Mbowe ni wa kumuonea huruma tu!

Mbowe ni wa kumuonea huruma tu!

Kwa ku-declare interest, binafsi sijawahi kukubali siasa za huyu mheshimiwa tangu dunia ianze, ila kwa udhaifu wa kibinadamu, kiukweli kabisa ningependa kum-favor na kuona akiachiliwa huru tu!

Naamini amejifunza sana sasa na ataweza kutofautisha kati ya siasa na sheria (ambazo kazitunga mwenyewe). Kujua pia ni ipi kati ya habari 100 za Mange ya kuichukua (Kama ipo).
Naamini pia ataweza kutambua japo kwa kuchelewa kuwa utawala umebadilika kweli na kuona kuwa yeye mwenyewe anatakiwa kubadilika kulingana na hali, maana utawala wa mazowea umepita.

Atatambua kuwa Tanzania kama nchi tulipoamua kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano tulitaka kubadilisha flavour, mambo yasiwe yale yale kila siku eti. Ni bahati nzuri ngalau kwa mara ya kwanza sasa kama nchi tunamaanisha.

Hapa nakumbuka enzi za JK yeye na wenzake walikuwa wanaitisha maandamano kadri wanavyojisikia bila hata kufuata taratibu, watu wanakufa na wengine wanapata vilema vya kudumu, lakini nani alijali? Just the next morning JK anawaita Ikulu kwenda kugonga glass, hapo hapo jioni yake tena wanamtukana matusi yote ndani na nje ya bunge pamoja na kumwita dhaifu. Mwenyewe anacheka tu, hana habari! Sana sana atasafiri siku mbili tatu nje ya nchi kidiplomasia hata kukwepa harufu ya samaki pale Feri.

Walikuwa serikali kivuli na nusu hasa ambapo serikali halisi ilikuwa mbili. Mheshimiwa ana msongo mkubwa wa mawazo kwa mambo mengi ndani ya chama yanavyokwenda hovyo na msongo wa mwili kwa kukaa mahabusu muda mrefu mpaka sasa, obvious, halafu ongeza na la ENL! Karibia kila kitu kimebadilika ndani ya miaka mitatu.

Daah! Binafsi natamani, pengine hata #1 angetamani kuona anatoka. Lakini ndiyo tunafanyaje sasa na nchi yetu ni ya kidemokrasia, tumechagua kufuata utawala wa sheria? Itakavyoamua mahakama ni sawa, ama siyo sawa kwa kukata rufaa, kwao ama kwa serikali. Ni pole tu kwa kweli! Hilo lipo ndani ya uwezo wangu, nalimudu.

Nawasilisha, Tindikali
View attachment 1039905
View attachment 1039907
View attachment 1039816
Hawa jamaa sio kwamba hawajitambui ila wanafanya kusudi. Wenyewe wanachotaka nikuingia ikulu, sasa hawajui njia za kuingilia ikulu matokeo yake wanatapatapa na kuleta kick zao zisizokuwa na mashiko. Yetu macho ila watambue kwa kuongoza nchi mbowe atambue huko kwao badoooo sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe hujielewi na umeandika kwa kufuata mihemuko, hivi ni nani mtu wa kwanza hapa nchini anayetakiwa kuonyesha njia ya kutii sheria?!,

(1) Hujui kufanya mikutano ya kisiasa ni haki ya kikatiba ya vyama vya siasa !?
(2) Hujui kuandamana ni njia moja ya kikatiba kudai haki?!
(3)Hujui kwamba hakuna mtu yeyote aliyejuu ya sheria--- licha ya wadhifa wake?!--- polisi wameelekezwa kuua ili wapandishwe vyeo.
(4) Hujui mtuhumiwa yeyote anatakiwa kwanza apelekwe mahakamani ili ajitetee ?! -- kuliko kutoa amri zinazo kiuka haki za kinadamu.
(5) Hujui kiongozi ni lazima aongozwe na katiba HEKIMA na BUSARA wala siyo jazba??
(6) Hujui kiongozi hatakiwi kutukana na kudharau watu??
(7) Hujui kiongozi hatakiwi awe na upendeleo wa sina yeyote??
(8) Hujui kiongozi anatakiwa alinde ulimi wake katika kila anachoongea??
(9) Hujui kiongozi ni yule anayepeleka maendeleo yanayojali kwanza hadhi ya utu na siyo yanayojali hadhi ya vitu??.
(10) Hujui hii nchi ni ya Watz wote na haimilikiwi na mtu au watu fulani au chama fulani??
(11) Hujui kila mtu anayohaki ya kutoa maoni yake bila hofu kwa mustakbali wa nchi bila kuvunja sheria?? (Freedom of expression )
Kweli kabisa, leo nimeyajua yote na nitaacha kuandika kwa kufuata mihemko
 
Chanzo ni maandamano yasiyofuata taratibu, yale yale ambayo kwa miaka ya nyuma ilikuwa poa tu!
Safari hii kafa mmoja na wamekomaliwa hatari
Demonstrations is not a crime...katiba inaruhusu. Mbowe ameonewa ila iko siku watalipa kisasi
 
Mbowe angekutana na wewe angekupa ushauri kama wa Yesu masiha alipowaona akina mama wakimlilia katika mateso yake. Acha kumlilia Mbowe, walilie watanzania wasiojua kuhusu kesho yao.
 
msitishe watu kwa kutumia magereza nyie....Mbowe ni mwendo mdundo!!
 
Chanzo ni maandamano yasiyofuata taratibu, yale yale ambayo kwa miaka ya nyuma ilikuwa poa tu!
Safari hii kafa mmoja na wamekomaliwa hatari

Kwa taarifa yako Mbowe hahitaji huruma ya mahakama wala ya rais bali anahitaji kutendewa haki na sheria za nchi kufuatwa. Kwenye uzi wako namba moja unachokionyesha sio sheria kufuatwa bali ni jinsi gani rais huyu na aliyepita wanatofautiana, japo sio kwenye kufuata sheria bali matumizi mabaya ya madaraka.
 
Chanzo ni maandamano yasiyofuata taratibu, yale yale ambayo kwa miaka ya nyuma ilikuwa poa tu!
Safari hii kafa mmoja na wamekomaliwa hatari

Kwahiyo ulitarajia wapewe ruhusa kuandamana kusema kwamba msimamizi wa uchaguzi kakwepa kuwaapisha mawakala wa cdm? Unatarajia hao wasimamizi wa uchaguzi waliokuwa wanakiuka kuwaapisha mawakala wa cdm na kugoma kupokea fomu za wagombea hawakuwa wanafuata maagizo ya Rais? Kwa sasa rais ndio anayeamua sheria zitekelezwe vipi, ila viburi vya hivyo ni vya muda tu.
 
Kwa taarifa yako Mbowe hahitaji huruma ya mahakama wala ya rais bali anahitaji kutendewa haki na sheria za nchi kufuatwa. Kwenye uzi wako namba moja unachokionyesha sio sheria kufuatwa bali ni jinsi gani rais huyu na aliyepita wanatofautiana, japo sio kwenye kufuata sheria bali matumizi mabaya ya madaraka.
Anayekiuka masharti ya dhamana anafutiwa dhamana, hiyo ndiyo haki
 
Anayekiuka masharti ya dhamana anafutiwa dhamana, hiyo ndiyo haki

Inaonekana sheria kwako inaanza kutekelezeka pale rais anapopata mpenyo wa kuitumia mahakama kuwakomoa wapinzani wake. Huna chochote unachoangalia kuhusu mwenendo mzima wa uchaguzi na ukiukwaji mkubwa wa sheria uliotokea wakati wa uchaguzi. Ndio maana nakuambia kinachofanyika sasa sio utekelezaji wa sheria, bali ni jinsi gani rais anaweza kuzitumia mahakama kufanya atakacho.
 
TANZANIA ni nchi huru

ukiishaitangaza kidunia, then inakuwaje?

mbona hao USA au UK hawajamtoa?

mtu anaumia ndanj mnaleta upuuzi, ndio maana, JPM anataka akili ike kichwani kwanza
Yeye huyo jpm akili anayo kichwani mpaka aweke ya wengine?
 
Na huoni hata inchi moja nyuma ya hilo "tabasamu" daah!
Wewe ndiyo mfano halisi wa aina ya watu anaowaongoza, nyumbu at it's purest form. Ni wa kumuonea huruma zaidi kwa kweli

Haihitaji huruma toka kwa shoga yoyote, hiyo ni changamoto ya kazi yake.
 
Kwa ku-declare interest, binafsi sijawahi kukubali siasa za huyu mheshimiwa tangu dunia ianze, ila kwa udhaifu wa kibinadamu, kiukweli kabisa ningependa kum-favor na kuona akiachiliwa huru tu!

