Mbowe - Ushahidi wa Video kwa Tume huru ya kimahakama si polisi watuhumiwa

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,899
Lema,+mbowe+Nyerere.jpg

Freeman Mbowe na Lema walipotinga kituo cha polisi

USHAHIDI WA VIDEO KUHUSU SHAMBULIO LA BOMU ARUSHA
Msimamo wa Mbowe - Tume huru ya kimahakama si polisi watuhumiwa
Kuhusu ushahidi anaodai unawahusisha polisi na tukio la bomu, Mbowe alisisitiza kuwa
Chadema kina ushahidi wa kutosha kuthibitisha hilo lakini alisema hakitaukabidhi mikononi mwa polisi.


Alisema hakitafanya hivyo kwa kuwa jeshi hilo ni watuhumiwa wakuu hivyo hawawezi kuwa na dhamira na nia njema katika upelelezi wao. Alisema ndiyo maana badala polisi kuwaona ni msaada, kimeanza kutoa vitisho kwa wote wanaosema waliwashuhudia askari wakishambulia watu kwa risasi kabla ya kuondoka na aliyerusha bomu kwenye gari lao.

“Chadema tuko tayari kukabidhi ushahidi huu kwa tume huru ya uchunguzi ya Mahakama. Rais Kikwete atumie mamlaka yake ya kikatiba kuunda tume kuchunguza tukio la bomu Arusha ili ukweli ujulikane. Polisi ni watuhumiwa katika jambo hili, hivyo hawana dhamira safi na ushahidi wetu,” alisema Mbowe.

Busara Lema na Mbowe kufika kituo cha polisi kuitika mwito
Lema, Mbowe wahujiwa kituo cha polisi kutokana na mkusanyiko wa kuaga miili ya marehemu iliyosababishwa na mlipuko wa bomu kwenye mkutano wa Chadema na kusababisha vifo pamoja na zile zilizofuatia wakati polisi ilipowasambaratisha wafuasi wa chama hicho kwa mabomu walipokusanyika kwenye Viwanja vya Soweto kwa lengo la kutoa heshima za mwisho kwa marehemu.


Wakiongozwa na mawakili watatu, Mbowe na Lema waliwasili polisi saa 3.50 asubuhi na kuhojiwa hadi saa 9.10.
Viongozi hao walipokewa na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha, Diwani Nyanda kabla ya kutenganishwa kwenye vyumba viwili tofauti kwa mahojiano.

Polisi waliwahoja mambo mawili:
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mbowe, Lema na wakili Albert Msando walitaja mambo mawili ambayo polisi waliwahoji kwanza ikiwa ni:


  1. Ushiriki wao katika mkusanyiko usio halali kwenye Viwanja vya Soweto, Jumanne iliyopita ambao ulisambaratishwa na polisi.
  2. Kauli yao ya kuwa na ushahidi unaohusisha polisi na tukio la bomu lililorushwa kwenye mkutano wa Chadema na kusababisha vifo vya watu wanne huku zaidi ya 60 wakijeruhiwa.

Hoja za utetezi Lema na Mbowe dhidi ya shutuma za polisi
Mbowe - Polisi ilituruhusu kuzungumza na wananchi
Mbowe alisema kwa pamoja wamewaeleza polisi kuwa hawaamini kama mkusanyiko wa Jumanne iliyopita haukuwa halali kwa sababu waliruhusiwa kuzungumza na wananchi waliokusanyika ili kuwashawishi watawanyike.


“Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD) wa Arusha, Gilles Mroto ndiye aliyeturuhusu kuzungumza na wananchi wale kuwataka watawanyike na ndicho tulichofanya, lakini tukashangaa kuanza kupigwa mabomu mara baada ya kuwataka watu wanaotaka kutoa heshima za mwisho kwa marehemu kwenda Hospitali ya Mount Meru,” alisema Mbowe.

Alisema Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja kuwa naye aliyewaomba viongozi wa Chadema kuwatawanya wafuasi wa chama hicho baada ya kuzuiwa kutoa heshima za mwisho katika viwanja hivyo vinavyomilikiwa na Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Police waanza kuchanganyikiwa na kutaka ushauri wa kisheria baada ya kuzidiwa hoja ya Mbowe
Akizungumza na waandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema polisi inawasiliana na wanasheria kutafuta ushauri wa hatua za kuchukua... “Polisi ndiyo wenye jukumu la kuchunguza na kukusanya ushahidi wote kuhusiana na matukio ya uhalifu. Hili ni jukumu la kisheria la polisi. Chadema wakabidhi ushahidi wao badala ya kupiga danadana ya kutaka tume huru ya uchunguzi ya kimahakama.”


