduma hizo?

Hii ikanikumbusha hoja ambayo aliitoa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Africa Mashariki wa Uganda (wakati huo) Eliya Kategeya ambaye alisema kwamba wapiga kura wa Afrika wanahitaji kupewa elimu ya uraia ili wajue haki na wajibu wao na akatoa mfano wa wapiga kura wa huko Uganda ambavyo wanaandaa nyimbo na sherehe za kumpongeza na kumshukuru mbunge au waziri aliyefanikisha ujenzi wa barabara, bila kujua kwamba ujenzi huo umefanikishwa kwa kodi zao hao wananchi na kwamba sasa wanalipwa kutokana na kodi zao hizo. Kwa hakika elimu ya uraia inahitajika pia hata kwa waandishi wanaoripoti matukio ya namna hii.

Ndugu yangu haya ndiyo yanayorudisha nyuma maendeleo ya nchi hii. Wapiga kura wanaswagwa kama mifugo na wenyewe ukiwasikia wanavyojipiga kifua na kutamka "jimboni kwangu" mara mia mia utadhani ni watu wa maana sana. Hata hizo constituency development funds sijui zinafanya kazi gani!
 
Hapa Dar mbunge wetu alitoa ahadi ya mambo ambayo angeyatekeleza katika siku 100 za kwanza za ubunge wake. Walipomfuata siku 200 baadaye na kumuuliza kulikoni akawajia juu na kuwambia kwamba hata mimba ikitunga huchukua miezi tisa ndiyo mtoto anazaliwa. Akawataka waache kumkera maana hata suti 4 hajanunua toka achaguliwe.

Nataka niipige moto kadi yangu ya kupigia kura.
 
Mbopo, natamani ungeona jinsi wabunge wetu wanavyojipiga kifua na kutoa jeuri kwamba yeye anafanya hivyo kwa mapenzi mema kwa wananchi wao wakati ukifika wakati wa kura za maoni au uchaguzi wanapiga magoti wakiomba waongezewe muda kwa sababu kuna mipango waliyopanga na inahitaji muda kuitekeleza. Bure kabisa!

Uzuri ni kwamba hata miaka mitano nayo inakimbia kama feni. Tutawaona safari hii wanakuja na staili ipi. Lakini kwa kweli inakera kuona watu wanalamba miguu watu walioomba kufanya kazi ya kuleta maendeleo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom