Mbunge adaiwa kuibiwa mil. 440/-

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,001
9,866
1578379337226.png


Mamilioni hayo ya shilingi yanadaiwa kuwa mali ya Mbunge wa Viti Maalum, Jackline Ngonyani (CCM).

Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Kanda ya Songea, Shabani Mwigole, jana alidai mahakamani mbele ya Hakimu Mkazi Kussaga Majinge kuwa kati ya Novemba 27, 2015 na Desemba 31, 2019, katika Benki ya CRDB Tawi la Songea, mshtakiwa, aliiba Sh. milioni 440, mali ya Jackline Ngonyani kinyume cha sheria.

Mwigole alidai kuwa mshtakiwa aliiba fedha alizopatiwa na mbunge huyo kwa lengo la kuzihifadhi kwenye yake ya benki, akifafanua kuwa badala ya kuzihifadhi, mfanyabiashara huyo anadaiwa kuzitumia kwa mambo yake binafsi, kinyume cha makubaliano yao.

Hata hivyo, mshtakiwa alikana shtaka hilo na kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Januari 17, mwaka huu.

Hakimu Mkazi Majige alisema dhamana ya mshtakiwa iko wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini watatu, wenye mali zisizohamishika zikiwa na thamani ya Sh. milioni 133 kila mmoja.

Chanzo: Nipashe
 
Hakika kazi ya ubunge raha sana, ndio maana siku hizi maprofesa, madaktari, wahasibu, wanasheria wote wanakimbilia huko, inalipa vizuri sana, uwe na jimbo, au uwe viti maalum, wewe tayari ni tajiri.

Milioni 400/= unampa mtu akupelekee bank, wewe uko busy na nini?!, hata jimbo huna!.wacha huyo mjasiriamali apite nazo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbunge huyu achunguzwe huenda akawa alikuwa anafisadi na kuwatuma watu wamuwekee pesa hizo labda kukwepa kamati ya maadili na fedha inayomtaka mtumishi wa umma kuorodhesha mali zake.

Alafu wabunge wa CCM mbona kama hamna hamueleweki unawezaje kumpa pesa mtuy et akupelekee bank kuanzia mwaka 2015 mpaka 2019 hujafuatlia unakuja kuibuka sasa.

Hata ningekuwa mimi ningekana. maana duuuuu!

Inaweza kuwa kweli akili ndogo inaongoza akili kubwa !
 
Hakika kazi ya ubunge raha sana, ndio maana siku hizi maprofesa, madaktari, wahasibu, wanasheria wote wanakimbilia huko, inalipa vizuri sana, uwe na jimbo, au uwe viti maalum, wewe tayari ni tajiri.

Milioni 400/= unampa mtu akupelekee bank, wewe uko busy na nini?!, hata jimbo huna!.wacha huyo mjasiriamali apite nazo.

Sent using Jamii Forums mobile app
hapa kuna "Gain tax"
 
wala hajui hiyo pesa kampatia lin make kataja mda usio na uhakika 2015_2019 haiingii akil juu ya uhalali wa madai hayo
 
Safi sana
Naomba money laundering ihamie upande wa pili wapate raha ya kuipitisha express.
 
Back
Top Bottom