Mbowe ndiye tatizo CHADEMA

There are currently 57 users browsing this thread. (18 members and 39 guests)
hao wasomi hapo kwenye Red si watoe maoni yao kuhusu hii thread?nimewaona hapo muda wote.wana maslahi gani na haya yaliyoandikwa mbona hawakitetei chama kama sisi? wanachekelea tu haya yaliyoandikwa kwa sababu yanawasaidia yanawabeba kiaina.toeni maoni yenu kuhusu hili

Watu wa aina yako ni fedhea kwa chama, huwezi kuwasema watu kwa lugha zenye upoyoyo kiasi hicho.
Unaowasema wako huru kwa majina yao, na wewe uko nyuma ya jina kivuli.

Sijaelewa uwezo wako wa kujiamini mpaka unaejiia mbunge uogope na ufiche jina/ naamini ukiwa mbunge, una uwezo wa kuongea kiundani mambo ya chama, sasa kwa nini unajificha kwa jina kivuli?

Tafadhali usihalalishe makundi ndani ya cdm kwa upayukaji wako huu.

Kama upo kwa kutengeneza makundi, basi uwe wazi pia, wapo watakao kuunga mkono.

Unasababisha viti maalumu wenzio wanadharauliwa kwa namna unavyojiweka kiheroro kwa hoja za makundi.
Nimeona umeandika kuwa wewe ni mbunge, ndio sababu nakunanga uache uzindakoti.
 
Mbowe ndiye tatizo kwa cdm, mnaona jamaa anavyowamaliza wanaompinga, eti kisa anataka aendelee kufanya biashara ndani ya cdm, mnakumbuka magari yake analazimisha atuuzie, anawaondoa wote wanaomkosoa, anawatumia watu tu, wakishamfanikisha anawatupa kama cond..m,huyu jamaa hafai nasikia anataka kuggombea urais ndio maana anafanya mbwmbwe sana na kuwahujumu wenzake,mbowe huna sifa ya kuwa rais wa nchi hii, hata moshi mjini unayotaka ukagombee ubunge utaabika kabisa.

Unataka ww uwe juu tu kuliko wengine na huna uimara wa kufikiri, kumbuka ulivyoropoka kwenye bajeti baada ya kikao cha bunge, sikia ulivyoropoka kuhusu madiwani arusha, halafu leo unakuja na ujinga wa kuwakana, nimeongea na wanachama wengi sana wamenipa huu ujumbe nikupe, kama ukimeza wembe umezs tu, hasa huku visiwani hutakiwi kuja kabisa shaurilo ukijipendekeza utaokona.
haya kwa uchaguzi wa cdm 2013 labda uuairishe eti, vinginevyo utaanguka na utashangaa.

Tunamkumbuka chacha wangwe sana, tunammis sana msema ukweli wetu sie, kwa nini unagombana na kila mtume ajaye cdm akiwa hakubaliani na wewe mbaba? wewe ni tatizo.
1. alitaka kuuzia wewe na nani?
2. vp alikutupa na wewe kama condom?
3. vp na wewe unataka kugombea huo urais?
4. hiyo ya kumeza wembe sound like mipasho, vp unimbia bend gani ya tarab? kakae na wambea wako mmeze nyembe vizuri
 
sisi wenye chama tunakukemea ushindwe mfululizo, hata mje mia moja hamtatuyumbisha, bila shaka utakuwa ni mmoja wa waliokatwa katika uchaguzi. Nenda kwenye chama chenu mkajivue magamba.

Hey bro, what hell are u talking? please usitake kutuingiza kwenye mabishano yenu.
Nawaomba sana muepuke kuingizwa kwenye mitego inayowapima na kuwagundua udhaifu wenu.
Sasa hapo sisi tulioenguliwa bavicha unataka kutahalalishia ugomvi na chama, acha kauli hizi zenye uwewe kaka tafadhali sana.
Natamani nikujue hata jina lako halisi, but mara nyingi watu wenye senteso za aina hii ni wanafiki au pia waweza kuwa ni magamba unataka kugombanisha wanachama kinzani wako.

POLE SANA KWANI UYATARAJIAYO HUTAYAONA KAMWE.
 
eti miss parliament/ Regia
kwa hiyo regia wewe ni nani mpaka uwaamuru watu wahamie kule, kumbe upo humu kwa kazi kama mtumwa wa watu fulani , au unaposema fadhila kwa mbowe na slaa inamaana chama ni kampuni ya mtu, kwa hiyo kama wamekisaidia chama unataka hata wakiwa wanafanya ujinga waachwe tu kwa kuwa wamekifikisha cdm hapa, au kwa kuwa umepewa ubunge viti maalum kwa fadhila ndio maana unalipafadhila sio kosa lako.

JikeDume aka Mchange..Naona umeamua kuning'ang'ania sana.Kwanza kabisa nakupa pole kwa kukosea kuotea,hisia zako umepotea kabisa.Muwe mnatuuliza hivi huwa tunawajuaje baadhi ya watu humu pamoja na kutumia ID za Siri? Pili,Mimi sio Miss Parliament na yawezekana kabisa Miss Parliament sio mwanamke kama mnavyodhani,hilo ni jina tu kama mabvyo wewe unavyojiita jike dume wakati ni mwanaume.Nimefuatilia posts za Miss Parliament kwenye sredi hii ameanza kuchangia saa 10:54 AM wakati huo mimi nilikuwa Bungeni tangu saa tatu asubuhi mpaka saa 7 mchana,amechangia tena saa 11:01AM na saa 12:01 PM mida yote hii nilikuwa Bungeni.Waulize rafiki zako wabunge watakwambia na kwa bahati nzuri hata kama mtu akitumia simu basi post itaonyesha lakini pili simu zangu ni LG hazikamati ndani ya ukumbi wa Bunge.Ni Blackberry pekee ndio zinakamata network ndani ya Bunge. Tatu ninatumia jina moja tu ndani ya Jukwaa hili. Nne,Siwezi kumsema vibaya Zitto tena kwa jina la siri.Kama huna habari Zitto is my closely friend,more than a friend ninauthubutu wa kumwambia ana kwa ana,nimetofautiana naye kwa mengi sana bila kujificha na anatambua hilo.Tano,Kama huna taarifa nilikuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kabisa tulianza kuzungumzia kugombea kwake Urais.Ilikuwa ni mwaka 2007 nikiwa Afisa Vijana niliwahi kumwambia hivyo,he is my fan and he knows that. Sita siwezi kuanza kushabikia move yoyote ya mtu kugombea urais kwani mpaka sasa hakuna ajuaye,it is too early.Dr Slaa hakuwahi kusema wala kuwaza kugombea Urais,Mazingira na hali ya siasa vilimfanya chama kikampendekeza kwa lazima kugombea.Siasa za Tanzania zina dynamics nyingi hivyo sio rahisi kutabiri,ni mapema sana,as a young leader siwezi kujiingiza kwenye mtego huo.Pinda hakuwahi kuwaza kuwa PM leo hii ni PM,Sitta alijiamini kwa asilimia mia moja kuwa atarudi kuwa Spika lakini haikuwa hivyo,Anna Makinda hakufikiria kugombea Uspika lakini hali ya kisiasa imemfanya amekuwa Spika leo.Kwahiyo wapo watakaoonyesha nia leo na wanaweza wasithubutu hata kuchukua fomu na wapo ambao hawana hata ndoto na wanaweza kuchukua fomu na wengine wataukwaa hata Urais.

Saba,wewe na mwenzako msikurupuke na kuanza kuhisi hisi tu bila logic,siwezi kujiita Miss Parliament kwani mi sio Miss Parliament lakini pia kama nikiamua kutumia jina lasiri siwezi kutumia jina ambalo litasababisha watu wanihisi.Iam Smart enough bro!!
Nane,unafahamu fikia kuwa sijapewa Ubunge,Vigezo vilitumika nami niliqualify na pia niligombea Jimbo na nikakizidi kura.Jimbo langu ni la nane kitaifa kwa kuleta kura nyingi kwenye chama. Kama wewe unalipa fadhila za kusaidiwa kwenye uchaguzi basi kivyako.Mwenzako siwiwi wala sidaiwi na yeyote kuhusiana na Ubunge wangu zaidi ya Wananchi wa Kilombero,Morogoro na Tanzania kwa ujumla.

Mwisho nimemfahamu Zitto kabla yako kwahiyo usijafanye wewe ndio unauchungu sana naye.Mtatuacha kama mlivyotukuta.

Nadhani utakuwa umenielewa na siku nyingine jitahidi kutumia japo akili kidogo katika guess kwako.

Karibu Dodoma..
 
Watu wa aina yako ni fedhea kwa chama, huwezi kuwasema watu kwa lugha zenye upoyoyo kiasi hicho.
Unaowasema wako huru kwa majina yao, na wewe uko nyuma ya jina kivuli.

Sijaelewa uwezo wako wa kujiamini mpaka unaejiia mbunge uogope na ufiche jina/ naamini ukiwa mbunge, una uwezo wa kuongea kiundani mambo ya chama, sasa kwa nini unajificha kwa jina kivuli?

Tafadhali usihalalishe makundi ndani ya cdm kwa upayukaji wako huu.

Kama upo kwa kutengeneza makundi, basi uwe wazi pia, wapo watakao kuunga mkono.

Unasababisha viti maalumu wenzio wanadharauliwa kwa namna unavyojiweka kiheroro kwa hoja za makundi.
Nimeona umeandika kuwa wewe ni mbunge, ndio sababu nakunanga uache uzindakoti.

Mkuu kwani kuwa mbunge ni dhambi?mana umesema unamnanga kwa kuwa yeye ni mbunge!mbona unaleta vioja tena badala ya hoja?!

Toa hoja bwana acha kumtisha Miss P yeye katoa maoni yake na wewe toa maoni yako.