Alisema hata ikiundwa tume, bado jukumu la kuchunguza na kukusanya ushahidi litarejeshwa mikononi mwa polisi, hivyo Chadema wanapaswa kutimiza wajibu wa kusaidia uchunguzi kwa kuwasilisha ushahidi wao wa polisi kuhusika katika tukio la bomu.


 
Unasemaje mkuu?mbna hueleweki?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Umesoma tu heading bila kuipitia habari yote. Kichwa cha habari hakiwezi kukupatia supu yote vinginevyo kitaaluma nimekunyima haki ya kupitia habari yote kama kichwa cha habari kinakupatia jibu lililokamilika.
 
Huyu muuwaji awe na ushahidi atoe wapi kazi kuuwa watu tu linaroho mbaya kama nini.
 
Lema,+mbowe+Nyerere.jpg

Freeman Mbowe na Lema walipotinga kituo cha polisi

USHAHIDI WA VIDEO KUHUSU SHAMBULIO LA BOMU ARUSHA
Msimamo wa Mbowe - Tume huru ya kimahakama si polisi watuhumiwa
Kuhusu ushahidi anaodai unawahusisha polisi na tukio la bomu, Mbowe alisisitiza kuwa
Chadema kina ushahidi wa kutosha kuthibitisha hilo lakini alisema hakitaukabidhi mikononi mwa polisi.


Alisema hakitafanya hivyo kwa kuwa jeshi hilo ni watuhumiwa wakuu hivyo hawawezi kuwa na dhamira na nia njema katika upelelezi wao. Alisema ndiyo maana badala polisi kuwaona ni msaada, kimeanza kutoa vitisho kwa wote wanaosema waliwashuhudia askari wakishambulia watu kwa risasi kabla ya kuondoka na aliyerusha bomu kwenye gari lao.

"Chadema tuko tayari kukabidhi ushahidi huu kwa tume huru ya uchunguzi ya Mahakama. Rais Kikwete atumie mamlaka yake ya kikatiba kuunda tume kuchunguza tukio la bomu Arusha ili ukweli ujulikane. Polisi ni watuhumiwa katika jambo hili, hivyo hawana dhamira safi na ushahidi wetu," alisema Mbowe.

Busara Lema na Mbowe kufika kituo cha polisi kuitika mwito
Lema, Mbowe wahujiwa kituo cha polisi kutokana na mkusanyiko wa kuaga miili ya marehemu iliyosababishwa na mlipuko wa bomu kwenye mkutano wa Chadema na kusababisha vifo pamoja na zile zilizofuatia wakati polisi ilipowasambaratisha wafuasi wa chama hicho kwa mabomu walipokusanyika kwenye Viwanja vya Soweto kwa lengo la kutoa heshima za mwisho kwa marehemu.


Wakiongozwa na mawakili watatu, Mbowe na Lema waliwasili polisi saa 3.50 asubuhi na kuhojiwa hadi saa 9.10.
Viongozi hao walipokewa na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha, Diwani Nyanda kabla ya kutenganishwa kwenye vyumba viwili tofauti kwa mahojiano.

Polisi waliwahoja mambo mawili:
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mbowe, Lema na wakili Albert Msando walitaja mambo mawili ambayo polisi waliwahoji kwanza ikiwa ni:


  1. Ushiriki wao katika mkusanyiko usio halali kwenye Viwanja vya Soweto, Jumanne iliyopita ambao ulisambaratishwa na polisi.
  2. Kauli yao ya kuwa na ushahidi unaohusisha polisi na tukio la bomu lililorushwa kwenye mkutano wa Chadema na kusababisha vifo vya watu wanne huku zaidi ya 60 wakijeruhiwa.

Hoja za utetezi Lema na Mbowe dhidi ya shutuma za polisi
Mbowe - Polisi ilituruhusu kuzungumza na wananchi
Mbowe alisema kwa pamoja wamewaeleza polisi kuwa hawaamini kama mkusanyiko wa Jumanne iliyopita haukuwa halali kwa sababu waliruhusiwa kuzungumza na wananchi waliokusanyika ili kuwashawishi watawanyike.


"Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD) wa Arusha, Gilles Mroto ndiye aliyeturuhusu kuzungumza na wananchi wale kuwataka watawanyike na ndicho tulichofanya, lakini tukashangaa kuanza kupigwa mabomu mara baada ya kuwataka watu wanaotaka kutoa heshima za mwisho kwa marehemu kwenda Hospitali ya Mount Meru," alisema Mbowe.

Alisema Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja kuwa naye aliyewaomba viongozi wa Chadema kuwatawanya wafuasi wa chama hicho baada ya kuzuiwa kutoa heshima za mwisho katika viwanja hivyo vinavyomilikiwa na Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Police waanza kuchanganyikiwa na kutaka ushauri wa kisheria baada ya kuzidiwa hoja ya Mbowe
Akizungumza na waandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema polisi inawasiliana na wanasheria kutafuta ushauri wa hatua za kuchukua... "Polisi ndiyo wenye jukumu la kuchunguza na kukusanya ushahidi wote kuhusiana na matukio ya uhalifu. Hili ni jukumu la kisheria la polisi. Chadema wakabidhi ushahidi wao badala ya kupiga danadana ya kutaka tume huru ya uchunguzi ya kimahakama."


Alisema hata ikiundwa tume, bado jukumu la kuchunguza na kukusanya ushahidi litarejeshwa mikononi mwa polisi, hivyo Chadema wanapaswa kutimiza wajibu wa kusaidia uchunguzi kwa kuwasilisha ushahidi wao wa polisi kuhusika katika tukio la bomu.


Hawa chadema hawana lolote la maana wawe na ushahidi wautoe mtaa gani.

hivi chadema inaweza kuuwa na kujiandalia ushahidi kweli huku ni kuchezeana akiri.
 
mkuu hamna kutoa huo mkanda kwa policcm ambao ni watuumiwa wakubwa wa tukio la kimafia arusha.
 
Hawa chadema hawana lolote la maana wawe na ushahidi wautoe mtaa gani.

hivi chadema inaweza kuuwa na kujiandalia ushahidi kweli huku ni kuchezeana akiri.

unaongea kitu ambacho ukijui au uko period nini?punguza upimbi kwenye mambo ya msingi.
 
Lema,+mbowe+Nyerere.jpg


USHAHIDI WA VIDEO KUHUSU SHAMBULIO LA BOMU ARUSHA
Msimamo wa Mbowe - Tume huru ya kimahakama si polisi watuhumiwa
Kuhusu ushahidi anaodai unawahusisha polisi na tukio la bomu, Mbowe alisisitiza kuwa
Chadema kina ushahidi wa kutosha kuthibitisha hilo lakini alisema hakitaukabidhi mikononi mwa polisi.


Alisema hakitafanya hivyo kwa kuwa jeshi hilo ni watuhumiwa wakuu hivyo hawawezi kuwa na dhamira na nia njema katika upelelezi wao. Alisema ndiyo maana badala polisi kuwaona ni msaada, kimeanza kutoa vitisho kwa wote wanaosema waliwashuhudia askari wakishambulia watu kwa risasi kabla ya kuondoka na aliyerusha bomu kwenye gari lao.

“Chadema tuko tayari kukabidhi ushahidi huu kwa tume huru ya uchunguzi ya Mahakama. Rais Kikwete atumie mamlaka yake ya kikatiba kuunda tume kuchunguza tukio la bomu Arusha ili ukweli ujulikane. Polisi ni watuhumiwa katika jambo hili, hivyo hawana dhamira safi na ushahidi wetu,” alisema Mbowe.


Yale yale ya Bw.Zito Kabwe, nina Majina ya walioweka Fedha Uswisi na Serikali isipowataja nitapeleka Majina yao kwenye Mahakama ya Wananchi yaani nitawataja kwa majina mmoja baada ya mwingine, siku zikapita hadithi ikabadilika ikawa hata tukiwataja ni nini kitabadilika basi bora tusiwataje, lkn mwanzoni aliahidi kuwataja!

Ndio kama huyu Bw.Mbowe yeye anaoushahidi kama Polisi ndio walihusika basi autoe, atoe hata kopi tuuone na Polisi nao wauone, kwa nini anasita, anasema mpaka kuwe na Mahakama huru, hapo kuna mtego, kwa mfumo wa TZ ulivyo hakuna taasisi ambayo iko huru kwa 100% kwamba haihusiki na Serikali, hivyo danadana zitaanzia hapo, na hakuna cha ushahidi wala nini, hawa jamaa wote baba mmoja mama mmoja, PUCK THEM!