Naamini amejifunza sana sasa na ataweza kutofautisha kati ya siasa na sheria (ambazo kazitunga mwenyewe). Kujua pia ni ipi kati ya habari 100 za Mange ya kuichukua (Kama ipo).
Naamini pia ataweza kutambua japo kwa kuchelewa kuwa utawala umebadilika kweli na kuona kuwa yeye mwenyewe anatakiwa kubadilika kulingana na hali, maana utawala wa mazowea umepita.

Atatambua kuwa Tanzania kama nchi tulipoamua kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano tulitaka kubadilisha flavour, mambo yasiwe yale yale kila siku eti. Ni bahati nzuri ngalau kwa mara ya kwanza sasa kama nchi tunamaanisha.

Hapa nakumbuka enzi za JK yeye na wenzake walikuwa wanaitisha maandamano kadri wanavyojisikia bila hata kufuata taratibu, watu wanakufa na wengine wanapata vilema vya kudumu, lakini nani alijali? Just the next morning JK anawaita Ikulu kwenda kugonga glass, hapo hapo jioni yake tena wanamtukana matusi yote ndani na nje ya bunge pamoja na kumwita dhaifu. Mwenyewe anacheka tu, hana habari! Sana sana atasafiri siku mbili tatu nje ya nchi kidiplomasia hata kukwepa harufu ya samaki pale Feri.

Walikuwa serikali kivuli na nusu hasa ambapo serikali halisi ilikuwa mbili. Mheshimiwa ana msongo mkubwa wa mawazo kwa mambo mengi ndani ya chama yanavyokwenda hovyo na msongo wa mwili kwa kukaa mahabusu muda mrefu mpaka sasa, obvious, halafu ongeza na la ENL! Karibia kila kitu kimebadilika ndani ya miaka mitatu.

Daah! Binafsi natamani, pengine hata #1 angetamani kuona anatoka. Lakini ndiyo tunafanyaje sasa na nchi yetu ni ya kidemokrasia, tumechagua kufuata utawala wa sheria? Itakavyoamua mahakama ni sawa, ama siyo sawa kwa kukata rufaa, kwao ama kwa serikali. Ni pole tu kwa kweli! Hilo lipo ndani ya uwezo wangu, nalimudu.

Nawasilisha, Tindikali
View attachment 1039905
View attachment 1039907
View attachment 1039816
Ile chai watu walikunywa Ikulu sijui ilikuwa na nini ile.
Watu walitoka wapolee...wameitupa katiba mpya na tume mpya ya uchaguzi [emoji16][emoji16]
 
Inaonekana sheria kwako inaanza kutekelezeka pale rais anapopata mpenyo wa kuitumia mahakama kuwakomoa wapinzani wake. Huna chochote unachoangalia kuhusu mwenendo mzima wa uchaguzi na ukiukwaji mkubwa wa sheria uliotokea wakati wa uchaguzi. Ndio maana nakuambia kinachofanyika sasa sio utekelezaji wa sheria, bali ni jinsi gani rais anaweza kuzitumia mahakama kufanya atakacho.
Kwa sheria unazozijua wewe mtu akikiuka masharti ya dhamana anatakiwa kupelekwa Club Bilicanas kula bata siyo?
 
Chanzo ni maandamano yasiyofuata taratibu, yale yale ambayo kwa miaka ya nyuma ilikuwa poa tu!
Safari hii kafa mmoja na wamekomaliwa hatari


Huo ni uchambuzi finyu mno na wa upendeleo (biased).

Chambua hivi:-

(1) Kwanini waandamane?!
Waliandamana baada ya kutokusikilizwa kwa haki zao wakizozadai katika ule uchaguzi wa kinondoni/ kutokusikilizwa na mkurugenzi wa uchaguzi na waliandamana kwa kufuata haki ya kikatiba kudai madai yao yasikilizwe na watekelezewe na hii ni baada ya njia za kawaida kushindikana.
(2) Kuzuiwa kwa maandamano kwa mtutu wa bunduki "kuua" watu wasiokuwa na silaha walioandamana kisheria.
(3) Polisi wakafyatua risasi kuua watu walioandamana kikatiba na risasi ikampiga raia ambaye hakuwemo katika maandamano.


Ukianzia na hayo maelezo toka mwanzo, Sasa sema kwa HAKI ni nani alaumiwe??.
 
Back
Top Bottom