Then hoja ya makundi inatoka wapi hapa?lini ww umekua msemaji wa zitto na Kitila? Mana wameonyeshwa hapo juu tayari umekuja juu.
Wenye fikra pevu tumeshajua hii thread imebuniwa na kuletwa hapa kwa lengo maalumu, hiyo haisumbui
 
Umetumwa na NAPE wewe,hatuna mwanachama tahira kama wewe,MBOWE ni mwamba ndani ya chadema,mamluki hamna nafasi ndani ya CHADEMA,Kama mmetumwa na watu wa MAGAMBA imekula kwenu,sisi sasahivi tunafanya kazi usiku na mchana kwa ajiri ya chama huko vijijini kufungua matawi na na kujua na wanachama wapya.
Mtafungua hata mizizi lkn aibu yenu...huyo mbowe form four anawaongoza nn hana hoja zaidi ya kelele...nakumbuka nipo second year zito alitaka kugombea uwenyekiti...mapacha wahttp://www.google.com
 
Mtafungua hata mizizi lkn aibu yenu...huyo mbowe form four anawaongoza nn hana hoja zaidi ya kelele...nakumbuka nipo second year zito alitaka kugombea uwenyekiti...mapacha wahttp://www.google.com

--Wewe na Bill Gate ni hakika wewe ni msomi kuliko Bill gate maana BILL hakumaliza chuo ni UNI DROP OUT
lakini BILL anaongoza kampuni kubwa duniani na amewezesha mimi na wewe tunaweza kuongea kwa PC hii leo
Next time husupige kelele za ELIMU hasa kama umesoma na kufanya kazi TANZANIA
 
Jamaani huyu bibi ananichefua sana,nina fuatilia sana comments zako,hapa na kwingineko,ni aibuuu.. unapenda sana kujikita katika majungu na politics za personallity kuliko kuelekeza mind yako kwenye issues,ideas...yaan unaupenda umaarufu kwa kujitia kihere here eti nawe mwana harakati? u cant win that cheap popularity kwa migongo wa watu,politics has its own principles n u far from them... u are such a idiot political figure in your party and parliement as well. tumia akili katika agenda zako, kama huna akili washirikishe wenzio kina mdee watakusaidia,ask em hw did they survival as a public figure for 5yrs n still adorable?...ok lets say leo ume mu accuse on public (kwa maandishi yasiyo futika) huyu dogo mchange eti ndo dume jike,fine mfano asiwe yeye, una portray image gani kwake yeye na society as whole,mtakaa pa1 nyie kwenye chama kama sio unafiki?...binafsi sikuwahi kufaham kabla ya kua MP wa FREE seat,ila soon after kukufaham nimegundua you are nothin but chewed gum. achana na fitna kwa wabunge wenzio, zitto hata kama ana mapungufu yake lakini ana Qarisma ya kupendwa na watu+Uwezowke wa kujenga hoja,which matters a lot in politics kama hujui,kitu ambacho huna wewe...hebu fuata foot steps basi za ku behave kama wenzio kina owenya,lyimo,mdee,etc hata kama wana falls zao lakini kwenye public wana control midomo zao,funga domo lako tumekuchookaa...be a hero by holding your tongue...
wewe ubunge uliupata kwa kua kwa sababu chama kilipata nafasi ya viti maalumu ambavyo ilibidi vijazwe...
sorry kwa kutoka njee ya maada,but this is emergency case to attend...

JikeDume aka Mchange..Naona umeamua kuning'ang'ania sana.Kwanza kabisa nakupa pole kwa kukosea kuotea,hisia zako umepotea kabisa.Muwe mnatuuliza hivi huwa tunawajuaje baadhi ya watu humu pamoja na kutumia ID za Siri? Pili,Mimi sio Miss Parliament na yawezekana kabisa Miss Parliament sio mwanamke kama mnavyodhani,hilo ni jina tu kama mabvyo wewe unavyojiita jike dume wakati ni mwanaume.Nimefuatilia posts za Miss Parliament kwenye sredi hii ameanza kuchangia saa 10:54 AM wakati huo mimi nilikuwa Bungeni tangu saa tatu asubuhi mpaka saa 7 mchana,amechangia tena saa 11:01AM na saa 12:01 PM mida yote hii nilikuwa Bungeni.Waulize rafiki zako wabunge watakwambia na kwa bahati nzuri hata kama mtu akitumia simu basi post itaonyesha lakini pili simu zangu ni LG hazikamati ndani ya ukumbi wa Bunge.Ni Blackberry pekee ndio zinakamata network ndani ya Bunge. Tatu ninatumia jina moja tu ndani ya Jukwaa hili. Nne,Siwezi kumsema vibaya Zitto tena kwa jina la siri.Kama huna habari Zitto is my closely friend,more than a friend ninauthubutu wa kumwambia ana kwa ana,nimetofautiana naye kwa mengi sana bila kujificha na anatambua hilo.Tano,Kama huna taarifa nilikuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kabisa tulianza kuzungumzia kugombea kwake Urais.Ilikuwa ni mwaka 2007 nikiwa Afisa Vijana niliwahi kumwambia hivyo,he is my fan and he knows that. Sita siwezi kuanza kushabikia move yoyote ya mtu kugombea urais kwani mpaka sasa hakuna ajuaye,it is too early.Dr Slaa hakuwahi kusema wala kuwaza kugombea Urais,Mazingira na hali ya siasa vilimfanya chama kikampendekeza kwa lazima kugombea.Siasa za Tanzania zina dynamics nyingi hivyo sio rahisi kutabiri,ni mapema sana,as a young leader siwezi kujiingiza kwenye mtego huo.Pinda hakuwahi kuwaza kuwa PM leo hii ni PM,Sitta alijiamini kwa asilimia mia moja kuwa atarudi kuwa Spika lakini haikuwa hivyo,Anna Makinda hakufikiria kugombea Uspika lakini hali ya kisiasa imemfanya amekuwa Spika leo.Kwahiyo wapo watakaoonyesha nia leo na wanaweza wasithubutu hata kuchukua fomu na wapo ambao hawana hata ndoto na wanaweza kuchukua fomu na wengine wataukwaa hata Urais.