 
Polisi ya Tanzania inaongozwa na watu wa ajabu sana kama kweli unataka ukweli ujulikane kwanini unapiga tume huru ya majaji?? kwanini unaghaghania upewe ushahidi wewe huku ukiwa umetajwa kuhusika na tukio zima ??
 
uhuru_e92c0.jpg


Mahama ya kimataifa ya ICC imeakhirisha siku ya kuanza kusikilizwa kwa kesi dhidi ya rais Uhuru Kenyatta hadi tarehe 12 mwezi Novemba mwaka huu. Hii ni kufuatia ombi la mawakili wa Rais Kenyatta kutaka kesi yao kuahirishwa hadi mwezi Januari mwaka ujao. Mahakama iliamua kuwa upande wa Kenyatta unahitaji muda wa ziada ili kujiandaa ipasavyo kwa kesi, kwa sababu viongozi wa mashtaka walichelewa kufichua ushahidi walio nao dhidi ya rais Kenyatta. Kenyatta anakabiliwa na tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadmau wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya miaka sita iliyopita, akisemekana kuunga mkono mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya watu wa kabila moja.

Naibu Rais wa Kenya William Ruto naye pia anakabiliwa na kesi katika mahakama ya ICC kuhusu tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu kwa kupanga mashambulizi dhidi ya jamii hasimu. Majaji waliwaalika mawakili wa Uhuru Kenyatta kutoa maoni yao kuhusu muda wanaotaka ili kujiandaa kwa kesi dhidi ya mteja wao.
Baada ya kupokea maoni kutoka kwa upande wa utetezi, upande wa mashtaka, pamoja na waakilishi wa kisheria, majaji waliamua kuakhirisha kesi hiyo kutoka tarehe 9 Julai mwaka huu hadi Novemba. Tarahe hiyo mpya ilifikiwa baada ya kuzingatia maswala mbali mbali ikiwemo haja ya upande wa mashtaka kujiandaa vyema kwa utetezi wao na mipango ya usafiri.
Rais Kenyatta ameshtakiwa kwa kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi wa Kenya , makosa ya jinai ikiwemo, mauaji, kuwahamisha watu kinyume na sheria, ubakaji , mateso na vitendi vingine vya kinyama vinavyodaiwa kufanywa wakati wa ghasia hizo mwaka 2007/2008.


Ndege mjanja hunasa kwenye tundu bovu. Mtakwepakwepa lakini sheria hazikwepiki hata ukizichepusha kwa njia ye yote zitawafuata na ipo siku mtajutia mnayoyafanya leo.

Kumbuka unaweza kulazimisha mto kuhamisha toka kwenye mkondo wake, lakini kesho utashtukia maji yamebomoa kinga ile na kufuata mkondo wake wa asili.

Cheo si kinga ya kufanya utakacho hata kuvunja sheria. Leo hii Kenyatta kama alifikiria kuukwaa urais ni kinga, kinachoendelea ni sasa kusimama kizimbani kwenyte mahakama ya kimataifa hapa Arusha.
 
Polisi ya Tanzania inaongozwa na watu wa ajabu sana kama kweli unataka ukweli ujulikane kwanini unapiga tume huru ya majaji?? kwanini unaghaghania upewe ushahidi wewe huku ukiwa umetajwa kuhusika na tukio zima ??

System yote serikalini ni hovyo hovyo kabisa, umesikia Pinda alivyopindisha sheria za nchi na katiba bungeni kwa kuwapa mamlaka za mahakama polisi kinyume cha sheria. Polisi wanapewa na Pinda mamlaka za mahakama za kuadhibu kisheria. Serikali na vyombo vyake vyote vimepinda kama Pinda.
 
Yale yale ya Bw.Zito Kabwe, nina Majina ya walioweka Fedha Uswisi na Serikali isipowataja nitapeleka Majina yao kwenye Mahakama ya Wananchi yaani nitawataja kwa majina mmoja baada ya mwingine, siku zikapita hadithi ikabadilika ikawa hata tukiwataja ni nini kitabadilika basi bora tusiwataje, lkn mwanzoni aliahidi kuwataja!

