Mbowe ni wa kumuonea huruma tu!

Mbowe ni wa kumuonea huruma tu!

Upinzani na jela ni ndugu moja, ukiwa mpinzani na ukawa muoga wa jela bado hujawa mpinzani, wakina Mandela walikaa jela sana, wakina Haji Juma Duni, wakina Maalim Seif, walikaa jela sana sana.
 
mahakama imeamua kumkomesha mbowe kwa kuidharau...dharau vyote lakini sio mahakama,ngoja aendelee kupigwa pin huko
 
Kwa ku-declare interest, binafsi sijawahi kukubali siasa za huyu mheshimiwa tangu dunia ianze, ila kwa udhaifu wa kibinadamu, kiukweli kabisa ningependa kum-favor na kuona akiachiliwa huru tu!

Naamini amejifunza sana sasa na ataweza kutofautisha kati ya siasa na sheria (ambazo kazitunga mwenyewe). Kujua pia ni ipi kati ya habari 100 za Mange ya kuichukua (Kama ipo).
Naamini pia ataweza kutambua japo kwa kuchelewa kuwa utawala umebadilika kweli na kuona kuwa yeye mwenyewe anatakiwa kubadilika kulingana na hali, maana utawala wa mazowea umepita.

Atatambua kuwa Tanzania kama nchi tulipoamua kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano tulitaka kubadilisha flavour, mambo yasiwe yale yale kila siku eti. Ni bahati nzuri ngalau kwa mara ya kwanza sasa kama nchi tunamaanisha.

Hapa nakumbuka enzi za JK yeye na wenzake walikuwa wanaitisha maandamano kadri wanavyojisikia bila hata kufuata taratibu, watu wanakufa na wengine wanapata vilema vya kudumu, lakini nani alijali? Just the next morning JK anawaita Ikulu kwenda kugonga glass, hapo hapo jioni yake tena wanamtukana matusi yote ndani na nje ya bunge pamoja na kumwita dhaifu. Mwenyewe anacheka tu, hana habari! Sana sana atasafiri siku mbili tatu nje ya nchi kidiplomasia hata kukwepa harufu ya samaki pale Feri.

Walikuwa serikali kivuli na nusu hasa ambapo serikali halisi ilikuwa mbili. Mheshimiwa ana msongo mkubwa wa mawazo kwa mambo mengi ndani ya chama yanavyokwenda hovyo na msongo wa mwili kwa kukaa mahabusu muda mrefu mpaka sasa, obvious, halafu ongeza na la ENL! Karibia kila kitu kimebadilika ndani ya miaka mitatu.

Daah! Binafsi natamani, pengine hata #1 angetamani kuona anatoka. Lakini ndiyo tunafanyaje sasa na nchi yetu ni ya kidemokrasia, tumechagua kufuata utawala wa sheria? Itakavyoamua mahakama ni sawa, ama siyo sawa kwa kukata rufaa, kwao ama kwa serikali. Ni pole tu kwa kweli! Hilo lipo ndani ya uwezo wangu, nalimudu.

Nawasilisha, Tindikali
View attachment 1039905
View attachment 1039907
View attachment 1039816
Wakuonea huruma ni babaako aliye kuzaa ukiwa na mtindio

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naunga mkono hoja yako mkuu!... Nikiangalia picha ya Mbowe iliyopigwa jana kama binadamu nasikitishwa sana na hali yake kwa sasa... Lakina najiuliza, Hivi ilikuwa lazima kufika hatua ya kujiapiza katika kufanya siasa?... Kweli mkataa pema, pabaya panamgoja. Natumaini akifanikiwa kutoka atajirekebisha.. Inshaalah!
 

Attachments

  • Screenshot_2019-03-07 Mbowe ni wa kumuonea huruma tu - JamiiForums.png
    Screenshot_2019-03-07 Mbowe ni wa kumuonea huruma tu - JamiiForums.png
    143.6 KB · Views: 16
Wasioweza kijibu hoja zake nzito bungeni wanapata afueni akiwa ndani.
Kwa ku-declare interest, binafsi sijawahi kukubali siasa za huyu mheshimiwa tangu dunia ianze, ila kwa udhaifu wa kibinadamu, kiukweli kabisa ningependa kum-favor na kuona akiachiliwa huru tu!

Naamini amejifunza sana sasa na ataweza kutofautisha kati ya siasa na sheria (ambazo kazitunga mwenyewe). Kujua pia ni ipi kati ya habari 100 za Mange ya kuichukua (Kama ipo).
Naamini pia ataweza kutambua japo kwa kuchelewa kuwa utawala umebadilika kweli na kuona kuwa yeye mwenyewe anatakiwa kubadilika kulingana na hali, maana utawala wa mazowea umepita.

Atatambua kuwa Tanzania kama nchi tulipoamua kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano tulitaka kubadilisha flavour, mambo yasiwe yale yale kila siku eti. Ni bahati nzuri ngalau kwa mara ya kwanza sasa kama nchi tunamaanisha.