Saba,wewe na mwenzako msikurupuke na kuanza kuhisi hisi tu bila logic,siwezi kujiita Miss Parliament kwani mi sio Miss Parliament lakini pia kama nikiamua kutumia jina lasiri siwezi kutumia jina ambalo litasababisha watu wanihisi.Iam Smart enough bro!!
Nane,unafahamu fikia kuwa sijapewa Ubunge,Vigezo vilitumika nami niliqualify na pia niligombea Jimbo na nikakizidi kura.Jimbo langu ni la nane kitaifa kwa kuleta kura nyingi kwenye chama. Kama wewe unalipa fadhila za kusaidiwa kwenye uchaguzi basi kivyako.Mwenzako siwiwi wala sidaiwi na yeyote kuhusiana na Ubunge wangu zaidi ya Wananchi wa Kilombero,Morogoro na Tanzania kwa ujumla.

Mwisho nimemfahamu Zitto kabla yako kwahiyo usijafanye wewe ndio unauchungu sana naye.Mtatuacha kama mlivyotukuta.

Nadhani utakuwa umenielewa na siku nyingine jitahidi kutumia japo akili kidogo katika guess kwako.

Karibu Dodoma..
 
Time for commercial break
10za352.jpg
 
Mbowe ndiye tatizo kwa cdm, mnaona jamaa anavyowamaliza wanaompinga, eti kisa anataka aendelee kufanya biashara ndani ya cdm, mnakumbuka magari yake analazimisha atuuzie, anawaondoa wote wanaomkosoa, anawatumia watu tu, wakishamfanikisha anawatupa kama cond..m,huyu jamaa hafai nasikia anataka kuggombea urais ndio maana anafanya mbwmbwe sana na kuwahujumu wenzake,mbowe huna sifa ya kuwa rais wa nchi hii, hata moshi mjini unayotaka ukagombee ubunge utaabika kabisa.

Unataka ww uwe juu tu kuliko wengine na huna uimara wa kufikiri, kumbuka ulivyoropoka kwenye bajeti baada ya kikao cha bunge, sikia ulivyoropoka kuhusu madiwani arusha, halafu leo unakuja na ujinga wa kuwakana, nimeongea na wanachama wengi sana wamenipa huu ujumbe nikupe, kama ukimeza wembe umezs tu, hasa huku visiwani hutakiwi kuja kabisa shaurilo ukijipendekeza utaokona.
haya kwa uchaguzi wa cdm 2013 labda uuairishe eti, vinginevyo utaanguka na utashangaa.

Tunamkumbuka chacha wangwe sana, tunammis sana msema ukweli wetu sie, kwa nini unagombana na kila mtume ajaye cdm akiwa hakubaliani na wewe mbaba? wewe ni tatizo.

Unasutwa sana na tarehe uliyojiunga hapa JF. Anyway umefanya kazi yako tayari wahi Lumumba ofisini kwa Nape ukavute posho!!!

Tiba
 
Mbunge yoyote wa Chadema atakaekuja hapa akatupa maneno kapu tele kuwa yeye ni loyal sana kwa Zitto na hajawahi kwenda kinyume nae atakuwa anajidanganya tu. Sio nyie mlompigia kura ya kutokuwa na imani nae nyuma ya mgongo wake!

Baada ya kuji-proud kuwa unatumia ID nyengine miezi kadhaa nyuma, inachekesha kuona mtu anathubutu kusema hana ID nyengine.

Ukiwa muongo usiwe msahaulifu
 
Regia umenikosha sana kwa ku do the needful kwa yue bata. Kaza buti mama tunakuamini na tunajua unaweza. Achana na wapuuzi wafitinishaji
 
WARAKA WA CHACHA WANGWE.


