Kufuatia kusambaa mtandanoni kwa clip ya sauti inayodhaniwa kuwa ya Steve Nyerere akizungumza na Mama yake msanii Wema Sepetu, utata umeibuka mara baada ya kuwepo taarifa kuwa Steve Nyerere amedakwa na polisi kwa mahojiano maalumu.
Akizungumza leo na wanahabari, Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam Kamishna Sirro amesema yeye hajamuita Steve Nyerere lakini huenda akawa ameitwa na maafisa wake wa upelelezi kwa ajili ya mahojiano, jambo ambalo ni sahihi.
Sirro amesema kuna kikosi maalum alichokipa kazi hiyo ya kumkamata na kumhoji Steve Nyerere na endapo msanii huyo anahojiwa ataweza kuachiwa kama kikosi hicho kitajiridhisha kuwa anastahili dhama, lakini kama kitaona bado kinamuhitaji, kitaendelea kumshikilia.
Msanii huyo ameingia kwenye kadhia hiyo baada ya kusambaa kwa sauti zinazodaiwa kuwa ni mazungumzo kati yake na Mama wa Msanii Wema Sepetu, kuhusu sakata la dawa za kulevya linalomkabili Wema Sepetu.
Source: Eatv