Ndio kama huyu Bw.Mbowe yeye anaoushahidi kama Polisi ndio walihusika basi autoe, atoe hata kopi tuuone na Polisi nao wauone, kwa nini anasita, anasema mpaka kuwe na Mahakama huru, hapo kuna mtego, kwa mfumo wa TZ ulivyo hakuna taasisi ambayo iko huru kwa 100% kwamba haihusiki na Serikali, hivyo danadana zitaanzia hapo, na hakuna cha ushahidi wala nini, hawa jamaa wote baba mmoja mama mmoja, PUCK THEM!

hujui unachoongea unaitaji crash course civics kwa ufupi ni kwamba Rais hana uwezo wa ku control tume itayoundwa na majaji kwani imetamkwa kwenye katiba kumbuka rais hana uwezo wa kufukuza kazi majaji hao kwahiyo hawana sababu yeyote ya kumuogopa na ndio maana kama umefuatilia matukio mengi rais anapoombwa kuunda tume hiyo ili ukweli ujulikane huwa anakwepa na matokeo yake anawaambia watu kama nchimbi waunde kamati kwa sababu anajua ni rahisi kuwa control watu wa kwenye kamati kwa sababu hazina nguvu kikatiba.
 
Hayo maneno ya mkosaji,SASA IVI NI MWENDO WA KUPIGA TU,PIGA 2,
Na lazima wanyooke
watu wote wenye akili hawaongei hivyo. Ulimuona jana RPC wa Arusha alivyoongea kwa huzuni kutoka na kashfa hii. Hebu jaribu kufikiri kwa undani kidogo sio kiushabiki wa kisiasa, Wananchi wamebigwa kwa bomu. Watu wenye silaha hapo mkutanoni ni polisi, kisha wanaamua kuwapiga risasi wananchi, hii inaleta maswali mengi kuliko majibu yaliyotolewa. Hivi kweli ww inakuingia akilini eti walikuwa provoked, nani aliwaprovoke, bomu liliwaprovoke?

FIKIRI KABLA HUJAPOST, HAPA UNAMEET NA GT
 
["Chadema tuko tayari kukabidhi ushahidi huu kwa tume huru ya uchunguzi ya Mahakama. Rais Kikwete atumie mamlaka yake ya kikatiba kuunda tume kuchunguza tukio la bomu Arusha ili ukweli ujulikane. Polisi ni watuhumiwa katika jambo hili, hivyo hawana dhamira safi na ushahidi wetu," alisema Mbowe.
/QUOTE]

NDIO,polisi ni watuhumiwa,mwambie apeleka ushahidi huo pale unapoona utafanyiwa kazi,
Nyie ndo mnasema kuunda tume ni kupoteza fedha za walipakodi sa iweje leo mtake tume ya kimahakama?
Umepewa ushauri mzuri peleka ushahidi kwa RAISI WAKO,ambaye unataka aunde tume,pia itasaidia kupunguza upotevu wa kodi kwa kulipa iyo tume,

Mbowe kama anaipenda tanzania toa uo ushahidi ili ccm na serikali yake iumbuke
 
watu wote wenye akili hawaongei hivyo. Ulimuona jana RPC wa Arusha alivyoongea kwa huzuni kutoka na kashfa hii. Hebu jaribu kufikiri kwa undani kidogo sio kiushabiki wa kisiasa, Wananchi wamebigwa kwa bomu. Watu wenye silaha hapo mkutanoni ni polisi, kisha wanaamua kuwapiga risasi wananchi, hii inaleta maswali mengi kuliko majibu yaliyotolewa. Hivi kweli ww inakuingia akilini eti walikuwa provoked, nani aliwaprovoke, bomu liliwaprovoke?

FIKIRI KABLA HUJAPOST, HAPA UNAMEET NA GT

Fikiri kwanza wew ndo ujibu nilichopost
Na sipo kisiasa mkuu
NDIO,polisi ni watuhumiwa,mwambie apeleka ushahidi huo pale unapoona utafanyiwa kazi,
Nyie ndo mnasema kuunda tume ni kupoteza fedha za walipakodi sa iweje leo mtake tume ya kimahakama?
Umepewa ushauri mzuri peleka ushahidi kwa RAISI WAKO,ambaye unataka aunde tume,pia itasaidia kupunguza upotevu wa kodi kwa kulipa iyo tume,

Mbowe kama anaipenda tanzania toa uo ushahidi ili ccm na serikali yake iumbuke
 
Back
Top Bottom