UTANGULIZI.



Jumamosi, June 28 mwaka huu wajumbe kadhaa wa Kamati Kuu ya CHADEMA walidai kuwa wamesitisha Umakau Mwenyekiti wangu katika kikao kilichofanyika mjini Dodoma siku hiyo. Kesho yake Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe. FREEMAN MBOWE akaitisha mkutano wa waandishi wa habari na kutaja sababu za kunisimamisha uongozi.

Inatosha tu kusema kuwa sababu zote alizotoa ni za uzushi kama ile inayodai kuwa mimi navujisha siri za chama kwa viongozi wa CCM bila hata kutaja siri hizo, au kusema nimezitoa lini, wapi, na kwa kiongozi yupi?Kikao hicho kinachosemekana kunisimamisha uongozi, kilikuwa na wajumbe 31 ambao takribani nusu hawakuwa na uhalali wa kupiga kura kinyume cha katiba na kanuni za CHADEMA kwa vile walikuwa wameandaliwa kwa kazi hiyo. Wajumbe 7 walikataa kushiriki njama hizo.

Kufuatia jaribio hilo la kunivua uongozi kutokubalika kwa wanachama walio wengi wa CHADEMA , Mwenyekiti MBOWE na wafuasi wake wameendelea kuhaha kwa kuongeza sababu nyingine mbalimbali ili kuhalalisha njama zao. Sasa hivi wameingia hatua ya kuwashawishi wanachama wa Tarime eti wanifukuze uanachama.Kwa kuzingatia katiba, kanuni na taratibu za CHADEMA, nilichokifanya mimi baada ya kubaini njama zao ni kukata rufaa kwa Baraza Kuu la Chama, kupinga upotoshaji unaofanywa chini ya uongozi wa Mhe. MBOWE anayeonekana kutaka kuendesha chama kinyume na matarajio ya wanachama walio wengi.Hivyo basi zipo habari za uhakika kuwa kikao hicho cha Baraza Kuu hakitaitishwa ama kabisa, au kitacheleweshwa kwa makusudi, kwa visingizio mbalimbali ikiwemo kutokuwa na fedha za kukidhi gharama za kikao hicho.

Naomba nikiri kuwa ninakerwa sana na mtiririko mzima wa sakata hili linalozua mgogoro unaokiyumbisha chama. Ukweli ni kwamba mimi niligombea Umakamu Mwenyekiti nikiwa na agenda ya kufufua uhai wa chama kwa kukaripia vitendo visivyostahili katika kuendesha chama. Agenda yangu haijabadilika. Yote niliyoyasema wakati nagombea nafasi hii yanafahamika kwa wana CHADEMA wote.

Walikuwepo walioyalalamikia na walikuwepo walioyapongeza matamshi yangu hayo.Mwisho wa yote wana CHADEMA waliridhika kuwa ajenda yangu ilikuwa sahihi na hivyo wakanichagua kuwa Makamu Mwenyekiti. Hivyo basi hata kama ni kweli kuwa ulikuwepo mvutano wakati wa kampeni ile, lakini hilo ni jambo la kawaida katika uchaguzi. Nijuavyo mimi hayo yalitakiwa yawe si ndwele nasi tugange yajayo kwani wanachama walikwisha fanya uamuzi halali kupitia kura zao.

Baada ya kuingia kwenye wadhifa wa Makamu Mwenyekiti Taifa, nilifanikiwa kuzungumza na Mhe. MBOWE kuhusu mambo, hususan yale, niliyoyapigania wakati wa kinyang?anyiro kile na kumuomba tukae chini na kutafuta jinsi ya kufanikisha azma hiyo.Ni imani yangu kuwa waraka huu utawasaidia wanaCHADEMA wenzangu na watanzania wote kwa ujumla, kuelewa vizuri ukweli wa mambo niliyoyapigania kabla ya kuwa Makamu Mwenyekiti, na ninayoendelea kuyasimamia hivi sasa nikiwa Makamu Mwenyekiti, na inshallah nitakayoyatekeleza baadae kama Taifa Mwenyekiti wa CHADEMA.

Kimsingi mambo tunayotofautiana na Mhe. MBOWE ni haya yafuatayo:-

MATUMIZI YA RUZUKU
CHADEMA hupata ruzuku ya Tshs. 66,000,000 kwa mwezi (Milioni sitini na sita). Mimi nasema si haba hasa tukizingatia chama kilikotoka. Naamini kuwa kiasi hiki cha fedha kikisimamiwa vizuri kinaweza kukirahisishia chama kujieneza katika ngazi zote toka Tawi, Wilaya, Mkoa na Taifa.