Hapa nakumbuka enzi za JK yeye na wenzake walikuwa wanaitisha maandamano kadri wanavyojisikia bila hata kufuata taratibu, watu wanakufa na wengine wanapata vilema vya kudumu, lakini nani alijali? Just the next morning JK anawaita Ikulu kwenda kugonga glass, hapo hapo jioni yake tena wanamtukana matusi yote ndani na nje ya bunge pamoja na kumwita dhaifu. Mwenyewe anacheka tu, hana habari! Sana sana atasafiri siku mbili tatu nje ya nchi kidiplomasia hata kukwepa harufu ya samaki pale Feri.

Walikuwa serikali kivuli na nusu hasa ambapo serikali halisi ilikuwa mbili. Mheshimiwa ana msongo mkubwa wa mawazo kwa mambo mengi ndani ya chama yanavyokwenda hovyo na msongo wa mwili kwa kukaa mahabusu muda mrefu mpaka sasa, obvious, halafu ongeza na la ENL! Karibia kila kitu kimebadilika ndani ya miaka mitatu.

Daah! Binafsi natamani, pengine hata #1 angetamani kuona anatoka. Lakini ndiyo tunafanyaje sasa na nchi yetu ni ya kidemokrasia, tumechagua kufuata utawala wa sheria? Itakavyoamua mahakama ni sawa, ama siyo sawa kwa kukata rufaa, kwao ama kwa serikali. Ni pole tu kwa kweli! Hilo lipo ndani ya uwezo wangu, nalimudu.

Nawasilisha, Tindikali
View attachment 1039905
View attachment 1039907
View attachment 1039816

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kawaida unapomnyanyasa mtu, unapomtesa mtu, kwa kumwonea, ni yeye anayefaidika na hayo mateso. Ni kweli anateseka, kama alivyosema Tundu Lissu, kwamba kulala rumande siyo picnic, kuna mateso kule, lakini akaongeza kusema HAOGOPI. Kitu ambacho wakandamizaji kote duniani huwa wagumu kuelewa ni jinsi unavyoimarisha wapinzani wako kwa kuwatesa.

Tuelewane kwamba hapa siyo suala la sheria za nchi, bali ni suala la ukandamizaji, uminywaji wa haki wa makusudi ili kutekeleza malengo mahsusi. Sheria zinazotumiwa dhidi ya wapinzani zilitungwa na MKOLONI. Na mwathirika wa kwanza alikuwa ni NYERERE. lakini pia kuna sheria zinazopitishwa hivi sasa kwa kutumia wingi wa wabunge wa CCM, sheria kandaminzi. Hii ni nchi inayofuata DEMOKRASIA YA VYAMA VINGI, ambapo chama kilichoko madarakani, badala ya kufuata kanuni halali za mchezo kinatumia nafasi hiyo kuhakikisha kwamba kinaendelea kubaki hapo siyo kwa sanduku la kura bali kwa NGUVU YA DOLA.

Magufuli anadhoofisha vyombo vilivyoko kwenye mfumo ambavyo vinamdhibiti yeye na serikali yake. Mifano michache:
1)Tume ya Haki za binadamu na utawala bora, haina uongozi woote wa juu: Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mtendaji, Wakurugenzi wote, Makamishna wote. wamekuwa wakistaafu na hakuna wanaoteuliwa. na kwa sheria ya tume hiyo, haiwezi kufanya chochote kwa sasa. Haina meno.
2)CAG - amepunguziwa bajeti, anaandamwa na kukejeliwa na serikali kwa njia mbalimbali, mfano kupitia Spika Ndugai hivi karibuni.
3) Mahakama - Jaji mkuu anaporwa madaraka yake na Rais na anaruhusu hiyo, mahakimu wengi na majaji wamenunuliwa
4)Bunge - limenyonyolewa manyoya yoooote, sasa hivi ni kipaza sauti tu cha Magufuli

Sasa basi, asichoelewa Magufuli, huko "KUOZEA MAGEREZANI" kwa wapinzani alosema siku anafungua maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alipomsifu Lowasa kwa kuhudhuria hafla hiyo, ni KUIVA MAGEREZANI, na siyo KUOZA. Ila Magufuli ndiyo ANAOZA kwa kuwafunga wapinzani BILA MAKOSA.

Mbowe anakomazwa katika kupigania haki. hatutarajii ataogopa, bali atakuwa imara zaidi. Tundu Lissu alipopigwa risasi, wengi walitarajia kwamba sasa atakaa kimya. Lakini ndio wamemwongezea nguvu zakuisema zaidi serikali KANDAMIZI ya Magufuli. Magufuli anaujenga zaidi upinzani, hata pale anapowahonga wapinzani kuja CCM, anaimarisha upinzani kwa kuwaondoa wapenda fedha na mafisadi na kuwajaza CCM. kwa wenye akili, hilo wala si jambo la kushangilia. wanaoshangilia ujinga huo NI AKILI MATOPE
 
Labda nikuulize..taaluma yako ni nini..umesomea sheria au ndio nyie wa division five unajifanya unajua kila kitu..

Uniulizie kama nani..? Kuwa na adabu Bwana Mdogo, ni vizuri wakati mwingine ukaficha upumbavu wako.
 
Back
Top Bottom