Si kweli kwamba matatizo yote yatamalizwa na fedha hizi lakini basi hata ofisi za chama zinaweza kuwa hai nchi nzima kitu ambacho kwa sasa hakipo. Mahesabu yanaonesha kuwa mtaji wa laki moja (Tshs.100,000/=) kwa wilaya moja nchini inatosha, hivyo kwa Wilaya 126 kwa mwezi jumla yake ni Tshs. milioni 12 (Tshs. 12,600,000/= ) zinahitajika ( Wilaya 126 x 100,000 kila wilaya = 12,000,000/=)Hata tukisema tupeleke kiasi hicho kwa kila jimbo la uchaguzi jumla yake ni Tshs. Milioni 23 (Tshs. 23,000,000/=) kwa maana ya majimbo 213 x 100,000 = 23,000,000/=.
Mhe. MBOWE anasema hizo ni pesa nyingi sana kwa uimarishaji wa chama. Mimi nasema hapana, kiwango hiki kwa kila Wilaya au Jimbo la uchaguzi ni muafaka kwani haba na haba hujaza kibaba.Chini ya uongozi wa Mhe. MBOWE na wafuasi wake hawastaajabu kuwa kati ya Tshs. 374,144,000.40 zilizopatikana kama ruzuku katika ya Januari 1 na Juni, 30, 2008, Tshs. 350,000,000/= zilitumika Makao Makuu ya CHADEMA na Tshs. 25,000,000/= tu ndizo zilikwenda Wilayani kuimarisha chama.Mimi naona mgao huu unayatukuza Makao Makuu ya
CHADEMA isivyostahili wakati huo huo ukidhalilisha chama nchi nzima.


MADENI YA UCHAGUZI

Kufuatia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, Mhe. MBOWE alitufahamisha wanachama kuwa alikuwa anakidai chama US $ 181,949.00 sawa na Tshs. 218,338,546. Mpaka sasa chama kimekwisha mlipa Tshs. 175,000,000/=Baada ya kupata wadhifa wa Makamu Mwenyekiti, na kwa kuzingatia takwimu zionekanazo hapo juu katika kulinganisha matumizi ya fedha Wilayani na Makao Makuu niliamua kumshauri MBOWE asitishe kujilipa deni kutokana na fedha za ruzuku kwani siamini kuwa kulipa madeni yaliyopita kunaendana na utaratibu wa usimamizi wa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa toka serikalini.

Mhe. MBOWE alichachamaa na ndipo nilipomshauri kuwa kama ni hivyo basi atuthibishie pesa hizo anazodai alikikopesha chama ziliingia kwenye akaunti gani ya CHADEMA, kupitia hundi ipi, na lini? Nilimuomba pia kutaja ni kikao gani cha chama kiliidhinisha matumizi ya fedha hizo kwani kama hakuna ushahidi wa maidhinisho, ni dhahiri kuwa matumizi hayo hayakudhibitiwa na chama na kwa mantiki hiyo kuyafanya kuwa matumizi binafsi ya Mhe. MBOWE.Vilevile, nilimueleza kuwa matumizi ya fedha hizo alizodai alikikopesha chama yalikuwa yakinuka harufu ya UFISADI.

Stakabadhi zote kuhusiana na matumizi hayo zilionesha kuwa gharama za aidha ununuzi na / au ukodishaji wa vifaa hivyo, hazikutofautiana na viwango wanavyolipishwa watalii kwa huduma kama hizo, kwa maana ya gharama ya juu sana.Na kwa kuwa hata baada ya kuwa Mhe. MBOWE amekwisha lipwa zaidi ya nusu ya deni alilodai kuikopehsa CHADEMA, vifaa vyote yakiwemo magari, vipaza sauti na kadhalika vimebakia kuwa mali yake binafsi, basi bila kumficha nilimueleza kuwa huko ni kukinyonya chama kwa kukigeuza kitega uchumi cha watu binafsi.Kuhusu suala la kulipa madeni kupitia ruzuku ya serikali, nilimuomba Mhe. MBOWE afuatilie kwa Msajili wa Vyama vya siasa ili tupate ufafanuzi kama kweli fedha za ruzuku ya serikali kwa vyama vya siasa, inaweza kutumika kulipia madeni ya viongozi wa vyama hivyo yatokanayo na uchaguzi ili CHADEMA isiathirike kisheria.

Niseme kweli hapa kwamba, kwa vile wanaCHADEMA wengi walinichagua kuwa Makamu Mwenyekiti, na hata mimi mwenyewe tulikuwa wagombea wa nafasi za ubunge, udiwani n.k katika uchaguzi wa mwaka 2005 ningefarijika sana iwapo na sisi tungerejeshewa angalau chochote cha kufidia gharama zetu, kwa maana kwamba kama chama kimeamua kurudisha gharama hizo kiwalipe wote badala ya kulipa madeni kwa wateule wachache.

UTEUZI WA WABUNGE WA VITI MAALUM


Naamini ukweli wa suala hili hauna mjadala. Kwamba Mhe. MBOWE na wafuasi wake walighushi orodha ya majina ya viti Maalum badala ya kupeleka yaliyopendekezwa na Kamati Kuu sio siri.


Naamini hata Mhe. MBOWE anakubaliana nami kuwa suala hili si moja ya siri anazodai nimevujisha! Yamesemwa mengi juu ya mtafaruku uliojitokeza kuhusu viti maalum hadi baadhi ya waasisi wa chama wakataka kujitoa na hivyo kumlazimisha Mwenyekiti Taifa ( FREEMN MBOWE) na Katibu Mkuu (DR WILBROAD SLAA) kukiomba radhi kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kwa kukiuka katiba, kanuni na maadili ya chama katika suala hili la kugushi viti maalum.

Ni ukweli ulio wazi kuwa kitendo hicho cha upendeleo bado kina iumiza taswira ya CHADEMA. Chama kinaonekana kuendekeza ujanja ujanja kiasi kwamba watu na binti zao, wakwe zao, shemeji zao, waume wenzao, wachumba wa shemeji zao, wake wenza na kwa kiwango kikubwa watu wa kabila moja ndiyo wamekuwa sura ya CHADEMA bungeni.Katika hili nilichoweza kumueleza Mhe. MBOWE ni kuwa chaguzi mbalimbali tangu za Mitaa, Ubunge na Urais zinakaribia ni vizuri tufanye bidii kusambaza nguvu zetu nchi nzima tuwe na mtaji wa kura maeneo mengi ili kashfa kama hii isijirudie. Hii ni kwa msingi kuwa chama kikijitanua kutakuwa hakuna sababu ya kuwaona watu wa eneo fulani tu kuwa ndiyo mhimili wa CHADEMA na hivyo zikitokea fursa itakuwa rahisi chama kuwakilishwa na mtandao wake mpana badala ya koo au kabila fulani.Sasa kwa kuwa kuimarisha chama kitaifa maana yake ni matumizi ya fedha, nalo hili likawa nongwa ingawa kwa mtazamo wa Makao Makuu kulipa madeni kwa wateule wachache si nongwa.

Cha ajabu ni kwamba Mhe. MBOWE hakukana kuwa hili la viti maalum na hata upangaji wa ajira kwa ukabila una leta athari mbaya kwa mustakabali wa CHADEMA

Katika maongezi yangu nae nilikuwa wazi nilipotahadharisha kuwa:

1. Watanzania wakiendelea kuona kwamba CHADEMA inaendeshwa kwa misingi ya kikabila hawatajiunga na chama chetu na tutakosa wafuasi.


2. Watanzania wakiona kuwa sisi tumeweka mbele ukabila kuliko utaifa hawatatupa madaraka na kutawala kwa kuhofia yale yanayotokea nchi jirani kama Rwanda, Burundi, Kenya na kadhalika ambako nafasi za raia wote zimehodhiwa na kabila moja na hatma yake watu wamechinjana kama kuku kwa kupinga hilo.


Pia nilimwambia kwamba, kwa jinsi sura ya uteuzi wa Wakurugenzi na watendaji wengine wa Makao Makuu inavyoonekana, sasa tayari chama chetu kimebatizwa jina la CHAMA CHA WACHAGA, na hii si kuwatendea haki raia wengine na makabila yao ambao wataonekana kama punguani kujihusisha na chama na ukabila.Yote haya ninayosema kuhusu ukabila, upendeleo na kadhalika sio dhana tu. Kufuatia malalamiko mengi yaliyokuwa yakisikika nchi nzima kuhusu masuala haya, Kamati Kuu ya CHADEMA ilikwisha unda Tume kutafuta ukweli wa mambo hayo. Tume hiyo ya watu watano iliongozwa na Mhe. Merky Lugendo Mziray ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA nayo imekwisha toa taarifa yake kwamba Makao Makuu ya CHADEMA yanatawaliwa na ubaguzi wa kikabila, kidini na kielimu.


UTENDAJI WA KIBABE
CHADEMA ni chama kilicho njia panda kwa sasa kutokana na utendaji wa kibabe wa Mhe. MBOWE. Ninafahamu jinsi vyama vingine vya upinzani hapa nchini kama vile NCCR ? Mageuzi vilivyoporomoka haraka haraka mithili ya nyumba ya mabua. Chama NCCR ? Mageuzi kilifikia mahali pazuri tu hadi watu wakaanza kufikiria kuwa kingekuwa chama mbadala kwa CCM.



kwa bahati mbaya uchu wa madaraka, ulafi wa ruzuku, na tabia za kimangimeza kwa pamoja vikakiathiri hadi kupoteza umaarufu wake.Na hata vyama vingine vya upinzani vina dalili hizo hizo japo kwa viwango vinavyotofautiana. Ila badala ya kujichunguza na kujua kasoro zetu, kila siku vyama vyetu, vimekuwa vikidai kuwa ni chama tawala ndicho kinachoviroga, kama ambavyo Mhe. MBOWE ameanza kuweweseka kupitia vyombo vya habari.Napenda kuthibitisha kuwa katika mgogoro unaopaliliwa sasa na Mhe. MBOWE ndani ya CHADEMA kutokana na ufisadi, ufuska, ulevi wa madaraka na umangimeza chanzo chake ni tabia yake ya kuendesha chama kibabe. Mathalan kumzuia Martin Mung?ong?o Mkurugenzi aliyechaguliwa kwa kura kutofanya kazi zake ndani ya chama, madai ya kupigana na watendaji wa chama ndani ya baa na vitendo vingine vya aina hiyo ni ushahidi tosha wa hulka hii.

Hadi sasa Mhe. MBOWE amefanikiwa kukizuia chama hiki kisifanye kazi ya siasa mkoa wa Dar es salaam kwa miaka minne.Ninavyoongea hivi sasa CHADEMA imekuwa ikikimbia vikao vya Democratic Union of Afrika (DUA), Muungano wa Vyama Vya Upinzani, uliofanikisha CHADEMA kujuana na Conservative Party ya Uingereza na Republican ya Marekani. Vyama dada hivi vyote vinaulalamikia uongozi wa CHADEMA kwa kufuja fedha ya misaada na kuwasilisha kwao risiti za kugushi, kama ilivyofanyiwa Conservative Party baada ya kutoa msaada wa Tshs. 78,000,000 kwa ajili ya ununuzi wa baiskeli na pikipiki ambazo hazikununuliwa.Katika mkutano wa Kamati Kuu ya CHADEMA huko Dodoma hivi majuzi tu, Mhe. MBOWE kwa kauli yake aliwatisha wajumbe kuwa alikuwa amethibiti uwezekano wowote wa wajumbe kujisikia huru kwa kutoa mawazo ambayo yangepingana na ajenda yake aliyoitoa ghafla kikaoni kunisimamisha Umakamu Mwenyekiti.




Mhe. MBOWE Alikifahamisha kikao kuwa alitoa taarifa kwa IGP, SAID MWEMA kuwa kuna wahuni ambao walitaka kuuchafua mkutano wake, naye IGP akahakikisha kuwa mkutano ule unalindwa kwa kiwango cha kushtua kama ambavyo hata vyombo vya habari vimethibitisha.Hayo ni baadhi tu ya mambo yanayobainisha Mhe. MBOWE ni kiongozi wa aina gani.

HITIMISHO
Kama nilivyokwisha sema hapo awali, sijaacha na sintoacha ajenda yangu ya kufufua uhai wa CHADEMA kwani ndiyo ahadi iliyofanikisha kuchaguliwa kwangu kuwa Makamu Mwenyekiti Taifa. Nilipopata wadhifa huo nilianza kuitekeleza ajenda hiyo kupitia mahojiano na Mwenyekiti MBOWE kuhusu matumizi ya ruzuku, madeni ya uchaguzi, uteuzi wa wabunge wa viti maalum, nafasi za ajira Makao Makuu, na kuhusu mwenendo wa chama Mkoa wa Dar es salaam.

Nilijikuta katika mvutano mkubwa kila nilipogusa eneo lolote katika haya. Nakiri kuwa kwa kiwango kikubwa sikuwa na uwezo wa kubadili mambo hayo yaliyokuwa yakiratibiwa kwa ukaribu na Mhe. MBOWE na wafuasi wake kwani sikupewa ushirikiano wa aina yoyote na chama pale Makao Makuu.




Ni vigumu kuamini, lakini ni kweli kuwa sikuwa na ofisi Makao Makuu, sikupewa vitendea kazi kama magari, vipaza sauti na/au vyombo vya habari, na sikuwahi kupata taarifa yoyote ya kiutendaji toka Makao Makuu.Kwa kuzingatia yote hayo, naomba nichukue fursa hii kuwashukuru kwa dhati wanachama wa CHADEMA mkoa wa Dar es salaam ambao kwa pamoja tulisimama kidete kufufua uhai wa chama hapa jijini. Niseme tu ushirikiano wao wa hali na mali uliniwezesha kushughulikia masuala muhimu ya kitaifa na kimataifa.


Rai yangu kwa wana CHADEMA na wale wote wanaokitakia mema chama chetu na nchi yetu kwa ujumla ni kwamba kazi ya kupigania demokrasia ya kweli ndani na nje ya chama, kukiepusha chama na vitendo vya ukabila, migogoro,


ubadhirifu, umangimeza, ufisadi na ubaguzi wa aina yoyote bado inaendelea na nawaombeni mniunge mkono kwa hali na mali katika vita hii. Naamini tutashinda.Mungu Ibariki CHADEMA Mungu Ibariki TANZANIA Mungu Ibariki AFRIKA
 
Mwenyekiti wa chama aliekaa miaka mingi kuliko hata nyerere, mlafi wa madaraka.kwanini hio nafasi awaachii na wengine????
Tanzania hakuna chama kitakacholeta uhuru wa kweli!!! Naona ni vikundi vya ufisadi tu
 
Jina lake jingine ni MUGABE. Huu ni mwaka wa 14 akiwa kiongozi mkuu wa chama. Mtoto aliyezaliwa 2004 mwaka huu yupo kidato cha kwanza.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom